Tuesday, April 15, 2014
Monday, April 14, 2014
Madaktari wakuza 'uke' katika maabara
Madaktari nchini
Marekani wamefanikiwa kuwatengezea wanawake wanne sehemu ya uke kwa njia ya
kisayansi.
Walitumia mfano wa
seli ya uke na mifupa ya mwili kuweza kukuza uke huo katika maabara kwa
kuzingatia wastani na umbo la kila mwanamke.
Baada ya matibabu
hayo, wanawake hao wote inaarifiwa walielezea kupata hisia sawa na
kamilifu,matamanio, kuridhishwa wakati wa tendo la ndoa pamoja na kutopata
maumivu yoyote wakati wa tendo la ndoa.
Wataalamu walisema
kuwa utafiti wao, ambao matokeo yake yalichapishwa katika jarida la kisayansi
la Lancet, ni mfano wa hivi karibuni wa nguvu za mbinu tofauti na za kisasa za
matibabu.
Wanawake hao
walizaliwa na uke ambao haukuwa umeumbika vyema yaani ulikuwa na kasoro ya
maumbile , tatizo linalojulikana kama ‘vaginal aplasia.’
Matibabu ya kisasa kwa
tatizo kama hilo la kiafya yanaweza kuhusisha upasuaji ambapo ngozi au sehemu
ya utumbo inatumika.
Celi zilichukuliwa
kutoka kwa kizazi cha kila wanawake hao ambacho kilikuwa na kasoro ya maumbile
na kukuzwa katika maabara ili kuweza kuzaana.
Picha za kizazi cha
wanawake hao zilitumia kuwarekebishia uke wao.
Hili bila shaka ni
jambo geni katika sayansi ya matibabu na pia inatoa taswira ya mambo
yatakavyokuwa katika siku za usoni.
Jambo la Kutumia celi
za mwili kubadilisha maisha ya wagonjwa tayari limefanyika na kuwasiaidia
wagonjwa kupata kibofu cha mkojo, mishipa ya damu na koo.
Sasa unaweza kuongeza
kwenye orodha hiyo, uke na pua.
Kwa hisani ya BBCSWAHILI
DARAJA LA MTO MZINGA NA KONGOWE KIGAMBONI LAHARIBIKA VIBAYA
Kutokana na mvua kubwa zilizonyesha siku ya jumamosi na jumapili zimeleta athari kubwa kwa wakazi mbalimbali wa jiji la Dar es salaam,ambapo miundombinu na makaazi ya watu yameathiriwa vibaya na mvua hizo na kuacha baadhi ya familia kupoteza ndugu zao na kukatisha usafiri kutoka eneo moja kwenda jingine.
Hili nililishuhudia jana eneo la Mbagala(Darajani mzinga)ambapo jana asubuhi daraja hili lilikuwa linapitika kwa waenda kwa miguu peke yake na kuacha magari na bodaboda kubaki upande uliokuwepo .Pichani ni baadhi ya sehemu hizo korofi.
| Wakazi wa Kongowe wakiangalia maafa yaliyoletwa na Mvua hizo |
| Roli Kubwa la Mafuta lililotumbikia likijaribu kuvuka kwenye Daraja hilo la Kongowe likitokea Kigamboni |
| Sehemu ia daraja iliyoondolewa na maji |
| Wananchi wakijaribu kuvuka kwenda upande wa pili wa daraja baada ya maji ya mto kupungua |
| Add caption |
| Kibao kikionyesha kuwa barabara hiyo imefungwa kwa muda |
| Hapa ni Darajani Mzinga sehemu yalipokuwa yakihifadhiwa mabomba ya gesi |
| Wachina waliokuwa wakiishi eneo hilo wakiokoa vitu vyao |
| Jinsi kulivyokuwa kukionekana |
| Mto Mzinga Umefurika |
| Umati wa watu wakijaribu kuvuka |
| Umati wa watu wakijaribu kuvuka |
| Daraja limefungwa na wananchi wanapita kwa zamu upande mmoja |
Saturday, April 12, 2014
Friday, April 11, 2014
Ukraine yawatuliza wanaotaka kujitenga
![]() |
| Waziri Mkuu wa Mpito wa Ukraine |
Waziri Mkuu wa mpito wa Ukraine Arsenity Yatsenyuk amewaambia viongozi wa
eneo la mashariki mwa nchi hiyo kwamba amekusudia kuwaongezea madaraka zaidi
kwenye eneo hilo.
