Tuesday, November 8, 2016

BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 07.11.2016

Watu 17 wamefariki dunia katika ajali iliyohusisha lori la mizigo aina ya Scania lenye namba za usajili T198CBQ  na Noah ya abiria yenye namba za usajili T232BQR iliyotokea jana usiku katika kijiji cha Nsalala mkoani Shinyanga


kwa hisani ya ITV

Thursday, November 3, 2016

Dakika 12 za Hussein Bashe bungeni kuhusu wizara ya fedha

BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO 02.11.2016

Kenya yatangaza kuondoa wanajeshi Sudan Kusini

Kenya imetangaza kuwa inawaondoa wanajeshi wake kutoka kikosi maalumu cha Umoja wa Mataifa cha kudumisha amani kilichoko Sudan Kusini, baada ya kamanda wake kutimuliwa kazini.
Wizara ya Mashauri ya Kigeni imesema kuwa utaratibu wa kumuachisha kazi Jemedari Johnson Mogoa Kimani Ondieki haukuwa na uwazi.

Katibu Mkuu wa UN Ban Ki-moon alimfuta kazi Luteni Kanali Johnson Ondieki baada ya ripoti ya uchunguzi kusema alikosa kuwajibika kulinda raia mapigano yalipozuka upya nchini Sudan Kusini mwezi Julai.
Ripoti hiyo imesema walinda amani waliokuwa chini ya jemedari huyo hawakuchukua hatua yoyote wanajeshi wa serikali waliposhambulia kituo cha utoaji misaada mjini Juba na kuwadhulumu raia.
Kenya imesema uamuzi huo si wa haki na kutangaza kwamba itayaondoa mara moja majeshi yake yanayohudumu chini ya UN nchini Sudan.
Kadhalika, Kenya imejiondoa kutoka kwa mpango wa kutuma wanajeshi wa ziada kutoka nchi za kanda ambao walitarajiwa kutumwa kuimarisha kikosi cha UN nchini humo.
Kwenye taarifa yake, Kenya imesema kwa kumfuta Jenerali Gen Ondieki, Bw Ban alikosa kuangazia kiini cha matatizo yaliyobainika kwenye ripoti hiyo ya uchunguzi.

Habari kwa hisani ya bbcswahili.com


SEMINAR


MATOKEO LIGI YA VPL JANA NA MSIMAMO WA LIGI



Wednesday, October 19, 2016

Huduma Ya Afya Call

Sauti Sol wameitaja video iliyowapa changamoto wakati wa maandalizi...

