Wednesday, December 16, 2015

WAZIRI ATOA SIKU 14 KUKAGUA MIKATABA YA AJIRA

Waziri wa nchi ,Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera,Uratibu na Bunge,Kazi,Ajira,Vijana na Watu wenye Ulemavu,Jenista Mhagama metoa siku 14 kwa maofisa kazi wote nchini,kukagua mikataba ya ajira nchini.
Waziri alitoa agizo hilo jana jijini Dar es salaam alipotembelea kiwanda cha kutengeneza nguo cha Tooku Tanzania Germent kilichopo Mabibo External,ambacho wafanyakazi wake wana mgogoro na Mwajiri wao wakiomba kuongezwa mishahara


Friday, September 11, 2015

HABARI - SEPT.11.2015| STAR TV

HABARI - SEPT.11.2015| CHANNEL TEN

KUTOKA FACEBOOK



Mvua yasimamisha mechi za US Open


Michuano ya US Open kwa upande wa kinadada imesimamishwa kwa muda baada ya mvua kali kunyesha hali iliyosababisha ugumu wa mchezo huo. Serena Williams atapaswa kusubiri mpaka ijumaa ya leo kuendelea na ratiba ya kalenda ya Grand slam ya nusu fainali kwa wanawake ambapo atacheza dhidi ya Roberta Vinci. Hali hiyo ya mvua haikuzuia mchezo wa wanaume na uliendelea kama ulivyopangwa ambapo matumaini ya bara la Afrika kuendelea kuwepo katika michuano hiyo yalifikia tamati baada ya Kevin Anderson wa Afrika Kusini kushindwa kusonga mbele katika hatua ya nusu fainali kwa kufungwa na Stan Wawrinka seti 6-4 6-4 6-0.
Nusu kwa wanaume  fainali itakuwa:
Roger Federer vs Stan Wawrinka.
Novak Djokovic vs Marin Cilic.

Kwa hisani ya BBCSWAHILI

Wednesday, July 15, 2015

MWADUI KUTIMKIA AFRIKA KUSINI KUJIFUA

Kikosi cha Mwadui FC


Kocha wa timu ya Mwadui FC ya Shinyanga Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema wanatarajia kuuomba uogozi wa matajiri hao wa kanda ya ziwa kukiwezesha kikosi hicho kwenda nchini Afrika Kusini kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao wa 2015-2016 ambapo wao watashiriki ligi hiyo.
“Tunashukuru Mungu timu yetu imeanza ‘pre-season’ vizuri tukiwa na wachezaji wetu wote wapya tuliowasajili pamoja na walioipandisha timu hii, pre-season inaendelea vizuri tena sana kama tutaendelea hivi basi naamini tutakujakuwa washindani kama ilivyokuwa Kajumulo enzi za uhai wake”, amesema Julio, kocha mkuu wa Mwadui FC.
“Sunday Kayuni yeye ni ‘consultant’ kwahiyo amekuja huku kwa kazi hiyo na yeye anatoa ushauri wa hapa na pale lakini tunafanya kazi kubwa kusema kweli tunafurahia uwepo wake kwasababu yeye anaupeo mkubwa, kwahiyo tunaamini katika huo u-consultant wake atatusaidia kwa namna moja au nyingine”, ameeleza.
“Tumeuomba uongozi ili tuone kama tunaweza kupata safari ya South Africa maana sisi (Mwadui Mining) kule ndio makao makuu yetu ili tuweze kuendelea na pre-season kidogo kuimalizia na baadae kupata mechi za kirafiki ambazo zitatuweka pazuri”, ameongeza.

 “Mbeya City walifanya vizuri kwasababu wako nje ya Dar es Salaam, Dar es Salaam kuna vishawishi vingi sana lakini unapokuwa sehemu kama Mbeya, kule unafanya mazoezi magumu ambayo yanaingia ndani ya mwili, kwahiyo sisi hapa kwetu Mwadui ni sehem nzuri tupo mgodini tuna uwanja mzuri ambao nafikiri katika Tanzania ni uwanja wa pili baada ya uwanja wa Taifa”, alimaliza Julio.

Source:http://shaffihdauda.co.tz/

BAADA YA SIKU MOJA YA SEMINA, UTAONDOKA UKIWA NA UHAKIKA WA KWENDA KUSHINDA KWENYE BIASHARA NA UWEKEZAJI NA KUINUKA KIMAISHA!


Saturday, July 11, 2015

KITUO CHA POLISI BUNJU A CHACHOMWA MOTO

Wananchi wenye hasira waishio maeneo ya Bunju A wamechukua hatua hiyo ya kukichoma kituo hicho kidogo cha Polisi baada ya Gari kumgonga mtoto wa shule ya Msingi ya Bunju A na kufa hapo hapo.

Baada ya tukio hilo la kugongwa mtoto huyo,wanafuzi walikusanyika na kufunga barabara hiyo ya bagamoyo kwa kuishinikiza Tanroad kuweka matuta katika eneo hilo.Baada ya Muda si mrefu wananchi wa eneo hilo wenye hasira kali walichukua hatua hiyo ya kukivamia kituo hicho kilicho maeneo hayo na kuanza kukichoma moto na baadae Jeshi la Polisi kufika na kuwatanyisha wananchi hao.

Baadhi ya wanachi wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo



MAKADA WA CCM WAJITENGA NA MAAMUZI YA KIKAO

Wajumbe wa kamati kuu ya CCM hajakubaliana na maamuzi yaliyotoka kwenye kikao kilichofanyika jana usiku kuwateua wagombea wa nafasi ya Urais kupitia CCM kwa kutofuata katiba ,wanasema kikao hakikupokea majina yote, kililetewa majina machache yaliyojadiliwa na kamati ya maadili,Pia anasema katiba inataka mtu anayekubalika ndiye apewe nafasi lakini kikao kiliminya wanaokubalika kwa maslahi ya wasiokubalika haya yalisemwa na Mh.Nchimbi mbele ya waandishi wa habari,kwa sababu hiyo wajumbe hao wa kamati kuu ambao ni mh.Kimbisa,mh Sofia Simba na Mh.Nchimbi,wamejitenga na maamuzi ya kikao hicho na kutoyaunga mkono


Friday, July 10, 2015

MKUTANO WA WADHAMINI WA NDONDO CUP NA VIONGOZI MBALIMBALI NA MAKABIDHIANO YA VIFAA VYA MICHEZO

Ugiriki yatoa mapendekezo mapya kwa wakopeshaji wake

 Viongozi wa Ugiriki wametuma mapendekezo ya mageuzi ili kupata makubaliano na wakopeshaji wake na kukomesha mgogoro unaoendelea.
Viongozi hao wamepania hasa kuongeza VAT na mageuzi ya pensheni. Mapendekezo ambayo, dhidi ya matatizo yote, hayaonekani kuwa tofauti sana na kile kilichokuwa kinatakiwa na wakopeshaji wa Athens, ambao wanapaswa kuyajadili leo Ijumaa asubuhi.
Ugiriki hatimaye imetuma mapendekezo yake kwa ajili ya mageuzi kabla ya kutamatika kwa muda wa mwisho uliyowekwa na viongozi wa Ulaya. Mapendekezo hayo yanapaswa kufuata mkondo wa masharti yaliyopendekezwa na wakopeshaji wa wake.
Serikali ya Ugiriki imejikubalisha kuongeza VAT kwa asilimia 23 kwa ajili ya chakula na asilimia 13 kwa ajili ya hoteli. Serikali ya Ugiriki pia imepania kufuta au kusamehe polepole VAT zinazotozwa katika visiwa vya Ugiriki.
Ugiriki pia imepania kuongeza kodi katika makampuni makubwa na mashrika mengine yasiyo ya kiserikali. Kodi kwa bidhaa za anasa na matangazo ya biashara kwenye televisheni itawekwa mara moja. Bajeti takatifu katika sekta ya ulinzi itapunguzwa Euro milioni 300 na ubinafsishaji uliosimamishwa baada ya Alexis Tsipras kuchukua hatamu ya uongozi wa nchi, utarejeshwa.
Mageuzi mapya ya pensheni pia yanatazamiwa pia kufanyika. Umri wa miaka 67 unapaswa kuwa kigezo cha kukatisha tamaa ya kustaafu mapema pamoja na kufuta au kusamehe polepole posho ya mshikamano (EKAS).
Kulingana na nakala ya mapendekezo iliyotolewa na serikali ya Ugiriki, Ugiriki inataka suluhisho " ili kurekebisha" madeni yake makubwa, kwa asilimia 180 ya Pato la Taifa, pamoja na "pakiti ya Euro bilioni 35" iliyotengwa kwa ukuaji. Serikali ya Ugiriki imesema pia iko mbioni kutafuta fedha kwa jumla ya Euro bilioni 53.5 ifikapo mwishoni mwa mwezi Juni mwaka 2018 ili kufidia majukumu yake yanayohusiana na malipo yake ya mkopo.

Alshabab lawaachilia wanajeshi 2 wa Kenya

Polisi nchini Kenya wanasema kuwa maafisa wawili wa jeshi la Kenya waliotekwa na wanamgambo ya AL Shabaab yapata miaka miwili iliyopita wameachiliwa huru.
Mkuu wa polisi Joseph Boinnet amesema kuwa wanajeshi hao walikuwa wanahamishwa hamishwa upande wa Somalia kutoka kambi moja ya Al shabaab hadi nyingine.

Hakutoa maelezo zaidi juu ya namna walivyoachiliwa lakini amesema kuwa wako katika hali nzuri ya afya.

MESSI SINGANO AMWAGA WINO AZAM FC

Mchezaji wa zamani wa Simba Messi Singano,amesajiliwa na Timu ya Azam FC kwa mkataba wa miaka 2.
Hii inaonyesha kuwa Messi alikuwa amepania kujiunga na timu hiyo ya Azam FC baada ya kumalizana na Simba iliyomkuza.
Messi akisaini mkataba huo mbele ya viongozi wa Azam FC

Uzi mpya atakaotinga Messi akiwa na Azam FC


Wednesday, July 8, 2015


MAYWEATHER UVULIWA MKANDA WA UBINGWA

Hatua za kuvuliwa mkanda huo wa ubingwa wa WBO,uzito wa Welterweight unaohusisha kilo 67 na 77 ambao alishinda mwezi mei mwaka huu dhidi ya Manny Pacquiao kutokana na kushindwa kufuata sheria na kanuni za Shirikisho holo.
Kamati ya Mashindanoya WBO imesema kwamba haina jinsi ya kufanya zaidi ya kumvua mkanda huo Mayweather ambaye ameshindwa kulipa ada kutoka kwenye pambano alilopigana na Pacquiao.
Siku ya Ijumaa iliyopita ndio ilikuwa mwisho kwa Mayweather kutimiza vigezo hivo vya ubingwa wa WBO ikiwemo kulipa ada ya dola 200,000 kutoka katika pambano lake na Pacquiao pamoja na kujivua ubingwa wa uzito wa lightmiddleweight wa WBCna WBA 

Biotech factory for ant-malaria larvae launched in Tanzania

ZOEZI LA UANDIKISHWAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA LAPIGA HODI MKOA WA PWANI

Jumla ya watu 11,248,194 wamekwishwa andikikishwa kwenye Daftari la kudumu la wapiga kura zoezi ambalo bado linaendelea kwa sasa nchini likiwa limepiga hodi mkoani Pwani.
Haya yalisemwa na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya Taifa Ndg.Damiani Lubuva kijijini Msoga kata ya Msoga wilayani Bagamoyo mbele ya Mh.Raisi Dk.Jakaya Kikwete mara baada ya kujiandikisha.
Bw.Lubuva alisema kuwa lengo la Tume ni kuandikisha Watanzania Milioni 21 hadi23 kote nchinimara zoezi hilo litakapofikia tamati kati ya mwezi Julai na Agosti mwanzoni kama hakutatokea matatizo  
Anasema changamoto zilizojitokeza ni za kawaida hasa kutokana na mfumo huo kuwa ni mpya hivyo lazima kuwe na changamoto kama ilivyo kwenye jambo lolote jipya lazima liwe na changamoto zake
Mkoa wa Pwani unajumla ya vituo 1,752 vya kujiandikisha na mashine 932 ambapo kata ya Msoga kuna jumla ya vituo 17.Zoezi hilo lilianza jana na litamalizika Julai 20.
Ni fursa kwa wakazi wa Mkoa wa Pwani kujiandikisha katika daftari lakudumu la kupiga kura na kupata nafasi ya kuchagua viongozi wanaowataka katika uchaguzi.
Raisi Akijiandikisha kwenye Mfumo Mpya wa Kielekroniki wa BVR

Raisi akichukuliwa Alama ya Vidole na Afisa Tehama wa Tume

Raisi akipokea kitambulisho chake cha kupiga Kura kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume Bw.Lubuva



Picha kwa hisani ya Michuzi Blog

Monday, July 6, 2015

BASIL MRAMBA NA DANIEL YONA WAHUKUMIWA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam  imewahukumu kwenda jela miaka mitatu aliyekuwa waziri wa fedha wa zamami Basil Mramba na aliyekuwa waziri wa Madini na Nishati wa zamani Daniel Yona baada ya kukutwa na hatia ya uhujumu uchumi na matumizi mabaya ya ofisi na kuisababishia Serikali hasara ya Sh.Bilioni 11.7


USA 5-2 JAPAN KOMBE LA DUNIA LA WANAWAKE

Friday, June 12, 2015

COPA AMERICA KUMEKUCHA

Michuano mikubwa barani Amerika imeanza hapo jana kwa wenyeji wa mashindano hayo Chile kumenyana na Ecuador na wenyeji kuibuka na ushindi mnono wa Magoli 2-0.Mpambano huo ulifanyika katika jiji la Santiago.
Ikubukwe kuwa Chile haijachukua ubingwa huo kwa takribani miaka 99 sasa.
Kwa ushindi huo unawapa Chile ari ya kufanya vizuri zaidi katika mashindano ya mwaka huu.

Arturo Vidal akifunga goli la kwanza kwa penati


Wachezaji wa Chile wakishangilia ushindi baada ya mechi kuisha


Picha kwa hisani ya bbc sport

NAFASI ZA MASOMO CHUO CHA MAENDELEO NA USIMAMIZI WA MAJI


Nigeria na mikakati dhidi ya Boko Haram

Serikali ya Nigeria na nchi nyengine nne majirani zimekubaliana kuunda vikosi vya jeshi la pamoja ili kupambana na wapiganaji wa kiislamu wa Boko Haram.
Kikosi hicho kitapiga kambi katika mji mkuu wa Chad, Ndjamena, lakini kitakuwa chini ya usimamizi wa Nigeria.Nchi ya Chad, Cameroon, Niger na Benin pia zitatoa wanajeshi wake.
Baada ya mkutano huo uliofanyika katika mji mkuu wa Nigeria Abuja, katibu mkuu wa wizara ya ulinzi ya Nigeria, Aliyu Ismail, amesema kikosi hicho kitakuwa tayari kuanza kazi ifikapo mwezi July mwaka huu:"viongozi wa nchi na serikali za nchi za ukanda wa ziwa Chad na Benin zimechukua uamuzi ufuatao.
kupitisha dhana ya ufanyaji kazi, mikakati ya ufanyaji kazi na nyaraka zinazohusiana na kuundwa kwa vikosi vya pamoja katika kupambana na kundi la kigaidi la wapiganaji wa Boko Haram, kupitisha kupelekwa kwa vikosi hivyo katika makao makuu ya Ndjamena, Chad, kwa utekelezaji wa rasilimali watu na mahitaji ya kifedha.

Kwa hisani ya http://www.bbc.com/


GAZETI LA MWANANCHI LEO 12.6.2015




DIRA YA DUNIA ALHAMISI 11.06.2015

Monday, May 18, 2015

UNAFAHAMU NINI KUHUSU MTAJI WA KAMPUNI.

Huwezi kufikiria umiliki wa kampuni kabla ya kufikiria kuhusu mtaji wa kampuni. Mtaji wa kampuni ni suala nyeti kwa wenye wazo la kumiliki kampuni au wanaomiliki kampuni tayari. Mtaji ndio kila kitu katika kampuni. Tangu unapokuwa katika harakati za kusajili kampuni utalisikia neno hili mtaji karibia katika kila hatua unayopita. Niseme mapema kuwa mtaji mdogo ndio kampuni ndogo na mtaji mkubwa ndio kampuni kubwa. Kwa hili mitaji imegawanyika mara mbili upo mtaji wa maandishi unaokuwa kwenye katiba na waraka wa kampuni( MEMAT) na upo mtaji wa mali halisi ( physical assets)
Soma zaidi.http://sheriayakub.blogspot.com/2015/05/unafahamu-nini-kuhusu-mtaji-wa-kampuni.html

RAIS MSTAAFU MWINYI ATOA PONGEZI MAALUM KWA MAGUFULI

Saturday, May 16, 2015

Raisi wa Burundi Pierre Nkurunziza aonya juu ya jaribio lingine lolote la mapinduzi


Raisi wa Burundi Pierre Nkurunzizaamewatangazia raia wake kuwa sasa amani imerejea nchini humo ikiwa ni siku tatu baada ya kushindwa kwa jaribio la mapinduzi ya kijeshi.
Akihutubia wananchi kupitia runinga Pierre Nkurunziza ametoa onyo juu ya jaribio lingine lolote la kuchukua madaraka kwa nguvu litasababisha vita umasikini na majanga yalikwisha onekana katika taifa hilo.
Hayo yanajiri wakati Marekani ikitoa onyo hapo jana kwa raisi wa Burundi Pierre Nkurunziza kuhusu kutowania muhula wa tatu wa uongozi kwa vile kutazorotesha usalama nchini humo na kutishia misaada ya kimataifa.
Msemaji wa Washington Jeff Rathke ameeleza kuwa Marekani inawasiwasi kufuatia uwezekano wa kutokea ghasia zaidi baada ya raisi Nkurunziza kurejea nchini Burundi.
Msemaji wa washington amesema kuwa marekani bado inamtambua Nkurunzinza kama raisi halali wa Burundi licha ya kusisitiza kiongozi huyo kutowania muhula wa tatu.

Baadhi ya maafisa wa kijeshi walioshiriki kuongoza mapinduzi wamekamatwa huku wengine wakitokomea na kusakwa na majeshi tiifu kwa serikali akiwemo kiongozi wa mapinduzi hayo Generali Godefroid Niyombare, ambaye awali aliiambia AFP kuwa angejisalimisha kwa serikali.

TFF waigeuka kauli yao, sasa waibebesha msalaba CECAFA kuhusu Simba, Mbeya City

SHIRIKISHO la soka Tanzania, TFF, limeshindwa kuthibitisha moja kwa moja kama ni Simba au Mbeya City fc itakayoshiriki kombe la klabu bingwa Afrika mashariki na kati, maarufu kwa jina la ‘Kagame Cup’ linalotarajia kuanza kutimua vumbi Julai 11 hadi Agosti 2 mwaka huu jijini Dar es salaam.
Katibu mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine ameuambia mtandao huu kuwa CECAFA ndio watakaosema ni timu gani ya tatu nchini Tanzania wameialika kushiriki Kagame.
Kauli hii inatofautiana na ile aliyowahi kusema kupitia mtandao huu kuwa TFF wameichagua Simba badala ya washindi wa tatu wa msimu  wa 2013/2014 wa ligi kuu soka Tanzania bara, Mbeya City fc.
“Kimsingi na kwa taratibu wawakilishi wa Tanzania ni bingwa wa msimu uliopita (2013/2014) ambao ni Azam na mshindi wa pili ambaye ni Yanga anayefaidika na uenyeji wa Tanzania”. Amesema Mwesigwa na kuongeza: “Lakini Cecafa ina nguvu ya kuingiza klabu nyingine kutoka nchi mwenyeji au kutoka ukanda mwingine wa Cecafa. Watakaocheza ni Azam na Yanga, lakini tunategemea kupokea taarifa ya Cecafa kujua ni timu gani zimetumiwa mialiko. Cecafa yenyewe itathibitisha kuwa ni nani wa ziada wamemualika, lakini wanaoingia moja kwa moja kwa Tanzania kwa vigezo ni Azam (bingwa) na Yanga wanaofaidika na uenyeji wa Tanzania”.
Kauli hii inakinzana na kauli ya Mwesigwa aliyosema na kukaririwa na mtandao huu aprili 29 mwaka huu akisema Simba wamechaguliwa kuwakilisha Tanzania.
“Mbeya City walistahili, lakini niseme ukweli, tumeamua kumchukua Simba, kwanini? kwasababu ya rekodi yake. Amekuwa bingwa mara nyingi wa mashindano haya, kwahiyo ana nafasi yake sio katika Tanzania tu bali ukanda mzima,  na huwezi kumuondoa”. Alisema Mwesigwa na kuongeza: “Mwaka jana baada ya Azam kujitoa kushiriki mashindano mapya ya kagame, tuliwapa Mbeya City nafasi”.

Hata hivyo, Mbeya City fc wanaonekana kuisubiria kwa hamu nafasi hiyo na jana kocha mkuu wa Mbeya City Juma Mwambusi alisema bado hawana uhakika wa kushiriki kutokana na kushika nafasi ya tatu 2013/2014, lakini wanatamani kuona haki inatendeka.
Wadau wa soka wanasema tayari TFF wameshatuma jina la Simba, labda kwasasa wanawatupia mzigo Cecafa ili waonekane ndio wamewachagua Simba.
Hii inatokana na ukweli kwamba wapenda soka walichukizwa na kitendo cha TFF kuwatosa Mbeya City  fc wenye sifa na kuwapa nafasi Simba wasiokuwa na vigezo na sababu kubwa ikionekana ni maslahi kuliko kuendeleza soka.


 Kwa hisani ya http://shaffihdauda.co.tz/

Mgahawa wauza nyama ya binaadamu Nigeria

Mgahawa mmoja nchini Nigeria katika jimbo la Anambra umefungwa kufuatia viongozi wenye mamlaka nchini humo kung’amua kwamba moja ya vyakula vinavyouzwa mgahawani humo ni nyama ya binaadamu.

Polisi walipoitwa mgahawani hapo waliona vichwa viwili vya binaadamu vipya vyenye kuchuruza damu wakati walipokuwa wakiwakamata watu kumi na mmoja kutoka mgahawani hapo akiwemo mmiliki wa mgahawa huo,pia walikamatwa wanawake sita na wanaume wane, baada ya wasamaria wema kutoa taarifa hizo za kustaajabisha!
Damu zilizokuwa zikivuja kwenye vichwa hivyo vya wanaadamu,vilikuwa vimefungwa kwenye mifuko ya Rambo.
Polisi pia wamekamata bunduki aina ya AK-47 na silaha nyinginezo,seti ya magurunedi na simu kadhaa za kila aina wakati walipokuwa wakiwakamata watu hao.
Kila wakati nilipokuwa nikienda sokoni,na sababu kubwa hasa hoteli hiyo iko karibu na sokoni,nimekuwa nikishuhudia harakati za ajabu za watu kuingia na kutoka hotelini humo,watu wachafu na uchafu wao mwilini ni ule usioeleweka,hivyo sikushangazwa polisi walipogundua biashara hiyo haramu mapema wiki hii, anasema mkaazi wa eneo hilo.
Mchungaji mmoja akiwa katika mshtuko mkubwa baada ya kugundua kuwa alikuwa amekula nyama ya binaadamu,aliamua kwenda polisi kupeleka malalamiko yake .
Aliwaambia kuwa alikwenda kwenye mgahawa wa hoteli hiyo asubuhi na mapema,baada ya kupata staftahi,akaambiwa kwamba pande la nyama alilokula gharama yake ni naira 700 sawa na paundi mbili unusu alistaajabu mno.sikufahamu kuwa nimeuziwa nyama ya binaadamu nikaila na kwamba ilikuwa ghali sana.
Taarifa za watu nchini Nigeria kula nyama za watu zimekuwa ni uvumi wa muda mreefu, lakini hii ni mara ya kwanza mgahawa kuamua kuuza nyama za binaadamu tu.


Kwa hisani ya BBC-Swahili



Wanajeshi washika doria Bujumbura


Jeshi nchini Burundi linapiga doria kwenye mitaa ya mji mkuu Bujumbura ambapo waandamanaji wameahidi kufanya maandamano ya kupinga uamuzi wa rais wa kuwania muhula wa tatu.
Wanajeshi wana matumaini ya kuwakamata wanajeshi waasi ambao waliongoza mapinduzi ya wiki hii katika jaribio la kumpindua rais Pierre Nkurunziza.
Nkurunziza ametaka kusitishwa kwa maandamano hayo na kuyahusisha na jaribio hilo la mapinduzi.
Lakini baadhi ya makundi ya waandamanaji yamekana madai hayo na kumtaka tena rais kuiheshimu katiba.

Marekani nayo inasema kuwa Nkurunziza hastahili kuwania muhula mwingine ikiongeza kuwa serikali yake itawajibika kwa chochote kile kitakachotokea.

Kwa hisani ya BBC-Swahili

Wednesday, May 13, 2015

Taifa Stars yaelekea Afrika ya Kusini

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kesho Jumatano inatarajiwa kusafiri kuelekea nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kushiriki michuano ya kombe la COSAFA.
 
Michuano ya COSAFA inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Mei 17 mpaka Mei 30, 2015 katika viwanja vya Olympia Park na Moruleng jimbo la North West Province nchini Afrika Kusini ikishirikisha nchi za Kusini mwa Afrika huku Tanzania na Ghana zikiwa ni nchi waalikwa.
Taifa Stars itaondoka jijini Dar es salaam kesho majira ya saa 1 jioni, kwa usafiri wa shirika la ndege la Fasjet na kufika jijini Johanesburg saa 5 usiku.
Mara baada ya kupimwa afya jana na madaktari wachezaji Aishi Manula, Isihaka Hassan, Haroun Chanongo, Kelvin Friday na nahodha Nadir Haroub wamekutwa na majeruhi ambayo yamepelekea kutokuwepo katika kikosi kitakachosafiri kesho, watabakia nchini wakiendelea kufanya mazoezi chini ya ungalizi mpaka timu itakaporejea kutoka Afrika Kusini na kuungana kwa ajili ya maandalizi ya AFCON, huku Amri kiemba akipewa ruhusa kutokana na kuwa na matatizo ya kifamilia.
Msafara wa Taifa Stars utaongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa TFF, Ephaphra Swai ukijumuisha wachezaji 20 na benchi la ufundi, timu inatarajiwa kufikia katika hoteli ya Sun City iliyopo pembeni kidogo ya jiji la Rusterburg.

Barcelona yatinga fainali

Barcelona imetinga fainali ya michuno ya ligi ya Mabingwa, baada ya kumenyana Jumanne usiku wiki hii na Bayern Munich. Bayern Munich imeaga michuano hiyo, baada ya kuifunga Barcelona mabao 3-2 katika mchezo wa marudiano wa michuano ya nusu fainali ya Kombe la Mabingwa barani Ulaya.

Katika mchezo wa awali uliyochezwa wiki moja iliyopita, Barcelona iliifunga Bayern Munich mabao 3-0.
Barcelona inasubiri kucheza fainali Juni 6 mwaka 2015 na moja ya klabu itakayoshinda leo Jumatano usiku kati ya Real Madrid na Juventus.
Bayern Munich ndio iliyoanza kuona lango la Barcelona katika mchezo wa marudiano wa michuano ya fainali ya Kombe la Mabingwa barani Ulaya. Bao la kwanza la Bayern limefungwa na mchezaji kutoka Morocco Mehdi Benatia katika dakika ya 7 ya mchezo.

Katika dakiaka ya 15 Barcelona kupitia mchezaji wake Neymar ikasawazisha baada ya pasi aliyopewa na Luis Suarez kutoka kwa Muargentina Lionel Messi.
Barcelona iliendelea kushambulia lango la Bayern Munich na kufaulu katika dakika ya 29 kufunga bao la pili kupitia mchezaji wake Neymar, na kuongoza mabao 2-1 dhidi ya Bayern Munich.
Hadi wakati huo, Bayern Munich ilikua inataraji ifunge mabao 6-2 ili iweze kutinga fainali ya michuano ya ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Lakini hali hiyo haikutokea.
Hata hivyo Bayern ilikuja juu na kufaulu kusawazishabao la pili kupitia Robert Lewandowski katika dakiaka ya 40. .
Katika dakika ya 74, Bayern Munich kupitia mchezaji wake Thomas Müller ilifunga bao la tatu. Hadi kipenga cha mwisho Bayern Munich iliongoza kwa mabao 3-2 dhidi ya Barcelona. Licha ya Bayern kuibuka mshidi katika mchuano huo, ililazimika kuaga michuano hiyo, baada ya kupoteza katika mechi ya awali ya nusu fainali wiki moja iliyopita, ambapo ilifungwa mabao 3-0.
Barcelona, wamefanikiwa kutinga fainali baada ya kuibwaga Bayern Munich kwa jumla ya mabao 5-3 yaliyopatikana katika mikondo yote miwili waliyokutana kwenye hatua ya nusu fainali.
Jumatatu usiku wiki hii kutakuwa na mchuano kati ya Real Madrid dhidi ya Juventus kwenye uwanja wa Benabeu.

Shughuli za uokozi zakwama upya Nepal


Wafanyikazi wa mashirika ya kutoa misaada wamesema kuwa tetemeko la hapo jana nchini Nepal limeathiri kwa kiasi kikubwa.juhudi za kutoa misaada kwa waathiriwa wa tetemeko la awali lililosababisha vifo vya zaidi ya watu 8000 takriban majuma mawili yaliyopita.
 
Mashirika ya misaada yanasema kuwa maporomoko mapya ya ardhi sasa yemekatiza usafiri baada ya kuziba mabarabara yaliyokuwa yamesazwa na tetemeko la awali.
Hadi kufikia sasa inakisiwa kuwa takriban watu 65 wamepoteza maisha yao nchini Nepal huko maafa zaidi yakitarajiwa nchini India na Tibet ,China.
Shughuli za uokozi zimerejelewa Nepal, ambayo kwa mara ya pili ndani ya wiki tatu imekumbwa na tetemeko kubwa la ardhi.
Lakini bado kuna watu waliozikwa kwenye vifusi.
Maafisa wa huko wanasema kuwa wanatarajia idadi hiyo kuongezeka.
Kufikia sasa takriban watu 1,000 wamejeruhiwa na tetemeko hilo lipya.

Waathiriwa wengi wameripotiwa kufunikwa na vifusi karibu na kitovu cha tetemeko hilo katika mji wa Chautara
Watu wengi wamelala nje wakihofia kuwa wanaweza kuathirika zaidi wakiwa ndani ya nyumba zao.
Wakati huo huo helikopta ya kikosi cha majini cha Marekani,ambayo ilikuwa ikifanya kazi ya kusaidia kusambaza huduma za kibinaadamu nchini Nepal, haijulikani iliko.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa, ndani ya helikopta hiyo kulikuwa na watu wanane,miongoni mwao, sita ni askari wa kikosi cha majini cha Marekani na askari wawili wa jeshi la Nepal.
Maofisa wa serikali wa Marekani wamesema kwamba helikopta hiyo ilikuwa maeneo ya jirani na kijiji cha Charikot, ambacho kiliharibiwa vibaya na tetemeko la ardhi.

 
Kwa hisani ya bbcswahili.com

 

Tuesday, May 12, 2015

BAADHI YA MADHARA YA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA JIJINI DAR

Hii ni barabara ya mbozi Chang'ombe 


Eneo la Sokota barabara ya Mandela

Kero hii ya mvua na miundombinu mibovu ni hata kwa waenda kwa Miguu

Picha zote kwa hisani ya Mdau wetu Roman Mallya

Thursday, May 7, 2015

ATHARI ZA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA JIJINI DAR

Hapa ni maeneo ya Mchicha kutokea Vingunguti njia imejaa maji na haipitiki
Vingunguti

Maeneo ya Chang'ombe Mbozi Road

Picha zote kwa hisani ya Mdau wetu Maonyesho Ndege