Saturday, November 29, 2014

TAZAMA RATIBA YA LIGI KUU UINGEREZA LEO


KUTOKA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII





Tibaijuka:"Nilipokea pesa za Escrow"

Mjadala kuhusu kashfa ya uchotaji wa mamilioni ya fedha katika akaunti ya ESCROW ya Benki Kuu ya Tanzania umezidi kuunguruma nchini Tanzania kufuatia taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, PAC, na ripoti ya serikali kuhusu kashafa hiyo.
Mambo yaliyojitokeza katika ripoti ya PAC ni kutaja majina ya viongozi na maafisa wandamizi wa serikali walionufaika na magao huo.
Miongoni mwao ni waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka ambaye alizungumza na mwandishi wetu mjini Dodoma, Ben Mwang'onda ambaye alianza kwa kumuuliza kama kutajwa kwa jina lake alitendewa                                                                              haki


Source:BBC Swahili

VIOJA VYA MAKONDA WA DALADALA



KERO BARABARA YA MBOZI CHANG'OMBE

Hii imekuwa kero sasa kwa watumiaji wa barabara ya Mbozi,Chang'ombe viwandani,
Imekuwa ni kama tabia ya kawaida kuwepo kwa mabwawa makubwa ya maji katika eneo maarufu la kilipokuwa kiwanda cha kutengeneza biskuti,
Chakushangaza ni kuwa barabara hiyo inatumiwa na viwanda vikubwa vilivopo katika eneo hilo
kama Azam,Konyagi,Kioo na vingine vingi ambavyo hatujavitaja.
Inasikitisha maana hata wafanyakazi wa viwanda hivyo pia ni waathirika wa tatizo hilo .
Wito wetu mamlaka inayohusika shughulikieni jambo hili ili kutatua kero hiyo.

Bwawa kubwa la maji machafu

Ni shida hata jinsi ya kuvuka kufika upande wa pili

Ona waenda kwa miguu wanavyopata shida kuvuka

baada ya kujaribu kuvuka gari hii ilinasa

Wasamalia wema wakienda kutoa msaada


Foleni ya magari yakisubiri kuvuka



Tuesday, November 11, 2014

MGOGORO WA KANISA LA MORAVIA JIMBO LA KUSINI MAGHARIBI WAIBUKA UPYA OFISI ZA MAKAO MAKUU JIMBO ZAFUNGWA KWA MINYORORO

Baadhi ya Wachungaji na Waumini wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Oktoba 10 majira ya saa 11 jioni walifunga ofisi zote za Makao makuu ya Kanisa hilo zilizopo Jacaranda Jijini Mbeya na kumzuia aliyekuwa Mwenyekiti wa Jimbo Mchungaji Nosigwe Buya kuhama kwenye eneo hilo kwenda nyumba nyingine eneo la Saba saba.

Aliyeyeongoza zoezi hilo ni pamoja na Frank Phili Mtunza hazina wa Kanisa la Moravian Ushirika wa Bethelehem ulioko Mama John Jijini Mbeya akiwa na Mchungaji Mwilgumo pamoja na Mchungaji Mwakyoma.

Ofisi zilzofungwa kwa kutumia minyoro na mbao ni pamoja na ofisi ya Askofu Alinikisa Cheyo,Ofisi ya Katbu Mkuu,Ofisi ya Mtunza Hazina Mkuu na lango kuu la kuingilia makao makuu ya Kanisa hilo.

Hatua hii ya kufunga ofisi za Kanisa ni la pili kwa mwaka huu awali ilikuwa mwezi Julai mwaka huu ambapo waumini hao walifunga hivyo hivyo kabla ya Serikali kuingilia kati na kufanya suluhishi kupitia Kamati ya ulinzi na Usalama ya Wilaya na kuweka makubaliano.

Hata hivyo Phili alidai maagizo yaliyotolewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama hayakutekelezwa ikiwa ni pamoja na kumrudisha kazini Mchungaji Nosigwe Buya na kuacha kumhamisha kituo cha kazi.

Aidha waumini hao walichukua hatua ya kuzuia kuhamishwa kwa Mchungaji Buya ambapo alikuwa amefunga mizigo yake huku mkewe akishindwa kupika na kuwahudumia watoto kwa siku nzima na banda la mifugo limeezuliwa na mtu aliyetumwa kutoka ofisi kuu.

Pamoja na juhudi za Kanisa kujaribu kumhamisha Mchungaji Nosigwe Buya ziligonga ukuta baada ya ya waumini hao wasiozidi ishirini kumuondoa kijana aliyekuwa akiondoa mabati na mabanzi ya banda la mifugo kuondoka mara moja na kumtaka mke wa Mchungaji Buya Edda Kabuka kuendelea na shughuli zake.

