Saturday, July 11, 2015

KITUO CHA POLISI BUNJU A CHACHOMWA MOTO

Wananchi wenye hasira waishio maeneo ya Bunju A wamechukua hatua hiyo ya kukichoma kituo hicho kidogo cha Polisi baada ya Gari kumgonga mtoto wa shule ya Msingi ya Bunju A na kufa hapo hapo.

Baada ya tukio hilo la kugongwa mtoto huyo,wanafuzi walikusanyika na kufunga barabara hiyo ya bagamoyo kwa kuishinikiza Tanroad kuweka matuta katika eneo hilo.Baada ya Muda si mrefu wananchi wa eneo hilo wenye hasira kali walichukua hatua hiyo ya kukivamia kituo hicho kilicho maeneo hayo na kuanza kukichoma moto na baadae Jeshi la Polisi kufika na kuwatanyisha wananchi hao.

Baadhi ya wanachi wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo



No comments:

Post a Comment