Saturday, November 29, 2014
Tibaijuka:"Nilipokea pesa za Escrow"
Mjadala kuhusu kashfa ya uchotaji wa mamilioni ya fedha katika akaunti ya ESCROW ya Benki Kuu ya Tanzania umezidi kuunguruma nchini Tanzania kufuatia taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, PAC, na ripoti ya serikali kuhusu kashafa hiyo.
Mambo yaliyojitokeza katika ripoti ya PAC ni kutaja majina ya viongozi na maafisa wandamizi wa serikali walionufaika na magao huo.
Miongoni mwao ni waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka ambaye alizungumza na mwandishi wetu mjini Dodoma, Ben Mwang'onda ambaye alianza kwa kumuuliza kama kutajwa kwa jina lake alitendewa haki
Source:BBC Swahili
Mambo yaliyojitokeza katika ripoti ya PAC ni kutaja majina ya viongozi na maafisa wandamizi wa serikali walionufaika na magao huo.
Miongoni mwao ni waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka ambaye alizungumza na mwandishi wetu mjini Dodoma, Ben Mwang'onda ambaye alianza kwa kumuuliza kama kutajwa kwa jina lake alitendewa haki
Source:BBC Swahili
KERO BARABARA YA MBOZI CHANG'OMBE
Hii imekuwa kero sasa kwa watumiaji wa barabara ya Mbozi,Chang'ombe viwandani,
Imekuwa ni kama tabia ya kawaida kuwepo kwa mabwawa makubwa ya maji katika eneo maarufu la kilipokuwa kiwanda cha kutengeneza biskuti,
Chakushangaza ni kuwa barabara hiyo inatumiwa na viwanda vikubwa vilivopo katika eneo hilo
kama Azam,Konyagi,Kioo na vingine vingi ambavyo hatujavitaja.
Inasikitisha maana hata wafanyakazi wa viwanda hivyo pia ni waathirika wa tatizo hilo .
Wito wetu mamlaka inayohusika shughulikieni jambo hili ili kutatua kero hiyo.
![](//1.bp.blogspot.com/-c_yqiDS4zDA/VHl2FDExjQI/AAAAAAAADpY/y0GooxokgKg/s1600/IMG_1072.JPG)
Imekuwa ni kama tabia ya kawaida kuwepo kwa mabwawa makubwa ya maji katika eneo maarufu la kilipokuwa kiwanda cha kutengeneza biskuti,
Chakushangaza ni kuwa barabara hiyo inatumiwa na viwanda vikubwa vilivopo katika eneo hilo
kama Azam,Konyagi,Kioo na vingine vingi ambavyo hatujavitaja.
Inasikitisha maana hata wafanyakazi wa viwanda hivyo pia ni waathirika wa tatizo hilo .
Wito wetu mamlaka inayohusika shughulikieni jambo hili ili kutatua kero hiyo.
Bwawa kubwa la maji machafu |
Ni shida hata jinsi ya kuvuka kufika upande wa pili |
Ona waenda kwa miguu wanavyopata shida kuvuka |
baada ya kujaribu kuvuka gari hii ilinasa |
Wasamalia wema wakienda kutoa msaada |
Foleni ya magari yakisubiri kuvuka |
Tuesday, November 11, 2014
MGOGORO WA KANISA LA MORAVIA JIMBO LA KUSINI MAGHARIBI WAIBUKA UPYA OFISI ZA MAKAO MAKUU JIMBO ZAFUNGWA KWA MINYORORO
Baadhi ya Wachungaji na Waumini wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Oktoba 10 majira ya saa 11 jioni walifunga ofisi zote za Makao makuu ya Kanisa hilo zilizopo Jacaranda Jijini Mbeya na kumzuia aliyekuwa Mwenyekiti wa Jimbo Mchungaji Nosigwe Buya kuhama kwenye eneo hilo kwenda nyumba nyingine eneo la Saba saba.
Aliyeyeongoza zoezi hilo ni pamoja na Frank Phili Mtunza hazina wa Kanisa la Moravian Ushirika wa Bethelehem ulioko Mama John Jijini Mbeya akiwa na Mchungaji Mwilgumo pamoja na Mchungaji Mwakyoma.
Ofisi zilzofungwa kwa kutumia minyoro na mbao ni pamoja na ofisi ya Askofu Alinikisa Cheyo,Ofisi ya Katbu Mkuu,Ofisi ya Mtunza Hazina Mkuu na lango kuu la kuingilia makao makuu ya Kanisa hilo.
Hatua hii ya kufunga ofisi za Kanisa ni la pili kwa mwaka huu awali ilikuwa mwezi Julai mwaka huu ambapo waumini hao walifunga hivyo hivyo kabla ya Serikali kuingilia kati na kufanya suluhishi kupitia Kamati ya ulinzi na Usalama ya Wilaya na kuweka makubaliano.
Hata hivyo Phili alidai maagizo yaliyotolewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama hayakutekelezwa ikiwa ni pamoja na kumrudisha kazini Mchungaji Nosigwe Buya na kuacha kumhamisha kituo cha kazi.
Aidha waumini hao walichukua hatua ya kuzuia kuhamishwa kwa Mchungaji Buya ambapo alikuwa amefunga mizigo yake huku mkewe akishindwa kupika na kuwahudumia watoto kwa siku nzima na banda la mifugo limeezuliwa na mtu aliyetumwa kutoka ofisi kuu.
Pamoja na juhudi za Kanisa kujaribu kumhamisha Mchungaji Nosigwe Buya ziligonga ukuta baada ya ya waumini hao wasiozidi ishirini kumuondoa kijana aliyekuwa akiondoa mabati na mabanzi ya banda la mifugo kuondoka mara moja na kumtaka mke wa Mchungaji Buya Edda Kabuka kuendelea na shughuli zake.
Kwa upande wake Mchungaji Buya alisema kuwa hapingi kuondoka katika nyumba hiyo na kukataa kwenda kituo kingine cha kazi lakini ameshangazwa na kwenda kinyume na makubaliano ya kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya lakini kukiukwa maazimio ya yaliyofanyika mwezi Julai mwaka huu.
Pia alidai mgogoro huu umeligawanya Kanisa na kwamba hivi sasa mahubiri yanayofanyika kanisani yamekuwa ya kutpiana maneno kwa pande mbili zinazopingana na kufanya waumini kushindwa kupata ufumbuzi wa kudumu na kudai kuwa suluhu pekee iwe ni kuitisha mkutano mkuu wa Kanisa(Sinodi).
