Wednesday, April 17, 2013

BI KIDUDE HATUNAYE TENA

TASNIA ya Sanaa ya Muziki nchini Tanzania imepata pigo jingine baaada ya Gwiji la muziki wa mwambao wa pwani Fatuma Binti Baraka "Bi Kidude" kufariki dunia muda mfupi uliopita.
Taarifa za kifo cha mwanamuziki huyo zimetufikia  hivi punde toka kwa familia yake zinasema Bi Kidude aliekuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Hindu Mandal amefariki leo.
Bi Kidude atakumbukwa kama mwanamuziki mkongwe zaidi nchini ambaye alianza muziki akiwa na umri wa miaka 10 tu na aliwahi kupokea tuzo mbalimbali kutokana na mchango wake katika muziki wa mahadhi ya mwambao. Hakika sanaa nchini imepoteza moja ya nguzo kubwa.

hii ni baadhi ya nyimbo zake alizowahi kuimba enzi za uhai wake

No comments:

Post a Comment