Kwa upande wake Mchungaji Buya alisema kuwa hapingi kuondoka katika nyumba hiyo na kukataa kwenda kituo kingine cha kazi lakini ameshangazwa na kwenda kinyume na makubaliano ya kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya lakini kukiukwa maazimio ya yaliyofanyika mwezi Julai mwaka huu.

Pia alidai mgogoro huu umeligawanya Kanisa na kwamba hivi sasa mahubiri yanayofanyika kanisani yamekuwa ya kutpiana maneno kwa pande mbili zinazopingana na kufanya waumini kushindwa kupata ufumbuzi wa kudumu na kudai kuwa suluhu pekee iwe ni kuitisha mkutano mkuu wa Kanisa(Sinodi).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi alisema amesikitishwa na pande hizo zinazopingana na kwamba ni kwa nini mgogoro huo haupati ufumbuzi licha ya Kamati ya ulinzi na usalama kusuluhisha na kwamba Jeshi la Polisi litamkamata yeyote atakayevunja amani kwani kazi ya Jeshi la Polisi ni kulinda usalama wa Raia na mali zake.




KWA HISANI YA MBEYA YETU

TOPE LA VOLCANO LASABABISHA MOTO MAREKANI

Moto umetokea katika jimbo la Hawaii Nchini Marekani moto huo umeunguza nyumba ya ilikuwa jirani na eneo ambalo tope hilo la moto lilikuwa likitiririka.wenyeji wa nuyumba hiyo hawakuwepo,tope hilo halikusababisha madhara zaidi.




Picha kwa Hisani ya BBC SWAHILI.

AJALI TABATA SEGEREA

Muendesha pikipiki akiwa amelala chini baada ya ajali kutokea

Thursday, November 6, 2014

WAPENZI WA FILAMU KAENI MKAO WA KULA

KIONGOZI WA DINI AUWAWA NCHINI KENYA

 Watu wasiojulikani kwenye mji wa pwani nchini Kenya ,Mombasa wamemuua kwa kumpiga risasi kiongozi mashuhuri na mwenye msimamo wa wastani wa dini ya kislamu.
Sheikh Salim Bakari Mwarangi ambaye ni mwanaharakati wa kampeni dhidi ya itikadi kali alipigwa risasi wakati alipokuwa akirudi nyumbani kutoka msikitini jumanne usiku.
Viongozi sita wa dini ya kiislamu badhi yao wenye itikadi kali na wale walio na misimamo ya wastani wameuawa mjini Mombasa tangu mwaka 2012.
Eneo la pwani ya kenya lenye waislamu wengi limekumbwa na misururu ya mashambuli ya mabomu yanoyoaminika kutekelezwa na watu walio na uhusiano na kundi la Al shabaab lenye makao yake nchini Somalia.

Wednesday, November 5, 2014

RATIBA ZA UEFA CHAMPIONS LEAGUE LEO


MKURUGENZI ATAKA ‘CHOMACHOMA’ WADHIBITIWE

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara, Beatrice Dominic, amewataka Watendaji wa Kata na Vijiji kuwakamata wafanyabiashara wanaonunua korosho kinyume na utaratibu husika wa stakabadhi ghalani kwa madai kuwa wanaikosesha Halmashauri mapato ya ndani.
Agizo hilo amelitoa kwa nyakati tofauti wakati alipokuwa kwenye ziara ya kuhamasisha kilimo wilayani hapa hivi karibuni na kuongozana na wakuu wa idara mbalimbali wa Halmashauri hiyo, lengo likiwa kuangalia namna ya kuwadhibiti walanguzi hao maarufu kama Chomachoma.
Dominic, alisema tabia ya ununuzi holela wa korosho katika Wilaya ya Masasi hasa kipindi cha msimu wa ununuzi wa zao hilo, imeshamiri katika maeneo mbalimbali na kwamba kufanya hivyo ni kinyume na taratibu za ununuzi wa zao hilo.
Alisema kwa sasa utaratibu ambao unatambulika kisheria katika ununuzi wa mazao hasa korosho ni mkulima kwenda kuuzia ghalani na si vinginevyo na kwamba, kama kunawafanyabiashara wanaofanya wanaokwenda kinyume wanapaswa kuacha mara moja.
Mkurugenzi huyo, alisema inashangaza kuona kila mwaka wafanyabiashara hao wakinunua korosho kinyume na utaratibu wa stakabadhi ghalani, huku watendaji wa Kata pamoja na Vijiji wakiwa kimya bila ya kuwakamata na kuwafikisha sehemu husika ili sheria ichukue mkondo wake.
Alionya kuwa hatosita kumwajibisha mtendaji yeyote wa Kata na Kijiji iwapo hatashiriki kikamilifu mpango huo kabambe wa kudhibiti ununuzi huo wa korosho.
chanzo:Tanzania Daima

LILE SAKATA LA MKE KUISHI NA WANAUME WAWILI ZAIDI YA MIAKA 8 LACHUKUA SURA MPYA



Mume halali Rogers Halinga wakiwa na mkewe juliana Hosea kwenye kikao cha ndugu wa mume kijijini Ishungu


Sakata la mke kuishi na wanaume wawili lachukua sura mpya baada ya kikao cha ndugu wa mume halali Rogers Halinga kuketi kikao Kijiji cha Ishungu Kata ya Ruiwa Mbarali Mkoani Mbeya na kumtaka Biton Mwashilindi kufanya mazungumzo nao kabla hawajafungua madai ya ugoni Mahakani na kudai fidia.