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi alisema amesikitishwa na pande hizo zinazopingana na kwamba ni kwa nini mgogoro huo haupati ufumbuzi licha ya Kamati ya ulinzi na usalama kusuluhisha na kwamba Jeshi la Polisi litamkamata yeyote atakayevunja amani kwani kazi ya Jeshi la Polisi ni kulinda usalama wa Raia na mali zake.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvW3z6_wp8Drf83k4SMNklWCeghpKdYzQv5O_6M0N7qtq1zrv54a5Z0U0L3Ka1eMnnk7vSD2K2GavZHFxYyAtZs9_X0dXYM2g9VYVIquYFiqNAX8jLYHy3eE-AOfbpwcmfcysrqXJn8T4/s640/IMG-20141111-WA0014.jpg)
KWA HISANI YA MBEYA YETU
TOPE LA VOLCANO LASABABISHA MOTO MAREKANI
Moto umetokea katika jimbo la Hawaii Nchini Marekani moto huo umeunguza nyumba ya ilikuwa jirani na eneo ambalo tope hilo la moto lilikuwa likitiririka.wenyeji wa nuyumba hiyo hawakuwepo,tope hilo halikusababisha madhara zaidi.
Picha kwa Hisani ya BBC SWAHILI.
Thursday, November 6, 2014
KIONGOZI WA DINI AUWAWA NCHINI KENYA
Watu wasiojulikani kwenye mji wa pwani nchini Kenya ,Mombasa wamemuua kwa kumpiga risasi kiongozi mashuhuri na mwenye msimamo wa wastani wa dini ya kislamu.
Sheikh Salim Bakari Mwarangi ambaye ni mwanaharakati wa kampeni dhidi ya itikadi kali alipigwa risasi wakati alipokuwa akirudi nyumbani kutoka msikitini jumanne usiku.
Viongozi sita wa dini ya kiislamu badhi yao wenye itikadi kali na wale walio na misimamo ya wastani wameuawa mjini Mombasa tangu mwaka 2012.
Eneo la pwani ya kenya lenye waislamu wengi limekumbwa na misururu ya mashambuli ya mabomu yanoyoaminika kutekelezwa na watu walio na uhusiano na kundi la Al shabaab lenye makao yake nchini Somalia.
Wednesday, November 5, 2014
MKURUGENZI ATAKA ‘CHOMACHOMA’ WADHIBITIWE
MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara, Beatrice Dominic, amewataka Watendaji wa Kata na Vijiji kuwakamata wafanyabiashara wanaonunua korosho kinyume na utaratibu husika wa stakabadhi ghalani kwa madai kuwa wanaikosesha Halmashauri mapato ya ndani.
Agizo hilo amelitoa kwa nyakati tofauti wakati alipokuwa kwenye ziara ya kuhamasisha kilimo wilayani hapa hivi karibuni na kuongozana na wakuu wa idara mbalimbali wa Halmashauri hiyo, lengo likiwa kuangalia namna ya kuwadhibiti walanguzi hao maarufu kama Chomachoma.
Dominic, alisema tabia ya ununuzi holela wa korosho katika Wilaya ya Masasi hasa kipindi cha msimu wa ununuzi wa zao hilo, imeshamiri katika maeneo mbalimbali na kwamba kufanya hivyo ni kinyume na taratibu za ununuzi wa zao hilo.
Alisema kwa sasa utaratibu ambao unatambulika kisheria katika ununuzi wa mazao hasa korosho ni mkulima kwenda kuuzia ghalani na si vinginevyo na kwamba, kama kunawafanyabiashara wanaofanya wanaokwenda kinyume wanapaswa kuacha mara moja.
Mkurugenzi huyo, alisema inashangaza kuona kila mwaka wafanyabiashara hao wakinunua korosho kinyume na utaratibu wa stakabadhi ghalani, huku watendaji wa Kata pamoja na Vijiji wakiwa kimya bila ya kuwakamata na kuwafikisha sehemu husika ili sheria ichukue mkondo wake.
Alionya kuwa hatosita kumwajibisha mtendaji yeyote wa Kata na Kijiji iwapo hatashiriki kikamilifu mpango huo kabambe wa kudhibiti ununuzi huo wa korosho.
chanzo:Tanzania Daima
LILE SAKATA LA MKE KUISHI NA WANAUME WAWILI ZAIDI YA MIAKA 8 LACHUKUA SURA MPYA
Mume halali Rogers Halinga wakiwa na mkewe juliana Hosea kwenye kikao cha ndugu wa mume kijijini Ishungu |
Sakata la mke kuishi na wanaume wawili lachukua sura mpya baada ya kikao cha ndugu wa mume halali Rogers Halinga kuketi kikao Kijiji cha Ishungu Kata ya Ruiwa Mbarali Mkoani Mbeya na kumtaka Biton Mwashilindi kufanya mazungumzo nao kabla hawajafungua madai ya ugoni Mahakani na kudai fidia.
Kikao hicho kizito kilichofanyika nyumbani kwa Baba mzazi wa Rogers Halinga mzee Jason Halinga(95) Novemba mosi mwaka huu na kuhudhuriwa na ndugu lukuki na kumsikiza mke wa Rogers ili abaini ukweli juu ya mtoto aliyezua utata kuwa ni wa nani baina ya Rogers au Biton Mwashilindi.
Mwanamke huyo a(22) akijikanganya mara kadhaa katika kikao hicho akidai kuwa mtoto huyo ni wa Rogers kwa kuwa aliondoka baada ya kutokea mapishano na mumewe akiwa na ujauzito wa miezi minne ndipo alipoanza mahusiano ya kimapenzi na Biton hadi siku anajifungua mwaka 2012 akiwa mikononi mwa Biton ndipo alipoamua kumwandikisha mtoto katika kadi ya kliniki na cheti cha kuzaliwa jina la Biton.
Huku ndugu wakihamaki kutokana na kauli hiyo na kwamba yeye atamke wazi mtoto ni wa nani ndipo Juliana bila aibu kwa Baba Mkwe Mzee Jason Halinga alijibu kuwa mtoto ni wa Biton Mwashilindi,ambapo alimkabidhi mtoto huyo mwishoni mwa mwezi Octoba kwa hiari na wala hakuporwa kama alivyotoa taarifa Polisi.
