Shirikisho la soka la dunia FIFA, limewaambia viongozi wanaounda kamati
ya utendaji na viongozi wengine wa juu wa shirikisho hilo kurejesha saa
zipatazo 65 za gharama walizopokea kama zawadi kipindi cha kuelekea kombe la
dunia huko Brazil mwaka huu.
FIFA
imesema kitendo cha kurejesha saa hizo ni kutunza nidhamu.
Saa
hizo zinakadiriwa kuwa na gharama ya dolla elfu ishirini na tano kila moja na
zinatakiwa ziudishwe Octoba 24 ,mwaka huu.
Saa
hizo za kumbukumbu ya Parmigiani ziligawiwa na shirikisho la soka la Brazili
(CBF) wakati wa mkutano wa maandalizi wa FIFA uliofanyika mjini Sao Paulo.
FIFA
imesema kuwa kanuni za maadili zinazuia viongozi kupokea zawadi ambazo
zinathamani zaidi au zenye kuonesha ishara fulani.
Inasemekana
kwamba saa hizo zitatolewa kwa taasisi zinazojitegemea na si sile zinazojali
maslahi huko Brazili.
No comments:
Post a Comment