Huwezi kufikiria umiliki wa kampuni kabla ya kufikiria kuhusu mtaji wa kampuni. Mtaji wa kampuni ni suala nyeti kwa wenye wazo la kumiliki kampuni au wanaomiliki kampuni tayari. Mtaji ndio kila kitu katika kampuni. Tangu unapokuwa katika harakati za kusajili kampuni utalisikia neno hili mtaji karibia katika kila hatua unayopita. Niseme mapema kuwa mtaji mdogo ndio kampuni ndogo na mtaji mkubwa ndio kampuni kubwa. Kwa hili mitaji imegawanyika mara mbili upo mtaji wa maandishi unaokuwa kwenye katiba na waraka wa kampuni( MEMAT) na upo mtaji wa mali halisi ( physical assets)
Soma zaidi.http://sheriayakub.blogspot.com/2015/05/unafahamu-nini-kuhusu-mtaji-wa-kampuni.html
Monday, May 18, 2015
Saturday, May 16, 2015
Raisi wa Burundi Pierre Nkurunziza aonya juu ya jaribio lingine lolote la mapinduzi
Raisi wa Burundi Pierre Nkurunzizaamewatangazia raia wake
kuwa sasa amani imerejea nchini humo ikiwa ni siku tatu baada ya kushindwa kwa
jaribio la mapinduzi ya kijeshi.
Akihutubia
wananchi kupitia runinga Pierre Nkurunziza ametoa onyo juu ya jaribio lingine
lolote la kuchukua madaraka kwa nguvu litasababisha vita umasikini na majanga
yalikwisha onekana katika taifa hilo.
Hayo
yanajiri wakati Marekani ikitoa onyo hapo jana kwa raisi wa Burundi Pierre
Nkurunziza kuhusu kutowania muhula wa tatu wa uongozi kwa vile kutazorotesha
usalama nchini humo na kutishia misaada ya kimataifa.
Msemaji
wa Washington Jeff Rathke ameeleza kuwa Marekani inawasiwasi kufuatia uwezekano
wa kutokea ghasia zaidi baada ya raisi Nkurunziza kurejea nchini Burundi.
Msemaji
wa washington amesema kuwa marekani bado inamtambua Nkurunzinza kama raisi
halali wa Burundi licha ya kusisitiza kiongozi huyo kutowania muhula wa tatu.
Baadhi ya
maafisa wa kijeshi walioshiriki kuongoza mapinduzi wamekamatwa huku wengine
wakitokomea na kusakwa na majeshi tiifu kwa serikali akiwemo kiongozi wa mapinduzi
hayo Generali Godefroid Niyombare, ambaye awali aliiambia AFP kuwa
angejisalimisha kwa serikali.
TFF waigeuka kauli yao, sasa waibebesha msalaba CECAFA kuhusu Simba, Mbeya City
SHIRIKISHO la soka
Tanzania, TFF, limeshindwa kuthibitisha moja kwa moja kama ni Simba au Mbeya
City fc itakayoshiriki kombe la klabu bingwa Afrika mashariki na kati, maarufu
kwa jina la ‘Kagame Cup’ linalotarajia kuanza kutimua vumbi Julai 11 hadi
Agosti 2 mwaka huu jijini Dar es salaam.
Katibu mkuu wa TFF,
Mwesigwa Selestine ameuambia mtandao huu kuwa CECAFA ndio watakaosema ni timu
gani ya tatu nchini Tanzania wameialika kushiriki Kagame.
Kauli hii
inatofautiana na ile aliyowahi kusema kupitia mtandao huu kuwa TFF wameichagua
Simba badala ya washindi wa tatu wa msimu wa 2013/2014 wa ligi kuu soka
Tanzania bara, Mbeya City fc.
“Kimsingi na kwa
taratibu wawakilishi wa Tanzania ni bingwa wa msimu uliopita (2013/2014) ambao
ni Azam na mshindi wa pili ambaye ni Yanga anayefaidika na uenyeji wa
Tanzania”. Amesema Mwesigwa na kuongeza: “Lakini Cecafa ina nguvu ya kuingiza
klabu nyingine kutoka nchi mwenyeji au kutoka ukanda mwingine wa
Cecafa. Watakaocheza ni Azam na Yanga, lakini tunategemea kupokea taarifa
ya Cecafa kujua ni timu gani zimetumiwa mialiko. Cecafa yenyewe itathibitisha
kuwa ni nani wa ziada wamemualika, lakini wanaoingia moja kwa moja kwa Tanzania
kwa vigezo ni Azam (bingwa) na Yanga wanaofaidika na uenyeji wa Tanzania”.
