Wednesday, December 6, 2017

Azam TV - CECAFA: ZANZIBAR VS RWANDA (3-1) FULL HIGHLIGHTS (5/12/2017)

MWANAFUNZI AJIFANYA ASKARI WA JWTZ

Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam, inamshikilia mwanafunzi wa Sekondari ya Fahari iliyopo Goba, mwenye miaka 17 kwa kosa la kukutwa amevaa sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Kamanda Mambosasa amesema katika mahojiano ya awali, kijana huyo alijitambulisha kuwa ni askari kutoka 501 KJ Lugalo jijini Dar es Salaam.

Amesema baada ya kubanwa alikiri kupata sare hizo kwa rafiki zake na upekuzi ulipofanywa ndani ya begi alilokuwa nalo alikutwa na kofia nyingine moja ya jeshi hilo.


Pia, alikutwa na kitambulisho cha mtoto wa askari wa JWTZ Private Gabriel Kiwila wa 501 KJ. (Picha kwa hisani ya Mwananchi).

Thursday, November 30, 2017

Raisi wa Nigeria apinga raia wake kuuzwa kama mbuzi Libya

Raisi wa Nigeria Muhammadu Buhar amesemaraia wote wa Nigeria ambao wamekwama Libya watarejeshwa nyumbani.
Amesema hayo baada ya video za hivi karibuni mitandaoni zikionyesha waafrika wakiuzwa kwenya soko la mnada wa watumwa huko nchini Libya
Buhari amesema”baadhi ya raia wa Nigeria wanauzwa kama mbuzi dola kadhaa Libya”
Kwenye video iliyotolewa na shirika la habari la CNN mapema mwezi huu ,vijana kutoka mataifa ya Afrika kusini mwa jangwa la Salahara walionekana wakiuzwa kama wafanyakazi wa mashambani .
Walikuwa wakiuzwa $400 katika eneo ambalo halikuwekwa wazi huko Libya                                                     


 Picha kwa hisani ya cnn.com



MAJALIWA NAYE AWASHA MOTO BANDARINI DAR

Wednesday, November 29, 2017

Raila atishia kujiapisha kama rais siku kuu ya Jamhuri Dei

SIMBA YALETA BEKI WA GHANA KUCHUKUA NAFASI YA MAVUGO

Klabu ya Simba ipo kwenye hatua za mwisho kumalizana na beki kisiki raia wa Ghana, Malik Ismaila wa Tema Youth, kwa mujibu wa Mwanaspoti umeripoti kuwa nyota huyo tayari yupo Dar es salaam na dili lake likifanikiwa anatarajiwa kuchukua nafasi ya Laudit Mavugo ambaye anatarajiwa kutolewa kwa mkopo katika klabu ya Gor Mahia


kwa hisani ya:http://www.goal.com/sw

Makamu wa rais wa Tanzania amtembelea Tundu Lissu Hospitalini Nairobi

Makamu wa Raisi wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan amemtembelea Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu ambaye amelazwa katika hospitali ya Nairobi ambapo anaendelea na Matibabu.Makamu wa Raisi alimtembelea Mbunge huyo wa Singida Mashariki  muda mfupi baada ya kuhudhuria kuapishwa kwa Raisi wa Taifa la Kenya Uhuru Kenyatta tarehe 28November 2017.

Mheshimiwa Lissu amekuwa akipata matibabu katika hospitali hiyo tangu Septemba 7 baada ya shambulio la kupigwa risasi na watu wasiojulikana katika jaribio la mauaji huko nyumbani kwake mjini Dodoma