KUTOKA KWA MDAU WETU GUNDA FOUNDATION


vv
Mwaka 2016 Shirika la Twaweza Afrika Mashariki lilizindua utafiti wake (http://twaweza.org/go/uwezo-tz-2014) uliofanyika mwaka 2015 ukionesha ongezeko kubwa la watoto kushindwa kusoma ilhali wapo madarasa ya juu mfano darasa la nne nakuendelea.
Tafiti hizi sio za kusoma na kuangalia hivi hivi. Kila mmoja wetu anayo nafasi ya kusaidia anguko hili ambalo linazidi kumomonyoa na kuifanya Elimu kwa watoto wetu kuwa duni na yakukatisha tamaa.
Kama Marafiki wa Elimu kupitia Gunda Foundation Tanzania, tumekua tukifanya Harakati mbalimbali za kuwasaidia watoto kupenda kujifunza na kujisomea vitabu ili kukuza maarifa na kuboresha maendeleo ya ufahamu walionao.
Mwaka 2014 Gunda Foundation ilifanya Jitihada za mwanzo katika kuwasaidia watoto wa kata ya Msambara, Wilaya ya Kasulu mkoani kigoma kuweza kusoma.
Katika mradi huo ulijumuisha shule 7 za kata hio na jumla ya watoto 197 wa shule tano za kata hio waliingia katika utaratibu huu wakati wa likizo ya mwezi wa 12, 2014.
Watoto hawa walikua katika hatua tofauti tofauti za usomaji. Mbinu mbalimbali zilitumika ili kutambua uwezo halisi wa mtoto katika kusoma.
Utaratibu wa kuwatambua na kuwatenga watoto hawa ulikua kama ifuatavyo;
  1. Viliandikwa vikaratasi vikiwa na neno moja mpaka maneno mawili, kisha kutupwa katika eneo la shule vikiwa vya idadi ya kutosha;
  2. Wanafunzi wakiwa darasani waliruhusiwa kutoka darasani na kila mmoja alitakiwa aokote karatasi lolote atakalo liona katika mazingira ya shule yake na akisha okota basi akimbie mpaka katika uwanja wa shule na kusimama umbali wa mita 20 mbali na mwenzake;
  3. dsc02318
  4. Bila watoto kusomeana vikaratasi hivyo kutokana na umbali waliosimama mmoja hadi mwingine, Mwalimu alianza kuita mwanafunzi mmoja baada ya mwingine na akifika mwalimu humuomba mwanafunzi amsomee neno lililoandikwa katika karatasi aliyoiokota.
  5. Kwa njia hii makundi kadhaa yalitenganishwa kulingana na uwezo wa mtoto kusoma neno hilo kwa vigezo vya bila kusita;
  6. Watoto walioonesha udhaifu mkubwa waliingizwa darasani na kuandikiwa silabi “a” mpaka “z” ubaoni na walitakiwa wasome silabi zote mmoja baada ya mwingine ili mwalimu ajiridhishe zaidi katika uwezo wa mwanafunzi kusoma;dsc02326
  7. Hii ilifanyika ili kusaidia kumpa mtoto mkakati maalumu utakaomsaidia kusoma vizuri.
  8. Baada ya kuapata makundi ya uwezo tofauti wa usomaji mwalimu alianza mafunzo ya kuwaelekeza watoto kujifunza kusoma na programu hii ni ya mwezi mmoja na hufanyika katika kipindi cha likizo ya mihula ya wanafunzi.
  9. Kumbuka: Ukihitaji kuona video ya vitendo hivi au matokeo wasiliana nasi kwa namba 0674 14 12 09 au Baruapepe: gmpollo@gmail.comau fika Chuo cha Ualimu Korogwe onana na Mwalimu Gunda.
    Kuanzia mwaka huu 2016, Mwezi Octoba Marafiki wa Elimu kwa ushirikiano na Gunda Foundation wanatarajia kuifanya programu hii katika mkoa wa Tanga hususani katika Wilaya za Handeni Vijijini na Korogwe.
    Kwa Korogwe pia itahusisha Darasa la watu wazima na wale waliokosa nafasi ya kujiunga na darasa la kwanza wakiwa na umri mkubwa ili kuwapa fursa ya kujua kusoma na kuandika.
    Hivyo ukiwa kama mdau wa Elimu unaomba kama una mtoto, ndugu au jamaa asiejua kusoma na kuandika basi wasiliana nasi ili aweze kusaidiwa na HAKUNA MALIPO YOYOTE ATAKAYOCHANGIA KATIKA UJIFUNZAJI WAKE!
    9
    Sote tunawajibu kuwasaidia Watoto Wajifunze

Tuesday, July 12, 2016

Mkapa aunguruma UDSM, akiri kukosea sera ya ubinafsishaji, agusia katiba mpya

Mtoto apandikizwa pua mpya India



Madaktari nchini India wamepandikiza pua mpya katika uso wa mvulana wa miaka 12 iliokuwa imemea katika paa lake la uso.
Pua ya Arun Patel iliharibika alipougua ugonjwa wa homa ya kichomi
Maambukizi hayo yaliharibu pua yake akiwa mtoto mdogo.
Upandikizaji kama huo ulifanywa nchini China mwaka 2013 ambapo mtu mmoja ambaye aliharibu pua yake katika ajali alipewa pua mpya.
Wazazi wa Arun walimchukua na kumpeleka katika daktari mwengine katika kijiji cha jimbo la kati la Madhya Pradesh ambapo aliugua kichomi mda mfupi baada ya kuzaliwa.

Lakini matibabu aliyopewa yaliongeza hali yake na hivyobasi kupoteza pua yake.

Miaka kadhaa baadaye,kundi moja la madaktari katika mji wa Indore liliamua kufanya upasuaji usiokuwa wa kawaida ambapo Arun alipata pua mpya.

 kwa hisani ya BBCSwahili

Mabaki ya Wafilisti yapatikana Israel

Watafiti wa mambo ya kale nchini Israel wamegundua makaburi ya kwanza ya Wafilisti.
Makaburi hayo, yaliyopatikana eneo la Ashkelon, yaligunduliwa mwaka 2013, lakini habari hizo zilifichuliwa Jumapili.
Habari hizi ziliwekwa siri muda huo wote kuzuia kushambuliwa na waandamanaji wa makundi ya Wayahudi wahafidhina ambao hawakutaka makaburi hayo yafukuliwe.

