Wednesday, July 8, 2015

MAYWEATHER UVULIWA MKANDA WA UBINGWA

Hatua za kuvuliwa mkanda huo wa ubingwa wa WBO,uzito wa Welterweight unaohusisha kilo 67 na 77 ambao alishinda mwezi mei mwaka huu dhidi ya Manny Pacquiao kutokana na kushindwa kufuata sheria na kanuni za Shirikisho holo.
Kamati ya Mashindanoya WBO imesema kwamba haina jinsi ya kufanya zaidi ya kumvua mkanda huo Mayweather ambaye ameshindwa kulipa ada kutoka kwenye pambano alilopigana na Pacquiao.
Siku ya Ijumaa iliyopita ndio ilikuwa mwisho kwa Mayweather kutimiza vigezo hivo vya ubingwa wa WBO ikiwemo kulipa ada ya dola 200,000 kutoka katika pambano lake na Pacquiao pamoja na kujivua ubingwa wa uzito wa lightmiddleweight wa WBCna WBA 

No comments:

Post a Comment