Haya yalisemwa na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya Taifa Ndg.Damiani Lubuva kijijini Msoga kata ya Msoga wilayani Bagamoyo mbele ya Mh.Raisi Dk.Jakaya Kikwete mara baada ya kujiandikisha.
Bw.Lubuva alisema kuwa lengo la Tume ni kuandikisha Watanzania Milioni 21 hadi23 kote nchinimara zoezi hilo litakapofikia tamati kati ya mwezi Julai na Agosti mwanzoni kama hakutatokea matatizo
Anasema changamoto zilizojitokeza ni za kawaida hasa kutokana na mfumo huo kuwa ni mpya hivyo lazima kuwe na changamoto kama ilivyo kwenye jambo lolote jipya lazima liwe na changamoto zake
Mkoa wa Pwani unajumla ya vituo 1,752 vya kujiandikisha na mashine 932 ambapo kata ya Msoga kuna jumla ya vituo 17.Zoezi hilo lilianza jana na litamalizika Julai 20.
Ni fursa kwa wakazi wa Mkoa wa Pwani kujiandikisha katika daftari lakudumu la kupiga kura na kupata nafasi ya kuchagua viongozi wanaowataka katika uchaguzi.
![]() |
Raisi Akijiandikisha kwenye Mfumo Mpya wa Kielekroniki wa BVR |
![]() |
Raisi akichukuliwa Alama ya Vidole na Afisa Tehama wa Tume |
![]() |
Raisi akipokea kitambulisho chake cha kupiga Kura kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume Bw.Lubuva Picha kwa hisani ya Michuzi Blog |
No comments:
Post a Comment