Monday, April 15, 2013

Waasi wa M23 waionya Tanzania

Wanajeshi wa M23
Waasi wa kundi la M23 wameitaka Tanzania kuachana na mipango ya kuchangia wanajeshi wake katika kikosi cha Umoja wa Mataifa kinachopangwa kutumwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kupambana na waasi .
Waasi wa kundi hilo la M23 ambao wamekanusha madai ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa kwamba nchi jirani za Rwanda na Uganda zinawaunga mkono,wameonya katika baruwa iliyotumwa na kiongozi wa kisiasa wa kundi hilo Betrand Bisimwa kwa Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania kwamba daima wamekuwa wakipata ushindi dhidi ya vikosi vikubwa vyenye silaha nzuri.
Bisimwa ameandika " Jambo kama hilo litawakuta kikosi hicho cha Umoja wa Mataifa cha kuingilia kati iwapo busara yao itashindwa kufanya kazi kuingilia kati na kuzuwiya hali ya hatari ilioko kwenye mkondo huo."
Bisimwa amesema kwa ajili hiyo kundi hilo la waasi la M23 linaomba bunge na wananchi wa Tanzania kufikiria upya kwa uangalifu juu ya hali hiyo na kuishawishi serikali ya Tanzania kutowapeleka watoto wao wa kiume na wa kike wa taifa hilo la uadilifu kushiriki kwenye vita vya kipuuzi dhidi ya ndugu zao wa Congo.

No comments:

Post a Comment