Wednesday, December 18, 2013
12 MAHAKAMANI KWA UKEKETAJI SAME
Wanawake 12 ambao ni
wazazi wa wasichana 21 waliofanyiwa ukeketaji wilayani Same, mkoa wa
Kilimanjaro, kaskazini mwa Tanzania, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu
Mkazi, Same, wakati waliposomewa mashitaka yao kwa mara ya kwanza tangu
wakamatwe mwishoni mwa wiki iliyopita.
Watuhumiwa wote wanashitakiwa kwa kosa la
Ukatili dhidi ya watoto na kuwasababisha maumivu makali, shitaka ambalo wote
wamekana.
Tisa kati ya watuhumiwa hao 12 wameachiliwa
kwa dhamana, huku watatu wakibaki mahabusu kwa kushindwa kutimiza masharti ya
dhamana ambayo ni shilingi milioni mbili za Tanzania, sawa na dola 1250 za
Kimarekani.
Miongoni mwa washitakiwa, mmoja alikabiliwa na
mashitaka mawili, moja akiwa mzazi wa mmoja wa wasichana waliokeketwa na pia
akiwa ngariba.
Kutokana na mila na desturi ya baadhi ya
makabila nchini Tanzania, ukeketaji unafanyika japo ni kinyume cha sheria, huku
watu wanaokamatwa kuhusika na ukeketaji wakichukuliwa hatua za kisheria.
Kama watapatikana na hatia, wanawake hao
wanakabiliwa na kifungo kisichopungua miaka mitano jela au kutozwa faini kubwa.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 30 Desemba
2013, wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.
Habari kwa hisani ya BBC Swahili
Waliokufa Sudan Kusini ni '400 - 500'
Mamia ya watu
wanaaminika kufa wakati wa mapigano baina ya majeshi ya yanayomuunga mkono rais
wa Sudan Kusini na yale yanayomuunga mkono makamu wa rais, maafisa wa Umoja wa
Mataifa waliopo Sudan Kusini wamesema baada ya kunukuu ripoti ambayo bado
haijathibitishwa..
Wanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa wamesema
wameambiwa na vyanzo vya habari katika mji wa Juba kwamba idadi ya watu
waliokufa wanaweza kufikia 400 hadi 500.
Sudan Kusini imekuwa na mapigano ya siku mbili
kufuatia taarifa kwamba kulikuwa na jaribio la kumpindua rais Salva Kiir.
Mwanasiasa wa upinzani aliyeko uhamishoni Riek
Machar amekana madai ya serikali kuwa alijaribu kufanya jaribio hilo.
"Kilichotokea Juba ni kutokuelewana na
mgawanyiko baina ya vikosi vya ulinzi vya rais, sio jaribio la mapinduzi,"
aliiambia Sudan Tribuni, tovuti yenye makao yake Paris katika mahojiano
yaliyochapishwa siku ya jumatano.
Bwana Machar Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan
Kusini ambaye aliondolewa na rais Kiir mwezi Julai, amesema hana taarifa wala
hausiki kwa namna yoyote na jaribio hilo la mapinduzi.
Rais wa Sudan Kusin Salva Kiir amesema kundi
la wanajeshi wanaomuunga mkono makamu wa rais Machar walikuwa wakijaribu
kujitwalia madaraka kwa kwa nguvu siku ya Jumapilil usiku, lakini walishindwa.
Wakati mapigano yanaendelea siku ya jumatatu
na jumanne, serikali imesema wanasiasa kumi maarufu akiwemo waziri wa zamani wa
fedha, wametiwa mbaroni.
Taarifa za mapigano hayo zimefika kwenye
baraza la kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York siku ya jumanne, ambapo limesema
mapigano hayo yanaweza kuwa mapingano ya kikabila.