Kauli hii inakinzana
na kauli ya Mwesigwa aliyosema na kukaririwa na mtandao huu aprili 29 mwaka huu
akisema Simba wamechaguliwa kuwakilisha Tanzania.
“Mbeya City
walistahili, lakini niseme ukweli, tumeamua kumchukua Simba, kwanini? kwasababu
ya rekodi yake. Amekuwa bingwa mara nyingi wa mashindano haya, kwahiyo ana
nafasi yake sio katika Tanzania tu bali ukanda mzima, na huwezi
kumuondoa”. Alisema Mwesigwa na kuongeza: “Mwaka jana baada ya Azam
kujitoa kushiriki mashindano mapya ya kagame, tuliwapa Mbeya City nafasi”.
Hata hivyo, Mbeya City
fc wanaonekana kuisubiria kwa hamu nafasi hiyo na jana kocha mkuu wa Mbeya City
Juma Mwambusi alisema bado hawana uhakika wa kushiriki kutokana na kushika
nafasi ya tatu 2013/2014, lakini wanatamani kuona haki inatendeka.
Wadau wa soka wanasema
tayari TFF wameshatuma jina la Simba, labda kwasasa wanawatupia mzigo Cecafa
ili waonekane ndio wamewachagua Simba.
Hii inatokana na
ukweli kwamba wapenda soka walichukizwa na kitendo cha TFF kuwatosa Mbeya City
fc wenye sifa na kuwapa nafasi Simba wasiokuwa na vigezo na sababu kubwa
ikionekana ni maslahi kuliko kuendeleza soka.
Mgahawa wauza nyama ya binaadamu Nigeria
Mgahawa mmoja nchini Nigeria katika jimbo la Anambra umefungwa
kufuatia viongozi wenye mamlaka nchini humo kung’amua kwamba moja ya vyakula
vinavyouzwa mgahawani humo ni nyama ya binaadamu.
Polisi walipoitwa
mgahawani hapo waliona vichwa viwili vya binaadamu vipya vyenye kuchuruza damu
wakati walipokuwa wakiwakamata watu kumi na mmoja kutoka mgahawani hapo akiwemo
mmiliki wa mgahawa huo,pia walikamatwa wanawake sita na wanaume wane, baada ya
wasamaria wema kutoa taarifa hizo za kustaajabisha!
Damu
zilizokuwa zikivuja kwenye vichwa hivyo vya wanaadamu,vilikuwa vimefungwa
kwenye mifuko ya Rambo.
Polisi
pia wamekamata bunduki aina ya AK-47 na silaha nyinginezo,seti ya magurunedi na
simu kadhaa za kila aina wakati walipokuwa wakiwakamata watu hao.
Kila
wakati nilipokuwa nikienda sokoni,na sababu kubwa hasa hoteli hiyo iko karibu
na sokoni,nimekuwa nikishuhudia harakati za ajabu za watu kuingia na kutoka
hotelini humo,watu wachafu na uchafu wao mwilini ni ule usioeleweka,hivyo
sikushangazwa polisi walipogundua biashara hiyo haramu mapema wiki hii, anasema
mkaazi wa eneo hilo.
Mchungaji
mmoja akiwa katika mshtuko mkubwa baada ya kugundua kuwa alikuwa amekula nyama
ya binaadamu,aliamua kwenda polisi kupeleka malalamiko yake .
Aliwaambia
kuwa alikwenda kwenye mgahawa wa hoteli hiyo asubuhi na mapema,baada ya kupata
staftahi,akaambiwa kwamba pande la nyama alilokula gharama yake ni naira 700
sawa na paundi mbili unusu alistaajabu mno.sikufahamu kuwa nimeuziwa nyama ya
binaadamu nikaila na kwamba ilikuwa ghali sana.
Taarifa
za watu nchini Nigeria kula nyama za watu zimekuwa ni uvumi wa muda mreefu,
lakini hii ni mara ya kwanza mgahawa kuamua kuuza nyama za binaadamu tu.
Kwa hisani ya BBC-Swahili
Wanajeshi washika doria Bujumbura
Jeshi nchini Burundi linapiga doria
kwenye mitaa ya mji mkuu Bujumbura ambapo waandamanaji wameahidi kufanya
maandamano ya kupinga uamuzi wa rais wa kuwania muhula wa tatu.
