Maelfu ya raia wa
Afrika Kusini wanaandamana kupinga wimbi la visa vya hivi majuzi vya
mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni.
Mikutano mikubwa imeandaliwa katika mji
mkuu Johannesburg na katika mji wa Port Elizabeth ulioko kusini mwa nchi hiyo
ambao ulishuhudia mashambulio kadhaa dhidi ya wahamiaji wa mataifa ya kigeni
mnamo mwaka 2008.
Makundi ya kiusalama yanafanya misako
katika majumba ya makaazi katika mji wa Alexandra mjini Johannesburg, mahala
ambapo mashambulio kadhaa dhidi ya raia wa kigeni hasa Afrika yalifanyika
katika kipindi cha majuma kadhaa yaliyopita.
Mwaandishi wa BBC anasema kuwa, kuonekana
kwa walinda usalama barabarani kumeleta udhibiti na amani.
Source:bbcswahili.com
No comments:
Post a Comment