Kauli hiyo ya Juliana ililazimu kikao kupiga simu kwa mzazi wa Juliana anayeishi Lwanjilo wilayani Chunya kujua mustakabali wa kauli ya mtoto wao kwani ilidaiwa kuwa Biton aliwahi kwenda huko kujitambulisha kuwa yeye anaishi na mtoto wao na kwamba Biton hakujua kuwa Juliana aliwahi kuolewa kwani alidai kuwa yeye ni mwanafunzi wa VETA Mbeya na asimwambie kuwa yeye ni mwanandoa.
Baba mzazi wa Juliana Hosea Mwalukasa alidai kuwa ni kweli Biton alifika kwake lakini hakumpokea kwa kuwa alidai kuwa Juliana ni mke halali wa Rogers Halinga hivyo kama amezaa na Juliana amefanya kosa na kwamba atatozwa ugoni kwani Juliana hakuwahi kupewa talaka na Halinga.
Kikao hicho baada ya mvutano wa muda mrefu kiliamua kuwa endapo Biton anadai kuwa mtoto aliyezaliwa na Juliana aliyefahamika kwa jina la Zalida Biton(2) ni mtoto wake basi alipe fidia ya kuzaa na mke wa mtu kiasi cha shilingi milioni kumi au alipe n'gombe saba ili aweze kumkomboa mtoto wake na kwamba Juliana bado ni mke halali wa Rogers.
Kwa upande wake Biton Mwashilindi alidai kuwa hayuko tayari kulipa pesa hizo na kwamba yeye alikabidhiwa mtoto kihalali na Jeshi la Polisi Ocktoba 31 mwaka huu kituo kikuu cha kat mbele ya maafisa wa Jeshi la Polisi na kwamba hana kesi ya kujibu na kwamba anasubiri tu mtoto afikishe umri wa miaka saba ndipo amchuke.
Katika suala hili baadhi ya wadau wamelalamikia Jeshi la Polisi kwa kuamua masuala ya kisheria katika vituo vya Polisi badala ya mamlaka za kisheria zipo kama mahakama kuliko uamuzi uliotolewa na hali hii husababisha baadhi ya wananchi kujichukulia sheria mkononi.
Wamedai kitendo cha kukabidhiwa mtoto Biton bila kuchukuliwa vipimo vya DNA bado hakujatutua mgogoro huu na kwamba bado suluhu katika ndoa hiyo hiyo itakuwa ni kitendawiri kisicho na majibu.
Kwa hisani ya Mbeya yetu
Monday, October 27, 2014
Msichana asimulia ya Boko Haram
Ni miezi sita sasa baada ya wanamgambo wa kiislam wa kundi la Boko Haram kuwateka wanafunzi wasichana Zaidi ya 200 kaskazini mashariki mwa Nigeria, wasichana watatu ambao wametoroka wamezungumza katika mahojiano maalum na idhaa ya Kihausa ya BBC.
Tukio hili linakuja wakati serikali ya Nigeria ikiwa katika makubaliano ya kusimamisha mapigano dhidi ya Boko Haram hatua itakayo saidia kuwaachilia huru wasichana waliotekwa na kundi hilo .
'' nilikuwa nataka kurukia nje wakati msichana mwenzangu aliponikamata kwa nyuma na kusema watakupiga risasi kama utafanya hivyo. Nikasema, nini utofauti wataniua mimi hapa na kuacha maiti yangu ikusachukuliwa nilikuwa nalia na kuomba mpaka tulipoifikia kambini" Anasimulia msichana mmoja alitoroka mikononi mwa Boko Haram
Akizungumza katika mahojiano maalum na idhaa ya Kihausa ya BBC, Msichana huyu anakumbuka jinsi alivyokuwa nyuma ya Lori wakati wanapinaji wa Boko Haramu walipomteka yeye na wasichana wengine.
Zaidi ya wasichana 200 kati miongoni mwao walikuwa walitekwa lakini wale waliokimbia walibahatika kutoingia katika hofu kubwa kwenye mikono ya watekaji.
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadam la Human Rights Watch limesema wanawake wanaoshikiliwa na kundi la Boko Haramu wamekuwa wakinyanyaswa, kubakwa na hata kulazimishwa kuolewa.
Katika ripoti mpya ya shirika hilo inasema Wanamgambo hao wa Kiislam wamewawateka wanawake Zaidi ya 500 na wasichana tangu mwaka 2009.
Serikali ya Nigeria hivi karibuni imetangaza makubaliano ya kusimamisha mapigano dhidi ya Boko Haram ambayo hatua itakayawafanya wanamgambo ho kuachilia huru wasichana wa hao waliotekwa huko Chibok.
Lakini Boko Haram wenyewe hawajawahi kuthibitisha makubaliano yoyote ya kusitisha mapigano na hakuna dalili zozote za kuachiwa kwa wasichana haohivi karibuni.
Lakini kwa wale waliobahatika kutoroka, matatizo ya kisaikolojia bado yanawasumbua..
Kwa hisani ya BBC Swahili
Monday, October 6, 2014
Monday, September 22, 2014
Maandamano makubwa yaanza Hong kong
Maelfu ya wanafunzi mjini Hong Kong wameanza maandamano ya juma moja kupinga mpango wa serikali ya Uchina ya kuwakagua wagombea wa uchaguzi wa kiongozi wa eneo hilo.
Wengi waliandamana katika chuo kikuu cha Uchina kilichopo mjini humo.
Waliishtumu Uchina kwa kukiuka makubaliano ya kidemokrasia wakati Uingereza ilipoikabidhi uchina eneo hilo mnamo mwaka 1997.
Walimu 300 wa chuo hicho pia wanaunga mkono maandamano hayo,ambayo yanalenga kuanzisha kampeni kubwa ya uasi wa raia.
Uchina imekubali kufanya uchaguzi wa moja kwa moja mnamo mwaka 2017,lakini ina uwezo wa kuwachagua wagombea wachache wanaounga mkono Uchina.
Mkutano mkubwa zaidi umepangwa kufanyika mwezi ujao na kundi la Occupy Central ambalo limeahidi limeahidi kufanya maandamano makubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa HOng kwa niya ya kufunga eneo lote la katikati ya jiji hilo.
