Friday, March 7, 2014

MTOTO WA GADDAFI,SAADI ASHIKILIWA LIBYA


Serikali ya Libya imesema kuwa mtoto wa Kiongozi wa zamani wa nchi hiyo, Saadi Gaddafi, ameondoshwa nchini Niger hivi sasa anashikiliwa mjini Tripoli.
Saadi alitoroka baada ya baba yake, Kanali Muammar Gaddafi kuuawa wakati wa mapinduzi yaliyofanyika mwaka 2011 nchini Libya.
Anashutumiwa kuwafyatulia risasi waandamanaji na anadaiwa kutekeleza uhalifu mwingine wakati wa utawala wa baba yake, yeye alipokuwa Kiongozi wa vikosi maalum vya kijeshi.
Serikali ya Libya imetoa taarifa hiyo mapema siku ya alhamisi kuwa wamempokea akitokea Niger.

awali , Niger ilikataa ombi la Libya ilipotaka imsafirishe Saadi, huku waziri wa sheria wa Niger akihofu kuwa Saadi atahukumiwa adhabu ya kifo.

MALARIA YAWA UGONJWA HATARI ZAIDI

Watafiti kutoka Uingereza na Marekani wanasema kuwa mabadiliko ya hali ya hewa huenda yakazua ongezeko kubwa la maambukizi ya ugonjwa wa Malaria kote duniani huku ugonjwa huo ukienea katika maeneo ya milimani barani Afrika na Amerika ya Kusini.
Katika matokeo ya utafiti yaliyochapishwa kwenye jarida la Science, wanasayansi hao wanasema hata ongezeko dogo katika viwango vya joto siku za usoni huenda likaongeza kwa mamilioni maambukizi ya malaria.

Mbu anayesababisha malaria.
Watafiti wamepata ushahidi kwamba mbu anayebeba kimelea kinachosababisha malaria wanaelekea katika nyanda za juu wakati viwango vya joto vikipanda.
Watu wanaoishi katika maeneo ya nyanda za juu wanakosa kinga na hivyo kurahisisha maradhi ya malaria kuenea.
Takriban watu milioni mia mbili ishirini kote duniani huambukizwa ukonjwa wa malaria.


Mbu aneyesababisha malaria

Thursday, March 6, 2014

Mkasi - SO8E08 With Inspector Haroun

FOLENI KUBWA MBAGALA MZINGA DARAJANI JANA




Jana Jioni majira ya saa kumi na mbili jioni nilikuwa naelekea maeneo ya Mbagala Kongowe nikakutana na foleni kubwa sana ambayo ilisababishwa na ubovu wa barabara pamoja na magari kutofuata taratibu na sheria barabarani.nilikuwa kwenye bodaboda lakini ilinichuku kama dk 15 hivi kupita kwenye daraja hili kwa jinsi magari yalivyokaa vibaya na kusababisha kufunga njia.
Angalia baadhi ya picha nilizochukua nikiwa kwenye eneo hilo.

hakuna pa kutokea

Hizi ni baadhi ya bodaboda zikiwa kwenye foleni