Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry anatarajiwa kusafiri kwenda katika mataifa ya mashariki ya kati na Afrika kuanzia Jumanne ijayo kwa ziara itakayomchukua hadi Mei 27.
Kerry anatarajiwa kuanza ziara yake mjini Muscat siku ya Jumanne (21.05.2013), ikifuatiwa na Jordan siku ya Jumatano, ambako atakutana na kile kinachoitwa "washirika muhimu wa kimataifa", kuangalia uwezekano wa kupatikana kwa suluhisho la kisiasa kupitia majadiliano nchini Syria , wizara ya mambo ya kigeni nchini Marekani imesema katika taarifa.
Mkutano huo unakuja kabla ya mkutano mkubwa wa kimataifa kuhusu Syria unaopangwa na Urusi na Marekani , na ambao unatarajiwa kufanyika mwezi ujao.
Kerry akiwa katika majadiliano na rais Putin wa Urusi
Siku ya Alhamis na Ijumaa , Kerry anatarajiwa kuzuru Jerusalem na
Ramallah kufuatilia mazungumzo juu ya kuleta pamoja Israel na
Palestina katika meza ya majadiliano, kujadili amani, taarifa hiyo
imesema.Pia siku ya Ijumaa , Kerry anatarajiwa kusafiri kwenda mjini Addis Ababa kushiriki katika sherehe za siku mbili za kuadhimisha miaka 50 tangu kuundwa kwa Umoja wa nchi za Afrika OAU, ambao hivi sasa unajulikana kama Umoja wa Afrika, AU. viongozi kutoka sehemu mbali mbali za Afrika watahudhuria sherehe hizo.
Hapo Mei 26 , waziri Kerry anapanga kurejea mjini Amman Jordan kushiriki katika jukwaa la kiuchumi la dunia.
Wakati huo huo baraza la usalama la umoja wa mataifa linatafakari ombi kutoka kwa maafisa wa ngazi ya juu wa shirika la misaada la umoja huo linalodai kufikishwa kwa misaada katika nchi iliyoharibiwa kwa vita ya syria, hatua ambayo inaweza kusababisha hali ya mivutano baina ya Urusi na mataifa ya magharibi kuhusiana na upelekaji wa misaada ya kiutu kupitia mipakani, wamesema wanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa.
No comments:
Post a Comment