Raia 115 wa Afrika ya Kusini walifariki Nigeria
Serikali ya Afrika Kusini inasema kuwa watu miamoja
na kumi na tano wengi wao wakiwa raia wa Afrika Kusini, walifariki baada ya
kanisa kuporomoka nchini Nigeria.
Ndege iliyowabeba manusura wa mkasa huo, kumi na sita kati yao
wakiwa wamejeruhiwa vibaya, imewasili mjini Pretoria.
Zaidi ya watu 300 kutoka Afrika Kusini walikuwa wametembelea
kanisa hilo la 'All Nations in Lagos', ambalo linaongozwa na mhubiri T.B.
Joshua.
Inaarifiwa jengo hilo liliporomoka kutokana na ujenzi mbovu.
Mhubiri TB Joshua, amezua wasiwasi baada ya kuzungumzia kuona
ndege iliyokuwa inazunguka juu ya kanisa hilo kabla ya jengo lenyewe
kuporomoka.
Saturday, September 20, 2014
Balozi Sefue afunguka Katiba Mpya
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue amesema hakuna
uwezekano wa kubadili muundo wa muungano kutoka Serikali mbili kwenda Serikali
tatu katika mchakato wa Katiba.
Kauli ya Balozi Sefue imekuja ikiwa ni siku chache tangu Rais
Jakaya Kikwete kukutana na viongozi wa Kituo cha Demokrasia (TCD) na kutoa
uamuzi wa kuahirisha mchakato wa Katiba hadi baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka
2015.
Suala la muundo wa muungano lilichukua mjadala mkali ndani ya
Bunge Maalumu la Katiba huku wajumbe wanaounda kundi la Ukawa wakiunga mkono
mapendekezo ya Rasimu ya Katiba ya muundo wa Serikali tatu na wajumbe wa CCM
wakisisitiza muundo wa Serikali mbili.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na gazeti hili, Balozi
Sefue alisema mchakato wa Katiba unahitaji maridhiano, lakini suala la muundo
wa muungano halina maridhiano katika jamii hivyo litachelewesha upatikanaji wa
Katiba:
“Katika historia ya nchi yoyote, wakati unafika wananchi wakawa
na maridhiano fulani, wakaamua kuyaingiza ndani ya Katiba. Tatizo linajitokeza
pale watu au makundi fulani yanapong’ang’ania kuingiza ndani ya Katiba mambo
ambayo ni dhahiri hayana maridhiano ndani ya jamii. Mfano ni suala la muundo wa
Muungano,” alisema na kuongeza:
“Uzoefu wa Bunge Maalumu hadi sasa ni kuwa hakuna uwezekano wa
kupata maridhiano ya kubadili muundo wa Muungano kutoka Serikali mbili kwenda
tatu. Hutapata maridhiano hayo ndani ya Bunge Maalumu na hutapata maridhiano
ukienda kwa wananchi,” alisema.
Alisema anaamini wajumbe wa Bunge Maalumu walifanya uamuzi wa
busara kuliweka kando jambo hilo linalotugawa, na kuendelea kujadili Rasimu ya
Katiba kwa msingi wa mfumo uliopo wa Serikali mbili,” alisema.
Balozi Sefue aliongeza kuwa tangu suala hilo liwekwe kando
kumekuwa na kasi na matumaini ya kupata Katiba Mpya.
Alisema jambo hilo ni kubwa na uzoefu unaonyesha lina uwezo
mkubwa wa kutugawa na kuchelewesha kupatikana kwa Katiba Mpya.
Balozi Sefue alisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliamini
yatapatikana maridhiano kuhusu kubadili muundo wa Muungano, ilivyo sasa, ni
wazi kuwa maridhiano kuhusu mabadiliko hayo hayapo na hayatapatikana.
“Hakuna idadi ya makongamano na maandamano yatakayobadili hali
hiyo sasa,” alisema.
Licha ya kusema kuwa kuna matumaini ya kupata Katiba Mpya,
Balozi Sefue alisema ikishindikana Katiba iliyopo itafanyiwa marekebisho ili
ituvushe hadi mchakato utakaporejeshwa tena.
Kwa hisani ya http://www.mwananchi.co.tz/
RAISI WA UEFA AGOMA KURUDISHA SAA
Rais wa shirikisho la soka barani Ulaya UEFA Michel Platini |
Rais wa shirikisho la soka barani Ulaya UEFA Michel Platini amesisitiza
kuwa hatorejesha saa yenye thamani ya Yuro elfu kumi na sita aliyopewa kama
zawadi na shirikisho la soka nchini Brazil CBF.
Shirikisho
la soka duniani FIFA limewataka maafisa wote waliopewa saa hizo katika kombe la
dunia kuzirudisha kwa kuwa zawadi hizo zinakiuka maadili ya sheria za FIFA.
Lakini
Platini mwenye umri wa miaka 59 amesema yeye hawezi kurudisha zawadi.
Platini
amesema kuwa FIFA ilikuwa na habari kwamba zawadi hizo zilitolewa mnamo mwezi
juni ,lakini akashangazwa ni kwa nini shirikisho hilo halikuchukua hatua wakati
huo.
Saa
hizo zilitolewa na mmoja ya wafadhili wa shirikisho la soka
UFARANSA YAFANYA MASHAMBULIO DHIDI YA DOLA YA KIISLAMU
Ikulu ya Ufaransa imetangaza ijumaa wiki hii kwamba ndege zake za kijeshi zimeshambulia kwa mara ya kwanza ngome za wapiganaji wa Dola la Kiislam kaskazini mashariki mwa Iraq.
Ufaransa inashiriki katika vita vingine dhidi ya wapiganaji wa Dola la Kiislam nchini Iraq na Syria, baada ya kutuma wanajeshi wake nchini Mali na Jamhuri ya Afrika ya Kati. Ufaransa ni taifa la pili lenye nguvu duniani kuingia katika vita nchini Iraq, ikiiunga mkono Marekani katika vita vyake dhidi ya wapiganaji wa Dola la Kiislam.
Tangazo hilo la Ikulu ya Paris limebaini kwamba mashambulizi ya kwanza yameendeshwa katika baadhi ya maeneo mapema ijumaa wiki hii. Ndege za kijeshi zimekua zikilenga ngome za wapiganaji wa Dola la Kiislam kaskazini mashariki mwa Iraq.
Tangazo hilo limethibitisha kwamba ghala la vifaa vya kijeshi vya wapiganaji wa Dola la Kiislam limeteketezwa na mashambulizi hayo, huku likibaini kwamba mashambulizi hayo yataendelea hivi karibuni. Ndege hizo ziliyoendesha mashambulizi hayo zimerejea kwenye vitu vyao viliyotengwa katika mji wa Abou Dhabi kwenye umbali wa kilomita 1500 na eneo lililoshambuliwa.
Kwa mujibu wa wizara ya ulinzi, operesheni dhidi ya wapiganaji wa Dola la Kiislam imeendeshwa katika jimbo la Mossoul, nchini Iraq. Mashambulizi hayo yameendeshwa na ndege mbili za kijeshi ambazo zimekua zimebeba mabomu aina ya GBU 12, na aina nyingine ya ndege yenye chapa C-135FR pamoja na ndege nyingine ambayo imekua ikisaidia kupiga doria kwenye bahari Atlantic 2.
Mashambulizi hayo ya anga yametekelezwa chini ya uongozi wa jeshi la Ufaransa kwa ushirikiano na viongozi wa Iraq pamoja na washirika wa Ufaransa katika jimbo hilo, wizara ya ulinzi imebaini .
Alhamisi wiki hii katika mkutano na waandishi wa habari, rais wa Ufaransa François Hollande, alibaini kwamba muda umewadia wa kuanzisha mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Dola la Kiislam.
Tangazo hilo la Ikulu ya Paris limebaini kwamba mashambulizi ya kwanza yameendeshwa katika baadhi ya maeneo mapema ijumaa wiki hii. Ndege za kijeshi zimekua zikilenga ngome za wapiganaji wa Dola la Kiislam kaskazini mashariki mwa Iraq.
Tangazo hilo limethibitisha kwamba ghala la vifaa vya kijeshi vya wapiganaji wa Dola la Kiislam limeteketezwa na mashambulizi hayo, huku likibaini kwamba mashambulizi hayo yataendelea hivi karibuni. Ndege hizo ziliyoendesha mashambulizi hayo zimerejea kwenye vitu vyao viliyotengwa katika mji wa Abou Dhabi kwenye umbali wa kilomita 1500 na eneo lililoshambuliwa.
Kwa mujibu wa wizara ya ulinzi, operesheni dhidi ya wapiganaji wa Dola la Kiislam imeendeshwa katika jimbo la Mossoul, nchini Iraq. Mashambulizi hayo yameendeshwa na ndege mbili za kijeshi ambazo zimekua zimebeba mabomu aina ya GBU 12, na aina nyingine ya ndege yenye chapa C-135FR pamoja na ndege nyingine ambayo imekua ikisaidia kupiga doria kwenye bahari Atlantic 2.
Mashambulizi hayo ya anga yametekelezwa chini ya uongozi wa jeshi la Ufaransa kwa ushirikiano na viongozi wa Iraq pamoja na washirika wa Ufaransa katika jimbo hilo, wizara ya ulinzi imebaini .
Alhamisi wiki hii katika mkutano na waandishi wa habari, rais wa Ufaransa François Hollande, alibaini kwamba muda umewadia wa kuanzisha mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Dola la Kiislam.
Uhuru Kenyatta atakiwa mahakamani ICC 8,Octoba
Mahakama
ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imemtaka raisi
wa Kenya Uhuru Kenyatta kufika
mahakamani tarehe 8 mwezi Oktoba licha ya majaji wanaotarajiwa kusikiliza kesi
dhidi yake kuiahirisha.
majaji katika mahakama hiyo wanataka
kumhoji juu ya madai kwamba serikali yake imeficha hati iliyoombwa na waendesha
mashitaka wanaosikiliza kesi yake ya uhalifu dhidi ya ubinadamu.
Kesi hii imekuwa ikicheleweshwa mara
kadhaa sasa.hata hivyo raisi kenyata amekanusha kuandaa mauaji ya kikabila
baada ya uchaguzi mwaka 2007.
Takribani watu elfu moja mia mbili
waliuawa na laki sita kuyakimbia makazi yao.
Wiki mbili zilizopita, waendesha
mashitaka waliomba kesi dhidi yake kuahirishwa kwa muda usiojulikana, kwa vile
hawakuwa na ushahidi wa kutosha kwa sababu ya serikali ya Kenya kuweka vizuizi.
Friday, September 19, 2014
Ebola:MAAFISA WA AFYA WALIUAWA
Viongozi nchini Guinea wamesema tayari
wamepata maiti kadhaa za timu ya wahudumu wa afya pamoja na wanahabari
waliotoweka walipokuwa wakiendeleza harakati za kuwaelimisha na kuwahamasisha
wananchi kuhusu ugonjwa wa Ebola.
Msemaji wa serikali ya Guinea amesema kati ya miili hiyo ni ile
ya wanahabari watatu wa timu hiyo.
Timu hiyo ilisemekana kupotea baada ya kushambuliwa hapo jumanne
katika kijiji kimoja kilicho karibu na Mji wa Nzerekore ulio kusini mwa Guinea.
Mlipuko wa Ugonjwa huo ndio hatari zaidi kote duniani kwa sasa,
huku viongozi wakitahadharisha kwamba huenda watu zaidi ya 20,000
wakaambukizwa.
Timu hiyo ya madaktari watatu na wanahabari watu walipotea baada
ya kushambuliwa kwa mawe na wakaazi wa kijiji cha Wome, walipofika katika
kijiji hicho kilicho karibu na mahala ambapo mlipuko wa Ebola ulianzia.
Kwa mujibu wa mwanahabari mmoja aliyeweza kunusurika aliwaambia
wanaripota kwamba alipokuwa amejificha, aliweza kusikia wakaazi hao wa Wome
wakiwatafuta.
Wajumbe wa serikali wakiongozwa na Waziri wa Afya walitumwa
maeneo hayo lakini hawangeweza kufika kwa kutumia barabara kwani daraja
lilikuwa limewekwa vizuizi.
Hapo Alhamisi msemaji wa serikali ya Guniea Albert Damantang
Camara alithibitisha kwamba maiti nane zilikuwa zimepatikana na miongoni mwa hizo
zilikuwa zile za wanahabari watatu.
