Tuesday, January 22, 2013

MH. DK. HARRISON MWAKYEMBE AMEWAFUKUZA KAZI WATUMISHI WAWILI BANDARI



Waziri wa Uchukuzi Dokta HARRISON MWAKYEMBE amewaafukuza kazi EPHRAIM MGAWE, na Naibu wake Bwana JULIUS MFUKO kufuatia ripoti iliyotolewa na tume maalum ya kuchunguza hali ya uendeshwaji wa bandari hiyo na kuonyesha kuwa watendaji hao wamekosa umakini pamoja na kufanya uzembe uliopitiliza.
Akisoma ripoti hiyo Dokta MWAKYEMBE amesema kuwa Viongozi hao wameshindwa kuonyesha umaridadi wa kuisimamia bandari hiyo, hali iliyopelekea kuisababishia Hasara kubwa Serikali sambamba na kushusha hadhi ya Bandari ya Dar es Salaam, hadi kufikia hatua ya kutajwa kama Bandari isiyoingiza faida yoyote miongoni mwa Bandari 36 za barani Afrka.
Katika Hatua nyingine Dokta MWAKYEMBE ametangaza kuwafukuza kazi Meneja Mkuu wa Bandari hiyo KASSIAN NGAMILO pamoja na Meneja wa kitengo cha Mafuta CAPTAIN TUMAINI MASSAWE, kufuatia kushindwa kusimamia ipasavyo mikataba mbalimbali ya uondoshaji wa mafuta machafu bandari hapo sambamba na uzembe uliopitiliza.
Hata hivyo Dokta MWAKYEMBE amebainisha kuwa Wizara yake haitamvumilia mtendaji yeyote kutoka idara ama taasisi iliyo chini ya Wizara hiyo ambaye utendaji wake utaonekana kulega lega, na kusabaisha Serikali kupata hasara pasipo sababu za Msingi.
Kufukuzwa kwa Viongozi hao ni miongoni mwa utekeleza wa uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam ambayo imeshika nafasi ya Mwisho kwa uingizaji faida katika Bandari 36 za Bara la Afrika hii ni ikiwa ni Ripoti iliyotolewa hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment