Saturday, May 16, 2015

Raisi wa Burundi Pierre Nkurunziza aonya juu ya jaribio lingine lolote la mapinduzi


Raisi wa Burundi Pierre Nkurunzizaamewatangazia raia wake kuwa sasa amani imerejea nchini humo ikiwa ni siku tatu baada ya kushindwa kwa jaribio la mapinduzi ya kijeshi.
Akihutubia wananchi kupitia runinga Pierre Nkurunziza ametoa onyo juu ya jaribio lingine lolote la kuchukua madaraka kwa nguvu litasababisha vita umasikini na majanga yalikwisha onekana katika taifa hilo.
Hayo yanajiri wakati Marekani ikitoa onyo hapo jana kwa raisi wa Burundi Pierre Nkurunziza kuhusu kutowania muhula wa tatu wa uongozi kwa vile kutazorotesha usalama nchini humo na kutishia misaada ya kimataifa.
Msemaji wa Washington Jeff Rathke ameeleza kuwa Marekani inawasiwasi kufuatia uwezekano wa kutokea ghasia zaidi baada ya raisi Nkurunziza kurejea nchini Burundi.
Msemaji wa washington amesema kuwa marekani bado inamtambua Nkurunzinza kama raisi halali wa Burundi licha ya kusisitiza kiongozi huyo kutowania muhula wa tatu.

Baadhi ya maafisa wa kijeshi walioshiriki kuongoza mapinduzi wamekamatwa huku wengine wakitokomea na kusakwa na majeshi tiifu kwa serikali akiwemo kiongozi wa mapinduzi hayo Generali Godefroid Niyombare, ambaye awali aliiambia AFP kuwa angejisalimisha kwa serikali.

No comments:

Post a Comment