Dar es Salaam. Kiungo wa Yanga, Athuman Idd ‘Chuji’ ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mechi ya kituo cha SuperSport katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya Simba iliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Chuji alionyesha kiwango cha juu katika mchezo huo
ulioshuhudiwa na mashabiki 57,406 kwa kuiunganisha vyema safu ya kiungo
ya Yanga.
Baada ya mechi hiyo kituo cha SuperSport
kilichoonyesha mechi hiyo moja kwa moja kilimtangaza Chuji kuwa mchezaji
bora wa mechi hiyo na kuwafunika Didier Kavumbagu na Hamisi Kiiza
wafungaji wa mabao ya Yanga.
Chuji alisema tuzo hiyo ameipokea kama changamoto
kubwa kwake katika kuhakikisha anaendelea kucheza kwa kiwango cha juu
siku zote.
“Nimefurahi kusikia hivyo sababu SuperSport ni
watu wa mpira na watakuwa wameona uwezo wangu katika mechi hii, lakini
hali hiyo naichukua kama moja ya changamoto kwangu,” alisema Chuji.
Yaliyostaajabisha kipute cha watani wa jadi kama kawaida ya mtanange wa
watani wa jadi yaani Simba na Yanga huwa haukosi matukio mageni ambayo
huacha simulizi kwa mashabiki.
Haya ni baadhi tu matukio yaliyojiri kwenye mchezo huo uliopigwa mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mwamuzi aanguka, mpira wasimama
Mashabiki wa soka walipigwa na “bumbuwazi” baada
ya mwamuzi Martin Saanya aliyekuwa anachezesha mpambano huu wa Simba na
Yanga kulala chini ghafla.
Tukio hili ambalo ni nadra kutokea kwenye viwanja
vya soka lilisababisha mpira kusimama kwa muda mrefu, ingawa ilikuja
kubainika kwamba alipigwa kiwiko wakati akisuluhisha ugomvi baina na
beki Said Nasoro ‘Cholo’ wa Simba na mshambuliaji wa Yanga, Didier
Kavumbagu.
No comments:
Post a Comment