Wanajeshi
wana matumaini ya kuwakamata wanajeshi waasi ambao waliongoza mapinduzi ya wiki
hii katika jaribio la kumpindua rais Pierre Nkurunziza.
Nkurunziza
ametaka kusitishwa kwa maandamano hayo na kuyahusisha na jaribio hilo la
mapinduzi.
Lakini
baadhi ya makundi ya waandamanaji yamekana madai hayo na kumtaka tena rais
kuiheshimu katiba.
Marekani
nayo inasema kuwa Nkurunziza hastahili kuwania muhula mwingine ikiongeza kuwa
serikali yake itawajibika kwa chochote kile kitakachotokea.
Kwa hisani ya BBC-Swahili
Wednesday, May 13, 2015
Taifa Stars yaelekea Afrika ya Kusini
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kesho Jumatano inatarajiwa kusafiri kuelekea nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kushiriki michuano ya kombe la COSAFA.
Taifa Stars itaondoka jijini Dar es salaam kesho majira ya saa 1 jioni, kwa usafiri wa shirika la ndege la Fasjet na kufika jijini Johanesburg saa 5 usiku.
Msafara wa Taifa Stars utaongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa TFF, Ephaphra Swai ukijumuisha wachezaji 20 na benchi la ufundi, timu inatarajiwa kufikia katika hoteli ya Sun City iliyopo pembeni kidogo ya jiji la Rusterburg.
Barcelona yatinga fainali
Barcelona imetinga fainali ya michuno ya ligi ya Mabingwa, baada ya kumenyana Jumanne usiku wiki hii na Bayern Munich. Bayern Munich imeaga michuano hiyo, baada ya kuifunga Barcelona mabao 3-2 katika mchezo wa marudiano wa michuano ya nusu fainali ya Kombe la Mabingwa barani Ulaya.
Katika mchezo wa awali uliyochezwa wiki moja iliyopita, Barcelona iliifunga Bayern Munich mabao 3-0.
Barcelona inasubiri kucheza fainali Juni 6 mwaka 2015 na moja ya klabu itakayoshinda leo Jumatano usiku kati ya Real Madrid na Juventus.
Bayern Munich ndio iliyoanza kuona lango la Barcelona katika mchezo wa marudiano wa michuano ya fainali ya Kombe la Mabingwa barani Ulaya. Bao la kwanza la Bayern limefungwa na mchezaji kutoka Morocco Mehdi Benatia katika dakika ya 7 ya mchezo.
Katika dakiaka ya 15 Barcelona kupitia mchezaji wake Neymar ikasawazisha baada ya pasi aliyopewa na Luis Suarez kutoka kwa Muargentina Lionel Messi.
Barcelona iliendelea kushambulia lango la Bayern Munich na kufaulu katika dakika ya 29 kufunga bao la pili kupitia mchezaji wake Neymar, na kuongoza mabao 2-1 dhidi ya Bayern Munich.
Hadi wakati huo, Bayern Munich ilikua inataraji ifunge mabao 6-2 ili iweze kutinga fainali ya michuano ya ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Lakini hali hiyo haikutokea.
Hata hivyo Bayern ilikuja juu na kufaulu kusawazishabao la pili kupitia Robert Lewandowski katika dakiaka ya 40. .
Katika dakika ya 74, Bayern Munich kupitia mchezaji wake Thomas Müller ilifunga bao la tatu. Hadi kipenga cha mwisho Bayern Munich iliongoza kwa mabao 3-2 dhidi ya Barcelona. Licha ya Bayern kuibuka mshidi katika mchuano huo, ililazimika kuaga michuano hiyo, baada ya kupoteza katika mechi ya awali ya nusu fainali wiki moja iliyopita, ambapo ilifungwa mabao 3-0.
Barcelona, wamefanikiwa kutinga fainali baada ya kuibwaga Bayern Munich kwa jumla ya mabao 5-3 yaliyopatikana katika mikondo yote miwili waliyokutana kwenye hatua ya nusu fainali.
Jumatatu usiku wiki hii kutakuwa na mchuano kati ya Real Madrid dhidi ya Juventus kwenye uwanja wa Benabeu.