Hata
hivyo hajafafanua ni kwa kiasi gani atawapa mamlaka hayo na kwamba madaraka
hayo kama yanaweza kuwaridhisha wakazi wa eneo hilo lenye viwanda la Mashariki
mwa Ukraine ambalo linataka kujitenga.
Bwana
Yatsenyuk ameutembelea mji wa Donetsk katika jitihada zake za kushughulikia
msimamo wa waandamanaji wanaounga mkono Urusi ambao wameteka majengo ya
serikali za mtaa na kutangaza uhuru kutoka nchi ya Ukraine.
Wanaharakati
pia wameendelea kushikilia majengo ya serikali katika mji wa Luhansk.
Tayari
Ukraine imeishutumu Urusi kwa kuchochea uvunjifu wa amani nchini Ukraine.
UN yatowa onyo kali kwa serikali ya Burundi
Umoja wa Mataifa umetuma onyo kali kwa Serikali ya
Burundi na kuitaka kuchukua hatua za haraka kushughulikia vurugu za kisiasa na
kuheshimu haki za binadamu. “Tuna imani kwamba serikali ya Burundi
itazingatia haraka iwezekanavyo na kushughulikia (matatizo yote) yanayosababisha
vurugu na ukiukwaji wa haki za bin adamu”, amesema msemaji wa Umoja wa
Matiafa Stéphane Dujarric.
Aidha, umoja huo umebainisha kuwa endapo vitendo vya ukiukwaji wa
haki za binadamu na uchochezi wa vurugu vitaendelea, basi wahusika watawajibika
mbele ya mahakama za kimataifa.
“iwapo hakutochukuliwa hatua, huku ukiukwaji wa haki za binadamu
zikiendelea, hatutosita kuwachukuklia hatua za kisheria wahusika, na
ikiwezekana wafikishwe mbele ya mahakama ya kimataifa wajibu tuhuma
zinazowakabili”, ameendelea kusema Dujarric.
Mshauri maalumu wa Umoja wa Mataifa wa kitengo cha kuzuia mauaji
ya kimbari, Adama Dieng yuko ziarani mjini Bujumbura, ambako atajadili hofu hio
ya kutokea kwa mauaji ya kimbari na viongozi wa Burundi.
Onyo hilo ni miongoni mwa tahadhari ziliyokua zikitolewa hivi
karibuni na Umoja wa Mataifa pamoja na balozi wa Marekani kwenye Umoja wa
Mataifa, Samantha Power.
Akiwa ziarani mjini Bujumbura hivi karibuni, balozi Samantha
Power, aliwatajka viogozi wa Burundi kuheshimu uhuru wa kisiasa, na vilevile
kuheshimu katiba ya nch, ambayo utawala unajaribu kuifanyiya marekebisho.
“ Tunasisitiza kuheshimu katiba ya nchi, ambayo ni sheria
mama ya Burundi, na vilevile kuheshimu haki za binadamu,” alisema Samantha
Power baada ya mazungumzo na rais Pierre Nkurunziza.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, lilielezea aprili mosi
wasiwasi wake, juu ya mvutano wa kisiasa unaoendelea nchini Burundi.
Katika tangazo liliyotolewa jana alhamisi, Baraza la Usalama la
Umoja wa Mataifa, limeelezea kwa mara nyingine wasiwasi wake juu ya uhuru wa
kujieleza na mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa vya upinzani na mashirika
ya kiraia.
Wajumbe 15 wa baraza hilo, wameelezea wasiwasi wao juu “ya vitisho
na kufungwa kiholela pamoja na machafuko yanayotekelezwa na vijana kutoka vyama
vya kisiasa”.
Wajumbe hao wametoa wito kwa serikali ya Burundi kutowafumbia
macho wafuasi wa chama tawala ambao wamekua wakijihusisha na maovu mbalimbali,
mkiwemo unyanyasaji na ukiukwaji wa haki za binadamu.
