Wednesday, December 18, 2013

Kansiime Anne Profile: Get to know the real me

12 MAHAKAMANI KWA UKEKETAJI SAME

Wanawake 12 ambao ni wazazi wa wasichana 21 waliofanyiwa ukeketaji wilayani Same, mkoa wa Kilimanjaro, kaskazini mwa Tanzania, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Same, wakati waliposomewa mashitaka yao kwa mara ya kwanza tangu wakamatwe mwishoni mwa wiki iliyopita.
Watuhumiwa wote wanashitakiwa kwa kosa la Ukatili dhidi ya watoto na kuwasababisha maumivu makali, shitaka ambalo wote wamekana.
Tisa kati ya watuhumiwa hao 12 wameachiliwa kwa dhamana, huku watatu wakibaki mahabusu kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni shilingi milioni mbili za Tanzania, sawa na dola 1250 za Kimarekani.
Miongoni mwa washitakiwa, mmoja alikabiliwa na mashitaka mawili, moja akiwa mzazi wa mmoja wa wasichana waliokeketwa na pia akiwa ngariba.
Kutokana na mila na desturi ya baadhi ya makabila nchini Tanzania, ukeketaji unafanyika japo ni kinyume cha sheria, huku watu wanaokamatwa kuhusika na ukeketaji wakichukuliwa hatua za kisheria.
Kama watapatikana na hatia, wanawake hao wanakabiliwa na kifungo kisichopungua miaka mitano jela au kutozwa faini kubwa.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 30 Desemba 2013, wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.


Habari kwa hisani ya BBC Swahili

Waliokufa Sudan Kusini ni '400 - 500'


Mamia ya watu wanaaminika kufa wakati wa mapigano baina ya majeshi ya yanayomuunga mkono rais wa Sudan Kusini na yale yanayomuunga mkono makamu wa rais, maafisa wa Umoja wa Mataifa waliopo Sudan Kusini wamesema baada ya kunukuu ripoti ambayo bado haijathibitishwa..
Wanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa wamesema wameambiwa na vyanzo vya habari katika mji wa Juba kwamba idadi ya watu waliokufa wanaweza kufikia 400 hadi 500.
Sudan Kusini imekuwa na mapigano ya siku mbili kufuatia taarifa kwamba kulikuwa na jaribio la kumpindua rais Salva Kiir.
Mwanasiasa wa upinzani aliyeko uhamishoni Riek Machar amekana madai ya serikali kuwa alijaribu kufanya jaribio hilo.
"Kilichotokea Juba ni kutokuelewana na mgawanyiko baina ya vikosi vya ulinzi vya rais, sio jaribio la mapinduzi," aliiambia Sudan Tribuni, tovuti yenye makao yake Paris katika mahojiano yaliyochapishwa siku ya jumatano.
Bwana Machar Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan Kusini ambaye aliondolewa na rais Kiir mwezi Julai, amesema hana taarifa wala hausiki kwa namna yoyote na jaribio hilo la mapinduzi.
Rais wa Sudan Kusin Salva Kiir amesema kundi la wanajeshi wanaomuunga mkono makamu wa rais Machar walikuwa wakijaribu kujitwalia madaraka kwa kwa nguvu siku ya Jumapilil usiku, lakini walishindwa.
Wakati mapigano yanaendelea siku ya jumatatu na jumanne, serikali imesema wanasiasa kumi maarufu akiwemo waziri wa zamani wa fedha, wametiwa mbaroni.
Taarifa za mapigano hayo zimefika kwenye baraza la kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York siku ya jumanne, ambapo limesema mapigano hayo yanaweza kuwa mapingano ya kikabila.


Mkasi - SO7E11 With Muumin Mwinjuma