Alieleza ya kwamba miili hiyo ilipatikana katika pipa moja la
shule ya msingi iliyo katika kijiji hicho, na kuongeza kuwa timu hiyo iliuawa
kinyama na wakaazi hao.
kwa hisani ya bbcswahili.com
NI MTIKISIKO
MTIKISIKO mkubwa wa kisiasa jana
umelikumba taifa, baada ya wafuasi wa Chadema kupambana na polisi katika maeneo
mbalimbali.
Hali hiyo,
ilianza kuonekana mapema jijini Dar es Salaam, wakati Mwenyekiti wa Chadema,
Freeman Mbowe aliwapowasili Makao Makuu ya Jeshi la Polisi saa tano asubuhi kwa
ajili ya kuhojiwa.
Mbowe
aliitwa kuhojiwa na viongozi wa jeshi hilo kwa madai ya kutoa kauli za
uchochezi wiki iliyopita.
Akizungumza kwenye mkutano wa
Kamati Kuu ya chama chake, Mbowe alisema wataitisha maandamano na migomo
isiyokuwa na kikomo nchi nzima kuishinikiza Serikali kusitisha Bunge Maalumu la
Katiba linaloendelea mjini Dodoma.
Mbowe
aliwasili polisi saa 5 asubuhi akisindikizwa na msafara wa magari matano
yaliyobeba baadhi ya wanachama, mawakili na viongozi wa chama hicho.
Baada ya
kuwasili katika eneo hilo, wanachama hao walipinga kiongozi wao kushuka ndani
ya gari hadi atakapoingia ndani ya lango kuu.
Wanachama
hao walisikika wakisema ‘Peoples’ huku wengine wakiitikia ‘Power’.
Kitendo
hicho kilipingwa na polisi waliokuwa wakilinda lango hilo na kuamuru Mbowe
ashuke na kuingia kwa miguu ndani ya jengo hilo.
Kitendo
hicho kilionekana kuwakera wafuasi waliokuwa wamekusanyika eneo hilo na kuamua
kusukuma lango hilo kwa nguvu ili waweze kuingia pamoja na kiongozi wao.
Kutokana
na hali hiyo, wafuasi hao waligoma na kuanza kupambana na polisi ambao nao
walijihami kwa kuzuia geti la lango wakiwa ndani.
Baada ya
mabishano ya muda mrefu, ndipo polisi walipokubali Mbowe aingie na gari ndani
ya jengo hilo huku wakizuia msafara wa magari mengine.
Kutokana
na uamuzi huo, mawakili walilazimika kushuka ndani ya gari.
Mmoja wa
askari aliyekuwa getini hapo, alisikika akisema anayepaswa kuingia ndani ya
jengo ni Mbowe na mawakili wake.
“Tumekubaliana
gari linaloingia ndani ni moja tu la mwenyekiti, msilazimishe matumizi ya
nguvu,” alisikika akisema askari huyo.
Kitendo
hicho kilipingwa na wanachama hao huku wakitaka wabunge, mawakili na viongozi
wengine waingie ndani.
Kutokana
na hali hiyo, polisi walikubali na kuwaruhusu viongozi hao kuingia ndani huku
wakiwaamuru wanachama wengine na waandishi wa habari kusimama umbali wa mita
200 kutoka kwenye lango hilo.
Baada ya
kutokea kwa tangazo hilo, wafuasi hao walikaidi amri hiyo na kusababisha askari
D. D. Zahoro kuamuru kutumika nguvu kuwatawanya pamoja na waandishi wa habari
hali iliyosababisha kujitokeza kwa vurugu katika eneo hilo.
Vurugu
hizo zilidumu kwa muda wa saa moja na kusimamisha shughuli mbalimbali
zinazoendelea ndani ya jengo hilo na njia kufungwa kwa muda.
Katika
vurugu hizo,wafuasi wanne wa chama hicho walikamatwa.
MWANDISHI
APIGWA
Katika
tukio hilo, mwandishi wa habari wa Gazeti la Tanzania Daima, Josephat Isango
alijikuta akishambuliwa vibaya na askari kwa virungu.
Licha ya
Isango kuonyesha kitambulisho, polisi hawakutaka kumsikiliza zaidi ya kuendelea
kumshushia kipigo na kumsababishia maumivu katika mguu wa kulia.
Kipigo
hicho kilisitishwa baada ya waandishi wengine kupiga kelele kuwaomba polisi
kumwachia kwa sababu alikuwa kwenye majukumu yake ya kazi.
MBOWE
AHOJIWA
Wakati
tukio hilo likiendelea, Mbowe alikuwa ndani ya jengo hilo akiendelea
kuhojiwa akiwa na mawakili wake sita.
Mawakili
hao, ni Peter Kibatala, Profesa Abdallah Safari, Mabere Marando, Nickson
Tugala, Tundu Lissu na John Malya.
Mahojiano
hayo yalianza saa tano na kudumu kwa zaidi ya saa nne. Ilipofika saa 8:49
mchana, mawakili wanne wakiongozwa na Lissu walitoka nje na kuzungumza na
wafuasi na waandishi wa habari.
“Mwenyekiti
yuko salama, aliitwa kwa ajili ya mahojiano na yamefanyika vizuri chini ya
mawakili.
“Polisi
wameomba tuzungumze na nyie tuwaombe muondoke kwa sababu mwenyekiti akitoka na
mkiwa wengi kunaweza kukawa na uvunjifu wa amani,” alisema Lissu.
Baadhi ya
wanachama hao walisikika wakisema hawawezi kuondoka kwa sababu hawawaamini
polisi.
“Sisemi
nawaamini polisi au la, tumekubaliana kwamba mwenyekiti atapata dhamana, hivyo
haitakuwa busara tukiondoka kwa maandamano, tulikuja kwa amani hatutaki mtu
atoke hapa akiwa amedhurika,” alisema Lissu.
Baadhi ya
wafuasi walikubali kuondoka huku wengine wakibaki.
Saa 9:17
alasiri, Mbowe alitolewa kwa kupitia mlango wa nyuma wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, huku akisindikizwa na magari manne kwenda Kituo cha Polisi Kati
ambako aliachiwa kwa dhamana.
MTIKILA
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila alifika eneo hilo akiwa kwenye bajaj, lakini alizuiwa kuingia ndani.
Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila alifika eneo hilo akiwa kwenye bajaj, lakini alizuiwa kuingia ndani.
