Kwa bahati mbaya ni kwamba kadri siku
zinavyokwenda mbele, vitendo vya watu kutekwa vinaonekana kuongezeka,
huku hofu kuu ikiwa ni nini kinachosababisha hayo au akina nani hasa
walioko nyuma ya vitendo hivyo vinavyoonekana kutishia maisha watu.
Watanzania waliowahi kutekwa
Baadhi ya watu ambao wameuawa katika mazingira
yenye utata ama yanayofanana nay a utekaji ni mwanasheria maarufu
nchini, Profesa Jwani Mwaikusa. Msomi huyu ambaye alikuwa Mhadhiri wa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kitivo cha sheria, aliuawa kwa kupigwa
risasi akiwa nje ya nyumba yake, huku wauaji wakiondoka bila kupora
chochote zaidi ya mkoba na makaratasi aliyokuwa nayo.
Profesa anakumbwa kwa mengi, mojawapo ni kwamba
alikuwa mmoja wa mawakili walikuwa wakiwatetea washtakiwa wa mauaji ya
kimbali Rwanda. Alikuwa akimtetea mfanyabiashara maarufu nchini Rwanda,
Yussuf Munyakazi aliyekuwa akihusishwa na mauaji hayo katika kesi
iliyokuwa ikiendelea katika Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari
ya Rwanda (ICTR), jijini Arusha.
Aliyekuwa akimtetea afungwa
Hata hivyo ICTR ilimtia hatiani Munyakazi kwa kumfunga miaka 25 kwa maelezo kuwa alihusika kwa namna moja ama nyingine kuendesha mauaji ya kimbari na kuteketeza familia huko Rwanda.
Munyakazi katika mashtaka yake alitakiwa na Serikali ya Rwanda akashtakiwe nchini kwao, lakini alikataa kwa kuhofia kutotendewa haki.Ni jitihada za Profesa Mwaikusa, zilizosababisha kesi yake iendeshwe ICTR Arusha hadi ilipotolewa hukumu.
Hata hivyo ICTR ilimtia hatiani Munyakazi kwa kumfunga miaka 25 kwa maelezo kuwa alihusika kwa namna moja ama nyingine kuendesha mauaji ya kimbari na kuteketeza familia huko Rwanda.
Munyakazi katika mashtaka yake alitakiwa na Serikali ya Rwanda akashtakiwe nchini kwao, lakini alikataa kwa kuhofia kutotendewa haki.Ni jitihada za Profesa Mwaikusa, zilizosababisha kesi yake iendeshwe ICTR Arusha hadi ilipotolewa hukumu.
Wakati hukumu inatolewa, Profesa Mwaikusa
alishauawa na watu wasiojulikana, jijini Dar es Salaam, kitendo ambacho
kinaonekana kumuumiza Munyakazi, kutokana na ukweli kuwa msomi huyo
alikuwa ana uwezo mkubwa katika masuala ya sheria, kiasi cha kufanikisha
asipelekwe Rwanda, kama Serikali ya nchi hiyo ilivyotaka.
Mhadhiri huyo mahiri aliuawa nyumbani kwake barabara ya Makonde eneo la Salasala, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Wakati Mwaikusa akijiandaa kushuka katika gari
lake, watu hao walimgongea kioo na kumwamuru kushuka, inaelezwa kuwa
Profesa Mwaikusa alisita, ndipo walimpommiminia risasi hadi kufa.
Wakati wamemaliza kumpiga risasi, alitokea mpwae
Profesa Mwaikusa, Gwamaka Daudi (25), kwa lengo la kumnusuru, kwa bahati
mbaya naye aliuawa kwa kupigwa risasi mgongoni.
Baada ya kuwaua ndugu wawili, watu hao walianza
kutoweka, kwa mbele wakaona kikundi cha watu ambalo walilitilia shaka
kwamba wanataka kupambana nao, ndipo walipompiga risasi mtu mwingine
aliyejulikana kwa jina la John Mtui (45).
Kama hiyo haitoshi matukio mengine zaidi ya watu kutekwa na hata kuuawa yanaonekana kuendelea.
Source:Mwananchi
Source:Mwananchi
No comments:
Post a Comment