Monday, May 20, 2013

Assad asisitiza hatajiuzulu

Rais wa Syria Bashir al Assad
 

Rais wa Syria Bashar al Assad amesisitiza kuwa hatajiuzulu kabla ya mwisho wa kipindi chake madaraka mwaka 2014, wakati bomu lililotegwa katika gari liua watu watatu katika mji mkuu Damascus.
"Kujiuzulu ni sawa na kukimbia", Assad amesema katika mahojiano na gazeti moja la Argentina la Clarin wakati alipoulizwa iwapo anaweza kufikiria kujiuzulu kama waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry anavyotaka.
"Sifahamu iwapo Kerry ama yeyote mwingine amepata madaraka ya watu wa Syria kuzungumzia kwa niaba yao juu ya nani anapaswa kuondoka madarakani na nani anapaswa kubaki. Suala hilo litaamuliwa na watu wa Syria katika uchaguzi wa rais mwaka 2014.

No comments:

Post a Comment