Kwa wiki kadhaa Umoja wa Mataifa umepata taarifa za kuaminika za
usambazaji wa silaha na sare za kijeshi kwa vijana wa chama tawala
Imbonerakure, shutuma ambazo zimetupiliwa mbali na serikali ya Burundi.
“Ni kweli kwamba kumekuwepo na matukio ya vurugu baina ya
vijana wa vyama mbalimbali vya kisiasa na sio tu chama tawala. Pia hakuna hali
ya kutokuwajibika kwa sababu uchunguzi unafanyika kuhusiana na matukio hayo na
tunapenda kuwaambia wananchi na jumuiya ya kimataifa kuwa nchi ya Burundi
haisanbazi silaha kwa vijana wa chama hicho tawala”, naibu msemaji wa rais
wa Burundi, Willy Nyamitwe.
Burundi inapitia wakati huu mgogoro mkubwa wa kisiasa kutokana na
mgawanyiko kati ya chama cha rais Pirrea Nkurunzia, chenye wahutu wengi na
chama cha UPRONA, chenye watutsi wengi.
Bunge la Burundi lilikataa katikati ya mwezi wa machi kuidhinisha
mswada wa sheria ya kufanya marekebiho ya katiba, ambayo kwa mujibu wa upinzani
ingelisababisha taifa hilo kuingia katika dimbwi la machafuko ya kikabila kama
yale yaliyoshuhudiwa katika miaka ya 1993-2006.
Vyombo vya sheria vya Burundi viliwahukumu hivi karibuni kifungo
cha maisha jela wafuasi 21 wa chama cha upinzani cha MSD kwa kuwatuhumu kwamba
“walianzisha vurugu wakitumia silaha”, baada ya makabiliano na polisi ambayo
iliwakatila wasifanye mazowezi ya kukimbia, wakati vijana wa chama tawala
wamekua wakifanya mazoezi hayo kila jumamosi.
Tuesday, March 11, 2014
Friday, March 7, 2014
MTOTO WA GADDAFI,SAADI ASHIKILIWA LIBYA
Serikali ya Libya imesema kuwa mtoto wa Kiongozi wa
zamani wa nchi hiyo, Saadi Gaddafi, ameondoshwa nchini Niger hivi sasa
anashikiliwa mjini Tripoli.
Saadi alitoroka baada ya baba yake, Kanali Muammar
Gaddafi kuuawa wakati wa mapinduzi yaliyofanyika mwaka 2011 nchini Libya.
Anashutumiwa kuwafyatulia risasi waandamanaji na anadaiwa
kutekeleza uhalifu mwingine wakati wa utawala wa baba yake, yeye alipokuwa
Kiongozi wa vikosi maalum vya kijeshi.
Serikali ya Libya imetoa taarifa hiyo mapema siku ya
alhamisi kuwa wamempokea akitokea Niger.
awali , Niger ilikataa ombi la Libya ilipotaka
imsafirishe Saadi, huku waziri wa sheria wa Niger akihofu kuwa Saadi
atahukumiwa adhabu ya kifo.
MALARIA YAWA UGONJWA HATARI ZAIDI
Watafiti kutoka Uingereza na
Marekani wanasema kuwa mabadiliko ya hali ya hewa huenda yakazua ongezeko kubwa
la maambukizi ya ugonjwa wa Malaria kote duniani huku ugonjwa huo ukienea
katika maeneo ya milimani barani Afrika na Amerika ya Kusini.
Katika matokeo ya utafiti yaliyochapishwa
kwenye jarida la Science, wanasayansi hao wanasema hata ongezeko dogo katika
viwango vya joto siku za usoni huenda likaongeza kwa mamilioni maambukizi ya
malaria.
Mbu anayesababisha malaria.
Watafiti wamepata ushahidi kwamba mbu
anayebeba kimelea kinachosababisha malaria wanaelekea katika nyanda za juu
wakati viwango vya joto vikipanda.
Watu wanaoishi katika maeneo ya nyanda za juu
wanakosa kinga na hivyo kurahisisha maradhi ya malaria kuenea.
Takriban watu milioni mia mbili ishirini kote
duniani huambukizwa ukonjwa wa malaria.