DODOMA
Polisi
mjini Dodoma, jana waliimarisha ulinzi kwa ajili ya kupambana na wafuasi wa
Chadema waliopanga kuandamana kupinga Bunge Maalumu la Katiba linaloendelea
mjini humo.
Miongoni
mwa maeneo yaliyokuwa na ulinzi mkali ni pamoja na jengo la Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Viwanja vya Nyerere Square na mitaa mbalimbali ya mjini
hapo.
Polisi
waliweka uzio wa kamba kilipo Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) na makutano ya
barabara jirani na stendi ya mabasi ya abiria yanayokwenda mikoani ili
kutoruhusu watu na magari kuelekea eneo la Bunge.
Jengo la
Bunge lilikuwa limezungukwa na askari wengi wenye silaha, farasi na mbwa
kuhakikisha usalama unakuwapo katika eneo hilo.
Ndani ya
eneo la Bunge, nako ulinzi ulikuwa mkali kwani kulikuwa na idadi kubwa ya
askari waliokuwa na silaha pamoja na mbwa.
Viwanja
vya Nyerere
Katika
viwanja vya Nyerere ambako wakazi wa Dodoma hupenda kukusanyika kwa ajili ya
kupumzika na kupata huduma za chakula na vinywaji, jana shughuli zilisimama kwa
muda kwa kuwa polisi walikuwa wameweka ulinzi tangu asubuhi.
Nje ya
viwanja hivyo, kulikuwa na vijana waliokuwa na mabango likiwamo lililosomeka
‘Sitta tumia busara ahirisha Bunge la Katiba’.
Katika
viwanja hivyo, polisi walionekana wakiwa wamekamata vijana wapatao kumi
waliodaiwa kuwa walikuwa wakitaka kuandamana.
Wakati
hali ikiwa hivyo katika maeneo hayo, ulinzi pia uliimarishwa katika mitaa
mbalimbali ya mji huo kwani askari polisi waliokuwa na silaha na askari kanzu,
walikuwa wametanda kila kona.
Chini ya
ulinzi huo, magari yaliyokuwa yamejaa askari polisi yakiwamo ya askari wa
Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), yalikuwa yakizunguka kila kona kuhakikisha
hakuna maandamano yatakayofanyika.
Gari la
Chadema
Pamoja na
askari kuimarisha ulinzi huo, gari la Chadema lenye namba za usajili T 792 CAX
likiwa na nembo ya M4C, nalo lilikuwa likipita katika mitaa ya mji huo ingawa
haikufahamika lilikuwa likifanya hivyo kwa maana gani.
Kuanzia
saa 12 alfajiri jana, ofisi za Chadema Mkoa wa Dodoma zilizoko eneo la Mji
Mpya, zilikuwa zikilindwa na askari polisi waliokuwa na silaha.
Radio za
kijamii zafungwa
Katika
hali ambayo haikujulikana wazi, radio za kijamii za mjini hapa hazikuwa hewani
jana asubuhi kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kudhibiti mawasiliano kati ya
Chadema na wananchi.
Taarifa
zilizopatikana baada ya mawasiliano hayo kukatika, zinasema redio hizo hazikuwa
hewani kwa saa kadhaa jana kwa vile viongozi wa Chadema walikuwa wakizitumia
kuhamasisha wananchi.
Miongoni
mwa waliodaiwa kutumia redio hizo ni Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Dodoma,
Jella Mambo ambaye awali alihamasisha maandamano hayo kupitia Redio Kifimbo na
Nyemo FM.
Hata
hivyo, taarifa nyingine zinasema redio hizo hazikuwa hewani kwa kuwa Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA) walikuwa wakifanya marekebisho ya masafa.
Akizungumza
na MTANZANIA jana, Mambo alikiri kutumia redio hizo kuhamasisha maandamano kwa
kuwa yalikuwa halali.
Pamoja na
hayo, alisema kama Jeshi la Polisi limedhamiria kudhibiti maandamano yao,
linatakiwa kuandaa fedha nyingi ili kukabiliana nayo.
“Hapa
Dodoma maandamano yapo ila tunayafanya kimkakati kwani watu wametawanyika
maeneo mbalimbali kila mmoja ana mabango yenye ujumbe tofauti, yakiwamo
tunayompongeza Rais Jakaya Kikwete kwa busara yake aliyoitumia kutaka mchakato
wa Katiba Mpya usikamilike kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015,” alisema
Mambo.
Wakati huo
huo, Mambo alisema gari moja la Chadema lililokuwa limebeba wajumbe wa Mkutano
Mkuu waliokuwa wakitoka Dar es Salaam kuelekea Mwanza, lilikamatwa na askari
polisi.
Kaimu
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Emannuel Lukura alikiri kukamatwa kwa gari na
wafuasi wanne wa chama hicho.
MBEYA
Habari
kutoka mkoani Mbeya, zinasema polisi wameendelea kutunushiana misuli na Chadema
kuhusu kufanyika au kutofanyika kwa maandamano ya kupinga kuendelea kwa Bunge
Maalumu la Katiba.
Chadema
imesisitiza kufanyika kwa maandamano hayo leo. Mratibu Kanda za Nyanda za Juu
Kusini, Franky Mwaisumbe aliliambia MTANZANIA jana kuwa licha ya polisi kudai
kuwa maandamano hayo ni batili, wao watahakikisha yanafanyika kwani lengo lao
ni kufikisha ujumbe kwa wananchi.
Alisema
wao wanachokifanya ni kutimiza azimio la Kamati Kuu lililotolewa wiki iliyopita
na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, alisema hadi jana jioni maandamano hayo
yalikuwa hayajaombewa kibali.
ARUSHA
Mkoani
Arusha, Chadema kimethibitisha kufanya maandamano leo, huku kikisema tayari
majimbo 14 kati ya 33 yamewasilisha barua katika vituo vya polisi kwa ajili ya
taarifa.
Katibu wa
Kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa akizungumza na MTANZANIA kwa njia ya simu
jana, alisema tayari wamekwishajipanga kuhakikisha wanafanya maandamano ya
amani ambayo hayatasababisha usufumbufu kwa watu wala kuvunja sheria yoyote.
“Lengo
letu ni ujumbe ufike kwa wabunge Dodoma, kwamba kikao wanachoendelea nacho
hakitatupa Katiba mpya. Sasa maandamano haya tumeyapa kwa mfumo wa pekee
kabisa,” alisema.
