Angalia picha ya waokoaji
Tuesday, March 11, 2014
Friday, March 7, 2014
MTOTO WA GADDAFI,SAADI ASHIKILIWA LIBYA
Serikali ya Libya imesema kuwa mtoto wa Kiongozi wa
zamani wa nchi hiyo, Saadi Gaddafi, ameondoshwa nchini Niger hivi sasa
anashikiliwa mjini Tripoli.
Saadi alitoroka baada ya baba yake, Kanali Muammar
Gaddafi kuuawa wakati wa mapinduzi yaliyofanyika mwaka 2011 nchini Libya.
Anashutumiwa kuwafyatulia risasi waandamanaji na anadaiwa
kutekeleza uhalifu mwingine wakati wa utawala wa baba yake, yeye alipokuwa
Kiongozi wa vikosi maalum vya kijeshi.
Serikali ya Libya imetoa taarifa hiyo mapema siku ya
alhamisi kuwa wamempokea akitokea Niger.
awali , Niger ilikataa ombi la Libya ilipotaka
imsafirishe Saadi, huku waziri wa sheria wa Niger akihofu kuwa Saadi
atahukumiwa adhabu ya kifo.
MALARIA YAWA UGONJWA HATARI ZAIDI
Watafiti kutoka Uingereza na
Marekani wanasema kuwa mabadiliko ya hali ya hewa huenda yakazua ongezeko kubwa
la maambukizi ya ugonjwa wa Malaria kote duniani huku ugonjwa huo ukienea
katika maeneo ya milimani barani Afrika na Amerika ya Kusini.
Katika matokeo ya utafiti yaliyochapishwa
kwenye jarida la Science, wanasayansi hao wanasema hata ongezeko dogo katika
viwango vya joto siku za usoni huenda likaongeza kwa mamilioni maambukizi ya
malaria.
Mbu anayesababisha malaria.
Watafiti wamepata ushahidi kwamba mbu
anayebeba kimelea kinachosababisha malaria wanaelekea katika nyanda za juu
wakati viwango vya joto vikipanda.
Watu wanaoishi katika maeneo ya nyanda za juu
wanakosa kinga na hivyo kurahisisha maradhi ya malaria kuenea.
Takriban watu milioni mia mbili ishirini kote
duniani huambukizwa ukonjwa wa malaria.
Mbu aneyesababisha malaria
Thursday, March 6, 2014
FOLENI KUBWA MBAGALA MZINGA DARAJANI JANA
Jana Jioni majira ya saa kumi na mbili jioni nilikuwa naelekea maeneo ya Mbagala Kongowe nikakutana na foleni kubwa sana ambayo ilisababishwa na ubovu wa barabara pamoja na magari kutofuata taratibu na sheria barabarani.nilikuwa kwenye bodaboda lakini ilinichuku kama dk 15 hivi kupita kwenye daraja hili kwa jinsi magari yalivyokaa vibaya na kusababisha kufunga njia.
Angalia baadhi ya picha nilizochukua nikiwa kwenye eneo hilo.
hakuna pa kutokea |
Hizi ni baadhi ya bodaboda zikiwa kwenye foleni |
Wednesday, March 5, 2014
Subscribe to:
Posts (Atom)