Monday, April 14, 2014

DARAJA LA MTO MZINGA NA KONGOWE KIGAMBONI LAHARIBIKA VIBAYA

Kutokana na mvua kubwa zilizonyesha siku ya jumamosi na jumapili zimeleta athari kubwa kwa wakazi mbalimbali wa jiji la Dar es salaam,ambapo miundombinu na makaazi ya watu yameathiriwa vibaya na mvua hizo na kuacha baadhi ya familia kupoteza ndugu zao na kukatisha usafiri kutoka eneo moja kwenda jingine.
Hili nililishuhudia jana eneo la Mbagala(Darajani mzinga)ambapo jana asubuhi daraja hili lilikuwa linapitika kwa waenda kwa miguu peke yake na kuacha magari na bodaboda kubaki upande uliokuwepo .Pichani ni baadhi ya sehemu hizo korofi.

Wakazi wa Kongowe wakiangalia maafa yaliyoletwa na Mvua hizo

Roli Kubwa la Mafuta lililotumbikia likijaribu kuvuka kwenye Daraja hilo la Kongowe likitokea Kigamboni

Sehemu ia daraja iliyoondolewa na maji


Wananchi wakijaribu kuvuka kwenda upande wa pili wa daraja baada ya maji ya mto kupungua


Add caption


Kibao kikionyesha kuwa barabara hiyo imefungwa kwa muda


Hapa ni Darajani Mzinga sehemu yalipokuwa yakihifadhiwa mabomba ya gesi

Wachina waliokuwa wakiishi eneo hilo wakiokoa vitu vyao


Jinsi kulivyokuwa kukionekana


Mto Mzinga Umefurika


Umati wa watu wakijaribu kuvuka 

Umati wa watu wakijaribu kuvuka


Daraja limefungwa na wananchi wanapita kwa zamu upande mmoja




No comments:

Post a Comment