Habari hii
kwa hisani ya Gazeti la Mtanzania
SAA ZA GHARAMA ZAWAPONZA MAOFISA WA FIFA
Shirikisho la soka la dunia FIFA, limewaambia viongozi wanaounda kamati
ya utendaji na viongozi wengine wa juu wa shirikisho hilo kurejesha saa
zipatazo 65 za gharama walizopokea kama zawadi kipindi cha kuelekea kombe la
dunia huko Brazil mwaka huu.
FIFA
imesema kitendo cha kurejesha saa hizo ni kutunza nidhamu.
Saa
hizo zinakadiriwa kuwa na gharama ya dolla elfu ishirini na tano kila moja na
zinatakiwa ziudishwe Octoba 24 ,mwaka huu.
Saa
hizo za kumbukumbu ya Parmigiani ziligawiwa na shirikisho la soka la Brazili
(CBF) wakati wa mkutano wa maandalizi wa FIFA uliofanyika mjini Sao Paulo.
FIFA
imesema kuwa kanuni za maadili zinazuia viongozi kupokea zawadi ambazo
zinathamani zaidi au zenye kuonesha ishara fulani.
Inasemekana
kwamba saa hizo zitatolewa kwa taasisi zinazojitegemea na si sile zinazojali
maslahi huko Brazili.
SCOTLAND YAKATAA UHURU KWA KURA YA KIHISTORIA
Raia wa Scotland wamefanya uamuzi wa mwisho kuwa wataendelea kubaki sehemu ya
Uingereza , raia kwa pamoja wamekataa uhuru wa Scotland.
Maeneo
31 kati ya 32 wamepika kura ya HAPANA siku ya Alhamisi na kuongoza kwa kura
1,914,187 dhidi ya 1,539,920.
Ushindi
huo ni asilimia 55 dhidi ya 45 waliokuwa wakiunga mkono hatua ya kujitenga.
Waziri
Kiongozi wa Scotland Alex Salmond amesema ameridhia kuanguka katika mchakato wa
kura ya maoni.
Tuesday, August 19, 2014
Ebola:Wagonjwa 17 wapatikana Monrovia
![]() |
Mmoja wa wanaume waliovamia kituo hicho na kumbeba mgonjwa |
Waziri wa habari wa Liberia Lewis Brown amesema kuwa wagonjwa wote 17 wa Ebola waliokuwa wametoweka kutoka kwa kituo cha kuwatenga na umma wamepatikana.
Kupatikana kwao imekamilisha idadi ya wote 37 waliokuwa katika zahanati iliyovamiwa na wenyeji jumamosi iliyopita.
Waziri Brown ameviambia vyombo vya habari kuwa wote walijipeleka katika hospitali kuu ya JFK katika mji mkuu wa Monrovia.Wagonjwa 37 walikuwa katika kituo hicho cha Ebola kilichoko karibu na kitongoji cha WestPoint Viungani mwa mji mkuu wa Monrovia kabla ya wenyeji kukivamia na kuwaachilia huru wagonjwa waliokuwemo kabla ya kukipora.
Awali waziri huyo alielezea kutamaushwa kwake na wizi huo ambao alisema ni jambo la kipuzi kujishirikisha na wagonjwa wa Ebola ilihali watu wengi tu wamepoteza maisha yao.
'' tukio hilo la WestPoint ni la kuvunja moyo sana maanake inahujumu juhudi zetu zote za kuzuia kuenea kwa homa hii ya Ebola,natumai tutarekebisha hali hii'' alisema bwana Brown.
20 waliosalia wako katika zahanati mbalimbali karibu na mji mkuu Monrovia .
Zahanati moja inaendeshwa na Hospitali kuu ya John F. Kennedy ilihali wengine wako katika zahanati ya ELWA nje ya mji huo.
Wote hao watachunguzwa kabla ya hatua madhubuti kuchukuliwa kwa maslahi ya Umma.
Katika hatua ya kushtua sana wakaazi wa vitongoji vya mji wa Monrovia walivamia zahanati hiyo iliyokuwa ikitumika kama kituo cha kuwatenga wagonjwa wa homa ya Ebola wakaipora na kuwaruhusu wagonjwa kutoroka.
''Kwa sasa tunashughulikia hali hii ilivyo kwani watu sasa wamerejea miongoni mwa jamii na hivyo kueneza maambukizi zaidi''
Zaidi ya watu 17 bado hawajulikani waliko baada ya kutoroka kutoka kituo cha kuwatenga wagonjwa wa Ebola.
''Kufuatia uvamizi huo tumejifunza mengi ''
Ajabu ni kuwa watu walikuja ndani ya kituo hicho walijileta huko wenyewe kwa hivyo sisi tunachukulia kuwa labda wagonjwa hao walitaka kusalia huko lakini wakalazimishwa kutoroka kukimbilia maisha yao kwa sababu wavamizi walikuwa wanapora mali ya Westpoint.
Brown alisema kuwa kwa sasa zahanati hiyo ya Westpoint Imefungwa lakini kuna mipango ya kuifungua tena.
''Tunafahamu kuwa kuna watu ambao bado wanashauku iwapo Ebola ipo ama hakuna lakini ukitizama takwimu kutoka jimbo la Lofa utaona kuwa idadi ya wahasiriwa imeanza kupungua.''
Lofa ndiyo iliyokuwa kitovu cha mlipuko ulioko sasa wa homa hii ya Ebola.
Zaidi ya watu 17 bado hawajulikani waliko baada ya kutoroka kutoka kituo cha kuwatenga wagonjwa wa Ebola.
Taharuki ilitanda kote nchini humo ,baada ya kituo kilichotengwa na kuwekewa kwa sababu ya kutoa matibabu kwa wagonjwa wa Ebola, kilishambuliwa na zana kuporwa katika mji mkuu wa Liberia, Monrovia.
Watu 37 waliowekwa hapo kuangaliwa kama wana dalili za Ebola walitoroka baada ya kituo hicho kuporwa Jumamosi usiku.
Washambuliaji walipora magodoro na vitu vingine.
Mafisa wakuu nchini Liberia wanajaribu kuwatafuta wagonjwa waliotoroka ili kuwarejesha tena kwenye kituo hicho.
Watu zaidi ya 400 wamekufa kwa sababu ya ebola nchini Liberia kati ya zaidi ya 1,000 katika kanda ya Afrika Magharibi.
Subscribe to:
Posts (Atom)