Barcelona inasubiri kucheza fainali Juni 6 mwaka 2015 na moja ya klabu itakayoshinda leo Jumatano usiku kati ya Real Madrid na Juventus.
Bayern Munich ndio iliyoanza kuona lango la Barcelona katika mchezo wa marudiano wa michuano ya fainali ya Kombe la Mabingwa barani Ulaya. Bao la kwanza la Bayern limefungwa na mchezaji kutoka Morocco Mehdi Benatia katika dakika ya 7 ya mchezo.
Katika dakiaka ya 15 Barcelona kupitia mchezaji wake Neymar ikasawazisha baada ya pasi aliyopewa na Luis Suarez kutoka kwa Muargentina Lionel Messi.
Barcelona iliendelea kushambulia lango la Bayern Munich na kufaulu katika dakika ya 29 kufunga bao la pili kupitia mchezaji wake Neymar, na kuongoza mabao 2-1 dhidi ya Bayern Munich.
Hadi wakati huo, Bayern Munich ilikua inataraji ifunge mabao 6-2 ili iweze kutinga fainali ya michuano ya ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Lakini hali hiyo haikutokea.
Hata hivyo Bayern ilikuja juu na kufaulu kusawazishabao la pili kupitia Robert Lewandowski katika dakiaka ya 40. .
Katika dakika ya 74, Bayern Munich kupitia mchezaji wake Thomas Müller ilifunga bao la tatu. Hadi kipenga cha mwisho Bayern Munich iliongoza kwa mabao 3-2 dhidi ya Barcelona. Licha ya Bayern kuibuka mshidi katika mchuano huo, ililazimika kuaga michuano hiyo, baada ya kupoteza katika mechi ya awali ya nusu fainali wiki moja iliyopita, ambapo ilifungwa mabao 3-0.
Barcelona, wamefanikiwa kutinga fainali baada ya kuibwaga Bayern Munich kwa jumla ya mabao 5-3 yaliyopatikana katika mikondo yote miwili waliyokutana kwenye hatua ya nusu fainali.
Jumatatu usiku wiki hii kutakuwa na mchuano kati ya Real Madrid dhidi ya Juventus kwenye uwanja wa Benabeu.
Shughuli za uokozi zakwama upya Nepal
Wafanyikazi wa
mashirika ya kutoa misaada wamesema kuwa tetemeko la hapo jana nchini Nepal
limeathiri kwa kiasi kikubwa.juhudi za kutoa misaada kwa waathiriwa wa
tetemeko la awali lililosababisha vifo vya zaidi ya watu 8000 takriban majuma
mawili yaliyopita.
Hadi kufikia sasa inakisiwa kuwa takriban watu 65 wamepoteza maisha yao nchini Nepal huko maafa zaidi yakitarajiwa nchini India na Tibet ,China.
Shughuli za uokozi zimerejelewa Nepal, ambayo kwa mara ya pili ndani ya wiki tatu imekumbwa na tetemeko kubwa la ardhi.
Lakini bado kuna watu waliozikwa kwenye vifusi.
Maafisa wa huko wanasema kuwa wanatarajia idadi hiyo kuongezeka.
Kufikia sasa takriban watu 1,000 wamejeruhiwa na tetemeko hilo lipya.
Waathiriwa wengi wameripotiwa kufunikwa na vifusi karibu na kitovu cha tetemeko hilo katika mji wa Chautara
Watu wengi wamelala nje wakihofia kuwa wanaweza kuathirika zaidi wakiwa ndani ya nyumba zao.
Wakati huo huo helikopta ya kikosi cha majini cha Marekani,ambayo ilikuwa ikifanya kazi ya kusaidia kusambaza huduma za kibinaadamu nchini Nepal, haijulikani iliko.
Taarifa za awali zinaeleza kuwa, ndani ya helikopta hiyo kulikuwa na watu wanane,miongoni mwao, sita ni askari wa kikosi cha majini cha Marekani na askari wawili wa jeshi la Nepal.
Maofisa wa serikali wa Marekani wamesema kwamba helikopta hiyo ilikuwa maeneo ya jirani na kijiji cha Charikot, ambacho kiliharibiwa vibaya na tetemeko la ardhi.
Kwa hisani ya bbcswahili.com
Tuesday, May 12, 2015
BAADHI YA MADHARA YA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA JIJINI DAR
Thursday, May 7, 2015
ATHARI ZA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA JIJINI DAR
Subscribe to:
Posts (Atom)