Mbu aneyesababisha malaria
Thursday, March 6, 2014
FOLENI KUBWA MBAGALA MZINGA DARAJANI JANA
Jana Jioni majira ya saa kumi na mbili jioni nilikuwa naelekea maeneo ya Mbagala Kongowe nikakutana na foleni kubwa sana ambayo ilisababishwa na ubovu wa barabara pamoja na magari kutofuata taratibu na sheria barabarani.nilikuwa kwenye bodaboda lakini ilinichuku kama dk 15 hivi kupita kwenye daraja hili kwa jinsi magari yalivyokaa vibaya na kusababisha kufunga njia.
Angalia baadhi ya picha nilizochukua nikiwa kwenye eneo hilo.
| hakuna pa kutokea |
| Hizi ni baadhi ya bodaboda zikiwa kwenye foleni |
Wednesday, March 5, 2014
Monday, February 17, 2014
Monday, January 27, 2014
BONANZA MITAANI
Friday, January 10, 2014
Yaya Toure bingwa wa Afrika
Mchezaji wa Manchester City ambaye pia hucheza nafasi ya kiungo cha kati katika timu ya Ivory Coast, Yaya Toure ndiye mwanasoka bora zaidi mwaka 2013 barani Afrika
Toure alikabidhiwa tuzo la (caf) mwaka wa tatu mfululizo katika sherehe zilizofanyika mjini Lagos, Nigeria Alhamisi usiku.
Taarifa zinazohusianaMichezoAidha Toure pia alishinda tuzo la BBC la mwanasoka bora zaidi barani Afrika mwaka jana.
Alikuwa anawania tuzo hilo dhidi ya mchezaji mwenzake wa Ivory Coast Didier Drogba, ambaye huchezea Galatasaray na John Mikel Obi mnigeria ambaye husakata soka nchini Uingereza.
"nimefurahi sana kwa sababu hii ni ishara kuwa nacheza vyema sana ,'' alisema Toure baada ya kupokea tuzo yake.
Lakini alisema kuwa majaji walikuwa na wakati mgumu kumchagua mchezaji bora kwa sababu washindani wenzake wote ni wazuri.
''Sikudhani kama nitashinda kwa sababu Drogba na Obi Mikel ni wasakataji wazuri wa kabumbu,'' aliongeza Toure.
Washidi wa hivi karibuni wa tuzo ya Caf
2013 Yaya Toure
2012 Yaya Toure
2011 Yaya Toure
2010 Samuel Eto'o
2009 Didier Drogba
2008 Emmanuel Adebayor
2007 Frederic Kanoute
2006 Didier Drogba
Abedi Pele wa Ghana alishinda tuzo hiyo mara tatu kati ya mwaka 1991-93 huku Samuel Eto'o akishinda kati ya mwaka 2003-05.
Bila shaka klabu ya Man City anakosakatia kambumbu Toure, bado haishinda kombe lolote la klabu lakini nyota yake imekuwa iking'aa sana nyumbani na katika nyanja za kimataifa.
Toure ndiye mchezaji pekee wa kiafrika kuwa katika orodha ya wachezaji 23 walioteuliwa kuwania tuzo la mchezaji bora la FIFA mwaka jana.
Mshindani wake wa karibu aliyekuwa pia anawania tuzo la Caf, Mikel, mwenye umri wa miaka 26, alisaidia Nigeria kushinda kombe la taifa bingwa Afrika mwaka 2013 nchini Afrika Kusini.
Taarifa zinazohusiana
Toure alikabidhiwa tuzo la (caf) mwaka wa tatu mfululizo katika sherehe zilizofanyika mjini Lagos, Nigeria Alhamisi usiku.
Taarifa zinazohusianaMichezoAidha Toure pia alishinda tuzo la BBC la mwanasoka bora zaidi barani Afrika mwaka jana.
Alikuwa anawania tuzo hilo dhidi ya mchezaji mwenzake wa Ivory Coast Didier Drogba, ambaye huchezea Galatasaray na John Mikel Obi mnigeria ambaye husakata soka nchini Uingereza.
"nimefurahi sana kwa sababu hii ni ishara kuwa nacheza vyema sana ,'' alisema Toure baada ya kupokea tuzo yake.
