Saturday, July 11, 2015

MAKADA WA CCM WAJITENGA NA MAAMUZI YA KIKAO

Wajumbe wa kamati kuu ya CCM hajakubaliana na maamuzi yaliyotoka kwenye kikao kilichofanyika jana usiku kuwateua wagombea wa nafasi ya Urais kupitia CCM kwa kutofuata katiba ,wanasema kikao hakikupokea majina yote, kililetewa majina machache yaliyojadiliwa na kamati ya maadili,Pia anasema katiba inataka mtu anayekubalika ndiye apewe nafasi lakini kikao kiliminya wanaokubalika kwa maslahi ya wasiokubalika haya yalisemwa na Mh.Nchimbi mbele ya waandishi wa habari,kwa sababu hiyo wajumbe hao wa kamati kuu ambao ni mh.Kimbisa,mh Sofia Simba na Mh.Nchimbi,wamejitenga na maamuzi ya kikao hicho na kutoyaunga mkono


No comments:

Post a Comment