Monday, May 20, 2013

Mchungaji Peter Msigwa wa CHADEMA akamatwa na Jeshi la Polisi.

Taaarifa kutoka Iringa zinasema mbunge wa Jimbo la Iringa Peter Msigwa wa CHADEMA amekamatwa na jeshi la polisi muda huu na yuko chini ya Ulinzi wa jeshi hilo.
Mchungaji Msigwa amekamatwa kwa amri ya Kamanda wa Polisi wa mkoa huo Michael Kamuhanda kwa madai kwamba anawaunga mkono wafanyabiashara ndogondogo wa manispaa hiyo Machinga wanaopambana na polisi wanaowakataza kufanya biashara mjini.

Mchungaji Msigwa amekuwa mtetezi mkubwa wa wafanyabiashara ndogondogo kiasi kwamba kila anapoonekana maeneo ya manispaa hiyo hujikuta gari yake ikisukumwa na Machinga hao.

Itakumbukwa ni wiki iliyopita tu mbunge wa viti maalum Chadema Chiku Abwao alimshambulia vikali Waziri William Lukuvi kwamba analitumia jeshi la polisi Iringa kukandamiza Chadema na viongozi wake.

Mchungaji Msigwa ambaye pia ni mbunge machachari wiki iliyopita ametishiwa na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kufikishwa mahakamani kwamba amemtuhumu kufanya biashara haramu ya pembe za ndovu.

Gari la Mbunge Mch.Msigwa kabla ya kukamatwa

Polisi wakitoka kumkamata Mch.Msigwa

No comments:

Post a Comment