Saturday, September 20, 2014

Uhuru Kenyatta atakiwa mahakamani ICC 8,Octoba


Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imemtaka raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta kufika mahakamani tarehe 8 mwezi Oktoba licha ya majaji wanaotarajiwa kusikiliza kesi dhidi yake kuiahirisha.
majaji katika mahakama hiyo wanataka kumhoji juu ya madai kwamba serikali yake imeficha hati iliyoombwa na waendesha mashitaka wanaosikiliza kesi yake ya uhalifu dhidi ya ubinadamu.
Kesi hii imekuwa ikicheleweshwa mara kadhaa sasa.hata hivyo raisi kenyata amekanusha kuandaa mauaji ya kikabila baada ya uchaguzi mwaka 2007.
Takribani watu elfu moja mia mbili waliuawa na laki sita kuyakimbia makazi yao.

Wiki mbili zilizopita, waendesha mashitaka waliomba kesi dhidi yake kuahirishwa kwa muda usiojulikana, kwa vile hawakuwa na ushahidi wa kutosha kwa sababu ya serikali ya Kenya kuweka vizuizi.

No comments:

Post a Comment