Wednesday, January 9, 2013

SIKUHUDHURIA MAZISHI YA SAJUKI KWA SABABU NILIKUWA BIZE STUDIO NIKIREKODI WIMBO WANGU"....WEMA SEPETU



Msanii anayefanya sanaa ya Uwigizaji hapa Nchini maarufu kwa jina la Wema Isaack Sepetu inasadikika kuwa hakuonekena kwenya Mazishi ya marehemu Juma Issa Kilowoko au maarufu kama Sajuki yaliyo fanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam siku ya tarehe 4 Januari mwaka huu.

Tukio hilo lilizua minong'ono kutoka kwa mashabiki wake pamoja na mastaa wenzake ambapo walishangazwa na Wema kutokuwepo msibani....

Meneja wa Wema Sepetu ambaye ni Bwana Martin Kadinda alisema kuwa sababu iliyomfanya mwanadada Wema kushindwa kufika msibani ni kuwa siku ambayo marehemu Sajuki anafariki dada yake na Wema nae alikuwa amejifungua Mtoto.

Pia alidai kuwa siku ambayo Sajuki anazikwa Wema alikuwa Studio akirekodi ngoma yake mpya ambayo anatarajia kuitoa mwanzoni mwa mwaka huu ili na yeye ajiweke sawa katika tasnia hii ya muziki wa kizazi kipya.


Source:THE SUPER STARS

No comments:

Post a Comment