Monday, April 15, 2013

MRITHI WA HUGO CHAVES APATIKANA

Rais Mpya wa Venezuela Nicolas Maduro
Tume ya uchaguzi nchini venezuela imetangaza kiongozi wa kisoshalisti Nicolas Maduro kama mshindi wa uchaguzi wa urais kwa asilimia 51 tu ya kura.
Hata hivyo ushindi huo dhidi ya mpinzani wake mkuu Henrique Capriles ulikuwa ni wa chini ya asilimia mbili, ikiwa ni chini ya robo ya kura zipatazo milioni 15 ya zile zilizopigwa .
Ni ushindi mdogo zaidi ikilinganishwa na ule alioupata kiongozi wa chama chake hayati rais Hugo Chavez,mwaka jana, muda mfupi kabla ya kifo chake.
Kufuatia tangazo la ushindi huo Bwana Maduro alivaa mavazi yenye rangi za bendera ya Venezuela akidai uchaguzi wake ni wa haki na wa kisheria na akawataka raia wawe watulivu. Aliahidi kuendeleza sera za Bwana Chavez.
Pindi habari zilizpojitokeza kuwa Maduiro alikuwa mshindi, wafuasi wake walianza kusherehekea mjini Caracas, huku wafuasi wa upinzani nao wakianza kupiga sufuria kuonyesha ghadhabu zao.
Katika hotuba yake ya ushindi akiwa nje ya ikulu ya rais, bwana Maduro, aliambia wafuasi wake kuwa ushindi wake ni halali na umeambatana na sheria.
Aliongeza kuwa kuchaguliwa kwake kunaonyesha kuwa marehemu Hugo Chavez anaendelea kushinda vita vikuu.
Aliwataka wale waliompigia kura na wapinzani wake kushirikiana kwa niaba ya ya nchi nzima.

No comments:

Post a Comment