Kikao hicho kizito kilichofanyika nyumbani kwa Baba mzazi wa Rogers Halinga mzee Jason Halinga(95) Novemba mosi mwaka huu na kuhudhuriwa na ndugu lukuki na kumsikiza mke wa Rogers ili abaini ukweli juu ya mtoto aliyezua utata kuwa ni wa nani baina ya Rogers au Biton Mwashilindi.

Mwanamke huyo  a(22) akijikanganya mara kadhaa katika kikao hicho akidai kuwa mtoto huyo ni wa Rogers kwa kuwa aliondoka baada ya kutokea mapishano na mumewe akiwa na ujauzito wa miezi minne ndipo alipoanza mahusiano ya kimapenzi na Biton hadi siku anajifungua mwaka 2012 akiwa mikononi mwa Biton ndipo alipoamua kumwandikisha mtoto katika kadi ya kliniki na cheti cha kuzaliwa jina la Biton.

Huku ndugu wakihamaki kutokana na kauli hiyo na kwamba yeye atamke wazi mtoto ni wa nani ndipo Juliana bila aibu kwa Baba Mkwe Mzee Jason Halinga alijibu kuwa mtoto ni wa Biton Mwashilindi,ambapo alimkabidhi mtoto huyo mwishoni mwa mwezi Octoba kwa hiari na wala hakuporwa kama alivyotoa taarifa Polisi.

Kauli hiyo ya Juliana ililazimu kikao kupiga simu kwa mzazi wa Juliana anayeishi Lwanjilo wilayani Chunya kujua mustakabali wa kauli ya mtoto wao kwani ilidaiwa kuwa Biton aliwahi kwenda huko kujitambulisha kuwa yeye anaishi na mtoto wao na kwamba Biton hakujua kuwa Juliana aliwahi kuolewa kwani alidai kuwa yeye ni mwanafunzi wa VETA Mbeya na asimwambie kuwa yeye ni mwanandoa.

Baba mzazi wa Juliana Hosea Mwalukasa alidai kuwa ni kweli Biton alifika kwake lakini hakumpokea kwa kuwa alidai kuwa Juliana ni mke halali wa Rogers Halinga hivyo kama amezaa na Juliana amefanya kosa na kwamba atatozwa ugoni kwani Juliana hakuwahi kupewa talaka na Halinga.

Kikao hicho baada ya mvutano wa muda mrefu kiliamua kuwa endapo Biton anadai kuwa mtoto aliyezaliwa na Juliana aliyefahamika kwa jina la Zalida Biton(2) ni mtoto wake basi alipe fidia ya kuzaa na mke wa mtu kiasi cha shilingi milioni kumi au alipe n'gombe saba ili aweze kumkomboa mtoto wake na kwamba Juliana bado ni mke halali wa Rogers.

Kwa upande wake Biton Mwashilindi alidai kuwa hayuko tayari kulipa pesa hizo na kwamba yeye alikabidhiwa mtoto kihalali na Jeshi la Polisi Ocktoba 31 mwaka huu kituo kikuu cha kat mbele ya maafisa wa Jeshi la Polisi na kwamba hana kesi ya kujibu na kwamba anasubiri tu mtoto afikishe umri wa miaka saba ndipo amchuke.

Katika suala hili baadhi ya wadau wamelalamikia Jeshi la Polisi kwa kuamua  masuala ya kisheria katika vituo vya Polisi badala ya mamlaka za kisheria zipo kama mahakama kuliko uamuzi uliotolewa na hali hii husababisha baadhi ya wananchi kujichukulia sheria mkononi.

Wamedai kitendo cha kukabidhiwa mtoto Biton bila kuchukuliwa vipimo vya DNA bado hakujatutua mgogoro huu na kwamba bado suluhu katika ndoa hiyo hiyo itakuwa ni kitendawiri kisicho na majibu.

Kwa hisani ya Mbeya yetu

Churchill Show Season 04 Episode 34

Moment of the day: Nyeri man lifts bag of cement with his teeth

Mkasi | S10E07 With Miss Tanzania 2013/14 - Happy Watimanywa