Tuesday, December 17, 2013
Monday, October 28, 2013
Mourinho amsifia Torres kwa kuipa Cheslea bao la ushindi
Kocha wa klabu ya soka ya Chelsea nchini Uingereza Jose Mourinho amemsifu mshambulizi Fernando Torres baada ya kuisaidia timu yake kupata ushindi wa mabao 2 kwa 1 dhidi ya Manchester City katika mchuano wa ligi kuu ya soka nchini humo mwishoni mwa juma lililopita
Thursday, October 10, 2013
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MBEYA KWA UMMA-AJALI YA GARI KUACHA NJIA, KUPINDUKA NA KUSABABISHA KIFO NA MAJERUHIKwa
MNAMO TAREHE 08.10.2013 MAJIRA YA SAA 16:00HRS HUKO
KATIKA ENEO LA RELINI – MLOWO BARABARA YA MLOWO/KAMSAMBA
WILAYA YA MBOZIMKOA WA MBEYA. GARI T.353 APR AINA YA TOYOTA HILUX
P/UP LIKIENDESHWA NA DEREVA ASIYEFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE,
LILIACHA NJIA NA KUPINDUKA KISHA KUSABABISHA KIFO CHA MTOTO PETRO S/O
KAUNDA, MIAKA 3, KYUSA, PIA MAJERUHI KWA MAMA MZAZI WA MTOTO HUYO AITWAE
FAUSTA D/O MBUBA, MIAKA 35, MNYIHA, MKULIMA, MKAZI WA KIJIJI CHA ITEMPULA
AMBAYE AMELAZWA ZAHANATI YA NAZARETH – MLOWO. CHANZO KINACHUNGUZWA.
DEREVA ALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO. MWILI WA MAREHEMU
UMEHIFADHIWA KATIKA ZAHANATI HIYO. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA
KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANAENDELEA KUTOA
WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO KWA KUZINGATIA
SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA
KUEPUKIKA. AIDHA ANATOA RAI KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA JUU YA MAHALI
ALIPO MTUHUMIWA AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI AKAMATWE NA SHERIA
ICHUKUE MKONDO WAKE, VINGINEVYO AJISALIMISHE MWENYEWE.
WILAYA YA KYELA – KUPATIKANA NA
BHANGI. MNAMO TAREHE 08.10.2013 MAJIRA YA SAA 16:00HRS HUKO ENEO LA
MBUGANI WILAYA YA KYELA MKOA WA MBEYA. ASKARI POLISI WAKIWA DORIA
WALIMKAMATA FRANK S/O ARON, MIAKA 27, KYUSA, MKULIMA, MKAZI WA MBUGANI
AKIWA NA BHANGI MISOKOTO 20 SAWA NA UZITO WA GRAM 120. MTUHUMIWA NI
MUUZAJI NA MVUTAJI WA BHANGI. TARATIBU ZINAFANYWA ILI AFIKISHWE
MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA
POLISI DIWANI ATHUMANI ANAENDELEA KUTOA WITO KWA JAMII KUACHA
KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA
YA MTUMIAJI.
[DIWANI ATHUMANI - ACP]KANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
KWA HISANI YA:mbeyayetu.blogspot.com
Wednesday, September 25, 2013
KENYA YATANGAZA SIKI 3 ZAMAOMBOLEZO
Kenya inaanza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kwa waathiriwa wa mashambulizi ya kigaidi yaliyofanyika katika jengo la kibiashara la Westgate mjini Nairobi.
Rais Uhuru Kenyatta pia ameseama kuwa bendera zitapeperushwa nusu mlingoti kwa heshima ya waliopoteza maisha yao katika mashambulizi hayo.Watu 67 wameuawa ikiwemo wanajeshi kadhaa wa usalama, ingawa kuna hofu kuwa idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka.
Maafisa wa uchunguzi wa kimataifa wanaungana na wale wa Kenya kujaribu kuondoa mili ambayo imenaswa kwenye vifusi vya jengo hilo ambalo sehemu yake iliporomoka jana. Nia ni kujaribu pia kutambua uraia wa washambulizi hao.
Baraza la usalama wa kitaifa linatarajiwa kukutana leo kudadisi yaliyotokea na kujiandaa kwa mkakati mpya wa kigaidi.
Magaidi watato wa kundi la Al Shabaa lililokiri kutekeleza mashambulizi hayo,waliuawa katika shambulizi hilo lililodumu siku nne na kuwa washukiwa wengine 11 walikamatwa wakijaribu kuondoka nchini.