 Taarifa zinasema ugunduzi huo huenda ukafichua mengi kuhusu asili ya Wafilisti ambao wamezungumziwa sana katika vitabu vya kidini.


Mafanikio hayo yalitokea mwisho wa mwaka wa 30 wa uchimbaji ulioongozwa na kundi la Leon Levy Expedition.
Viongozi wa uchimbaji huo wanasema walipata makaburi yaliyozingirwa na manukato, vyakula, mapambo, vito na silaha.
Yanadaiwa kujengwa na kutumiwa kati ya karne ya 11 na karne ya 8 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu.


"Baada ya kutafiti kuhusu Wafilisti kwa miongo mingi, hatimaye tunaweza kuwatazama,” anasema mmoja wa wanaakioloiia hao Daniel M Master.
“Kwa ugunduzi huu, tunakaribia kubaini siri za asili yao.”
Profesa Lawrence E. Stager ni mmoja wa wanaoongoza utafiti huo

Wanaakiolojia hao sasa wanafanya uchunguzi wa DNA pamoja na uchunguzi wa miale ya ukaa kubaini watu hao waliishi wakati gani.
Watafiti hutofautiana kuhusu asili ya Wafilisti, baadhi wakiamini walitoka Ugiriki, wengine visiwa vya Crete au Cyprus na wengine eneo la Anatolia nchini Uturuki.


Wafilisti huoneshwa katika Biblia kama maadui wakuu wa Waisraeli, na inadhaniwa walihamia Israel kutoka maeneo ya Magharibi karne ya 12 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu.
Anayefahamika zaidi ni Goliath, mpiganaji ‘jitu’ ambaye kwa mujibu wa Biblia, aliuawa na Daudi kabla yake kuwa Mfalme wa Waisraeli.
Katika Biblia, wanaoneshwa kama watu wakatili lakini mabaki yaliyopatikana yanaonekana kuashiria kwamba walikuwa na ustaarabu fulani.


Habari kwa hisani ya BBCSwahili

Saturday, July 2, 2016

KUTOKA TRA


AZAM MARINE WAJA NA SEA TAX

Kampuni ya usafirishaji majini ya Azaam Marine imekuja na huduma mpya ya usafirishaji wa majini jijini Dar es salaam.




UJENZI WA DARAJA LA KONGOWE - KIGAMBONI WAENDELEA

Daraja linalounganisha maeneo ya Mbagala Kongowe na Kigamboni lililopo eneo la Mbagala Kongowe ambalo lilikuwa shida kupitika wakati wa mvua kubwa sasa linajeungwa upya.Daraja hili ni kiungo kikukwa sana kwa wakazi waishio maeno ya Toangoma,Kibada na Kigamboni Kutokea Mbagala Kongowe.








Friday, July 1, 2016

KUTOKA BUNGENI



Kutoka Bungeni jijini Dodoma ,Wabunge wa kambi rasmi ya Upinzani jana asubuhi waliingia Bungeni wakiwa wote wamevalia nguo nyeusi walipohudhuria kikao cha Bunge la Bajeti.Baada ya Naibu Spika Dk Tulia Ackson kuingia Bungeni na kuongoza dua ya kuliombea Bunge walianza kunyanyua mabango mbalimbali na kutoka nje

TAARIFA KWA WATUMIAJI WA HUDUMA ZA KIBENKI



RATIBA YA LADY JAYDEE IDD PILI


Wednesday, April 20, 2016

RAIS MH.JOHN MAGUFULI AZINDUA DARAJA LA KIGAMBONI KATIKA PICHA

Raisi Mh John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi na wageni waliofika kushuhudia uzinduzi huo wa kihistoria wa daraja la kigamboni ambalo Mh Rais alishauri liitwe daraja la Nyerere

Mh Raisi akikata utepe kuashiria ufunguzi wa daraja hilo




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiteta jambo na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dkt Ramadhani Dau wakati wa  uzinduzi rasmi wa Daraja la Kigamboni katika wilaya mpya ya Kigamboni jijini Dar es salaam Aprili 19, 2016



Muonekano wa Daraja la Kigamboni


 Picha zote kwa hisani ya blog.ikulu.go.tz/