Lakini alisema kuwa majaji walikuwa na wakati mgumu kumchagua mchezaji bora kwa sababu washindani wenzake wote ni wazuri.
''Sikudhani kama nitashinda kwa sababu Drogba na Obi Mikel ni wasakataji wazuri wa kabumbu,'' aliongeza Toure.
Washidi wa hivi karibuni wa tuzo ya Caf
2013 Yaya Toure
2012 Yaya Toure
2011 Yaya Toure
2010 Samuel Eto'o
2009 Didier Drogba
2008 Emmanuel Adebayor
2007 Frederic Kanoute
2006 Didier Drogba
Abedi Pele wa Ghana alishinda tuzo hiyo mara tatu kati ya mwaka 1991-93 huku Samuel Eto'o akishinda kati ya mwaka 2003-05.
Bila shaka klabu ya Man City anakosakatia kambumbu Toure, bado haishinda kombe lolote la klabu lakini nyota yake imekuwa iking'aa sana nyumbani na katika nyanja za kimataifa.
Toure ndiye mchezaji pekee wa kiafrika kuwa katika orodha ya wachezaji 23 walioteuliwa kuwania tuzo la mchezaji bora la FIFA mwaka jana.
Mshindani wake wa karibu aliyekuwa pia anawania tuzo la Caf, Mikel, mwenye umri wa miaka 26, alisaidia Nigeria kushinda kombe la taifa bingwa Afrika mwaka 2013 nchini Afrika Kusini.
Taarifa zinazohusiana
Kenya:Al shabaab yapata kipigo
Jeshi la Kenya linalopambana na kundi la wanamgambo la al-Shabaab linasema angalau wapiganaji 30 wa kundi hilo wameuawa Kusini Magharibi mwa Somalia.
Msemaji wa jeshi hilo Meja Emmanuel Chirchir ameelezea kuwa jeshi la Kenya lilishambulia kwa mabomu mojawapo ya kambi za kundi hilo katika eneo la Gedo , Alhamisi Jioni.
Aliongeza kwamba miongoni mwa waliofariki ni makamanda kadhaa wa kundi hilo.
Al Shabaab hata hivyo hawajatoa tamko lolote kuhusu shambulizi hilo.
Kadhalika Al Shabaab walikiri kufanya shambulizi la kigaidi mjini Nairobi mwaka jana dhidi ya jengo la kifahari la Westgate na kuwaua watu 70.
Kenya imekuwa ikipambana na wapiganaji wa kundi hilo tangu mwaka 2011 Oktoba wanajeshi wake walipojiunga rasmi na vikosi vya muungano wa Afrika ambavyo tayari vilikuwa nchini Somalia kwa kazi hiyo.
Rais Uhuru Kenyatta ameahidi kuwa majeshi ya Kenya yataendelea va vita dhidi ya wanamgambao hao tangu waliposhambulia Kenya mwaka jana.
Msemaji wa jeshi hilo Meja Emmanuel Chirchir ameelezea kuwa jeshi la Kenya lilishambulia kwa mabomu mojawapo ya kambi za kundi hilo katika eneo la Gedo , Alhamisi Jioni.
Aliongeza kwamba miongoni mwa waliofariki ni makamanda kadhaa wa kundi hilo.
Al Shabaab hata hivyo hawajatoa tamko lolote kuhusu shambulizi hilo.
Kadhalika Al Shabaab walikiri kufanya shambulizi la kigaidi mjini Nairobi mwaka jana dhidi ya jengo la kifahari la Westgate na kuwaua watu 70.
Kenya imekuwa ikipambana na wapiganaji wa kundi hilo tangu mwaka 2011 Oktoba wanajeshi wake walipojiunga rasmi na vikosi vya muungano wa Afrika ambavyo tayari vilikuwa nchini Somalia kwa kazi hiyo.
Rais Uhuru Kenyatta ameahidi kuwa majeshi ya Kenya yataendelea va vita dhidi ya wanamgambao hao tangu waliposhambulia Kenya mwaka jana.
Wednesday, January 8, 2014
Subscribe to:
Posts (Atom)


















.jpg)
.jpg)