Katika hotuba yake kwa taifa siku ya Jumatano , Rais Uhuru Kenyatta alisema kuwa alihisi uchungu mkubwa na kuwa Kenya imejeruhiwa vibaya,lakini alielezea matumaini kwa kuwa shambulizi limeisha na kusema kwamba waliohusika watakiona cha mtemakuni.
Wakati huohuo, afisaa mmoja mkuu wa serikali ya Somalia, amesema kuwa hakuna suluhu la kijeshi kwa kundi la wanamgambo wa Al Shabaab nchini humo. Wanamgambo hao wameitikia kuhusika na mashambulizi ya kigaidi nchini Kenya ambao watu zaidi ya sitini wameuawa.
Akizungumza na mjumbe wa nchi hiyo katika Umoja wa Mataifa, Yusuf Mohamed Ismail Bari Bari, alisema kuwa serikali yake na jamii ya kimataifa inapaswa, kungazia zaidi mizizi ya tatizo la magaidi hao, upatikanaji wa rasilimali pamoja na uwakilishi wa kisiasa.
SKorea rejects Boeing, says F-15 not good enough
South Korea rejects Boeing, the sole remaining bidder, in $7.7B project for 60 fighter jets
SEOUL, South Korea (AP) -- South Korea on Tuesday rejected Boeing Co.'s bid to supply 60 fighter jets in the country's largest-ever weapons purchase even though it was the sole remaining bidder, and said it would reopen the tender.
Boeing had offered its F-15 Silent Eagle, but South Korean critics have said the warplane lacks state-of-the-art stealth capabilities and cannot effectively cope with North Korea's increasing nuclear threats.
Defense Ministry spokesman Kim Min-seok said officials decided at a meeting Tuesday to delay naming a winning bidder for the 8.3 trillion won ($7.7 billion) purchase, and would restart the bidding process at an early date.
He said South Korea must have better air power in line with an international trend to develop "fifth generation" fighters, and said the rejection of Boeing's bid was made in consideration of North Korea's nuclear weapons program and other factors. Ministry officials said he was referring to a warplane with cutting-edge radar-evading stealth functions which Boeing's plane does not have.
Boeing said in a statement that it was "deeply disappointed" by Tuesday's decision, adding it "rigorously" followed the South Korean arms procurement agency's instructions throughout the entire process.
Lockheed Martin's F-35 Joint Strike Fighter and EADS' Eurofighter Typhoon earlier competed in the bidding process but were eliminated for exceeding Seoul's budget cap.
The F-35 jet, which has been plagued by schedule delays and cost overruns, is widely regarded as a much more advanced and capable aircraft than its predecessors.
Japan announced in 2011 that it would buy 42 F-35 jets in a deal expected to cost more than $5 billion. Japan hopes to receive its first F-35s in 2016, at a cost of about $120 million per plane. But last year it threatened to cancel the multibillion-dollar deal if prices continue to rise or delays threaten the delivery date.
South Korea has traditionally favored importing fighter jets and other weapons from the U.S., which stations 28,500 troops in the country as deterrence against potential aggression from North Korea.
This spring, tensions on the Korean peninsula rose sharply, with Pyongyang threatening nuclear wars to protest toughened U.N. sanctions after its third nuclear test in February. The U.S. took the unusual step of sending its most powerful warplanes — B-2 stealth bombers, F-22 stealth fighters and B-52 bombers — to drills with South Korea in a show of force. B-2 and B-52 bombers are capable of delivering nuclear weapons.
In recent days, South Korean media, retired generals and weapons experts had pressed the government not to pick the F-15 Silent Eagle, arguing better stealth capabilities were needed.
"Only with stealth capabilities can (warplanes) covertly infiltrate North Korea and get rid of its nuclear threats," a group of 15 former air force chiefs of staff said in a recent letter addressed to President Park Geun-hye.
The
rivals Koreas have hundreds of thousands of combat-ready troops along a heavily
armed border as the 1950-53 Korean War ended in a truce, not a peace treaty.
North Korea's air force is relatively old and ill-prepared, but has a large
number of aircraft that could be a factor if a conflict were to break out
Monday, September 23, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)