Tuesday, July 12, 2016

Mkapa aunguruma UDSM, akiri kukosea sera ya ubinafsishaji, agusia katiba mpya

Mtoto apandikizwa pua mpya India



Madaktari nchini India wamepandikiza pua mpya katika uso wa mvulana wa miaka 12 iliokuwa imemea katika paa lake la uso.
Pua ya Arun Patel iliharibika alipougua ugonjwa wa homa ya kichomi
Maambukizi hayo yaliharibu pua yake akiwa mtoto mdogo.
Upandikizaji kama huo ulifanywa nchini China mwaka 2013 ambapo mtu mmoja ambaye aliharibu pua yake katika ajali alipewa pua mpya.
Wazazi wa Arun walimchukua na kumpeleka katika daktari mwengine katika kijiji cha jimbo la kati la Madhya Pradesh ambapo aliugua kichomi mda mfupi baada ya kuzaliwa.

Lakini matibabu aliyopewa yaliongeza hali yake na hivyobasi kupoteza pua yake.

Miaka kadhaa baadaye,kundi moja la madaktari katika mji wa Indore liliamua kufanya upasuaji usiokuwa wa kawaida ambapo Arun alipata pua mpya.

 kwa hisani ya BBCSwahili

Mabaki ya Wafilisti yapatikana Israel

Watafiti wa mambo ya kale nchini Israel wamegundua makaburi ya kwanza ya Wafilisti.
Makaburi hayo, yaliyopatikana eneo la Ashkelon, yaligunduliwa mwaka 2013, lakini habari hizo zilifichuliwa Jumapili.
Habari hizi ziliwekwa siri muda huo wote kuzuia kushambuliwa na waandamanaji wa makundi ya Wayahudi wahafidhina ambao hawakutaka makaburi hayo yafukuliwe.

 Taarifa zinasema ugunduzi huo huenda ukafichua mengi kuhusu asili ya Wafilisti ambao wamezungumziwa sana katika vitabu vya kidini.


Mafanikio hayo yalitokea mwisho wa mwaka wa 30 wa uchimbaji ulioongozwa na kundi la Leon Levy Expedition.
Viongozi wa uchimbaji huo wanasema walipata makaburi yaliyozingirwa na manukato, vyakula, mapambo, vito na silaha.
Yanadaiwa kujengwa na kutumiwa kati ya karne ya 11 na karne ya 8 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu.


"Baada ya kutafiti kuhusu Wafilisti kwa miongo mingi, hatimaye tunaweza kuwatazama,” anasema mmoja wa wanaakioloiia hao Daniel M Master.
“Kwa ugunduzi huu, tunakaribia kubaini siri za asili yao.”
Profesa Lawrence E. Stager ni mmoja wa wanaoongoza utafiti huo

Wanaakiolojia hao sasa wanafanya uchunguzi wa DNA pamoja na uchunguzi wa miale ya ukaa kubaini watu hao waliishi wakati gani.
Watafiti hutofautiana kuhusu asili ya Wafilisti, baadhi wakiamini walitoka Ugiriki, wengine visiwa vya Crete au Cyprus na wengine eneo la Anatolia nchini Uturuki.


Wafilisti huoneshwa katika Biblia kama maadui wakuu wa Waisraeli, na inadhaniwa walihamia Israel kutoka maeneo ya Magharibi karne ya 12 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu.
Anayefahamika zaidi ni Goliath, mpiganaji ‘jitu’ ambaye kwa mujibu wa Biblia, aliuawa na Daudi kabla yake kuwa Mfalme wa Waisraeli.
Katika Biblia, wanaoneshwa kama watu wakatili lakini mabaki yaliyopatikana yanaonekana kuashiria kwamba walikuwa na ustaarabu fulani.


Habari kwa hisani ya BBCSwahili

Saturday, July 2, 2016

KUTOKA TRA


AZAM MARINE WAJA NA SEA TAX

Kampuni ya usafirishaji majini ya Azaam Marine imekuja na huduma mpya ya usafirishaji wa majini jijini Dar es salaam.




UJENZI WA DARAJA LA KONGOWE - KIGAMBONI WAENDELEA

Daraja linalounganisha maeneo ya Mbagala Kongowe na Kigamboni lililopo eneo la Mbagala Kongowe ambalo lilikuwa shida kupitika wakati wa mvua kubwa sasa linajeungwa upya.Daraja hili ni kiungo kikukwa sana kwa wakazi waishio maeno ya Toangoma,Kibada na Kigamboni Kutokea Mbagala Kongowe.








Friday, July 1, 2016

KUTOKA BUNGENI



Kutoka Bungeni jijini Dodoma ,Wabunge wa kambi rasmi ya Upinzani jana asubuhi waliingia Bungeni wakiwa wote wamevalia nguo nyeusi walipohudhuria kikao cha Bunge la Bajeti.Baada ya Naibu Spika Dk Tulia Ackson kuingia Bungeni na kuongoza dua ya kuliombea Bunge walianza kunyanyua mabango mbalimbali na kutoka nje

TAARIFA KWA WATUMIAJI WA HUDUMA ZA KIBENKI



RATIBA YA LADY JAYDEE IDD PILI