Monday, July 1, 2013

Makao ya chama kikuu yavamiwa Misri

Sehemu ya waandamaji
Waandamanaji wanaopinga serikali nchini Misri, wamevamia makao makuu ya chama tawala cha Muslim Brotherhood mjini Cairo.

Inaarifiwa wamepora mali iliyokuwa kwenye ofisi hizo katika mji wa Moqattam wakitupa baadhi ya vitu nje ya madirisha kabla ya kuiteketeza ofisi yenyewe.

Awali, vuguvugu la upinzani lililoandaa maandamano hayo, ambayo yameshuhudia mamilioni ya watu wakijitokeza kuandamana nchini Misri, wametoa makataa kwa rais Morsi hadi Jumanne ajiuzulu.Rais Mohammed Morsi ni rais wa chama hicho cha kiisilamu chenye ushawishi mkubwa.
Taarifa iliyotolewa na kundi hilo, Tamarud au (waasi) ilisema kuwa bwana Morsi huenda akakumbana na raia wasiotii sheria kama njia ya kumuonyesha kuwa wanampinga ikiwa hataondoka mamlakani na kuruhusu uchaguzi kufanyika.
Mamilioni ya watu walihudhuria maandamano, nchini kote Jumapili kumtaka Morsi kuondoka mamlakani.
Pande zote husika zilishangazwa na maandamano yanayofanywa dhidi ya Morsi.
Upinzani ni muungano wa vyama vingi, vikiwemo vianvyomuunga mkono rais aliyeng'olewa mamlakani Mubarak pamoja na watu waliojitolea maisha yao kumuondoa mamlakani.
Changamaoto kwano ni kutafuta njia ya kuendwel;eza maandamno yenyewe hadi wanachokitaka kitakapotimia.
Masemaji wa rais Morsi ameitisha mkutano kati ya pande husika.
Kwa hilo kufanikiwa, rais atahitajika kujitolea na kukubali matakwa yao, ikiwemo hata kufanyia katiba marekebisho.
Hakuonyesha dalili za kutaka mwafaka na wanaompinga, alipokuwa anatoa hotuiba yake wiki jana.
Kwa waandamanaji, wanataka aondoke mamlakani kwa kuitisha uchaguzi wa mapema. Kwa sasa vurugu inaonekana zitaendelea kwa muda.

NI KWELI BARABARA ZA BONGO ZILIPIGWA DEKI KWA AJILI YA UJIO WA OBAMA


Hakikisha mwenyewe kama ni kweli barabara za jijini Dar es salaam zilipigwa deki kwa ajili ya ujio wa Raisi wa Marekani Mh.Barack Obama baada ya kumaliza ziara yake Afrika ya Kusini


URUGUAY VS ITALY HIGHLIGHT

Uruguay vs Italy 2-2 Full Highlights and Penalty Shootout (4-5)

BRAZIL VS SPAIN HIGHLIGHT

Brazil beat Spain in the final of Confederations Cup




Friday, June 28, 2013

Familia ya Mandela yakosoa wanahabari

Mabango ya kumtia moyo Mandela
Taarifa kutoka Ikulu ya Afrika Kusini zinasema kuwa hali ya kiafya ya rais mstaafu Nelson Mandela sio nzuri na kuwa imezorota katika saa 48 zilizopita.
Baada ya kumtembelea hospitalini, mwanawe mkubwa wa kike Makaziwa, alisema hali inaonekana kuwa mbaya lakini akaongeza kuwa Mandela anaweza kuwasikia jamaa zake wanapomuita huku akijaribu kufungua macho yake.

Wamevuka mipaka ya maadili. Wakati hayati Margaret Thatcher alipokuwa mgonjwa mbona sikuona, ukaribu wa vyombo vya habari kiasi ninachokiona kwa banangu? Ni kwa sababu hii ni nchi ya kiafrika. wanahisi kuwa hapa wanaweza kuvuka mipaka wanavyotaka, '' alisema MakaziweMakaziwe amesema “Nimekasirishwa sana. Kwa sababu Mandela ni kiongozi mashuhuri duniani, haimaanishi utu wake udhalilishwe pamoja na kuvuka mipaka kuingilia mambo yake binafsi Hapa naona kuna ubaguzi wa rangi, huku vyombo vingi vya kimataifa vikivuka mipaka, ni kama ndega aina ya Tai au Vulture wanaosubiri Simba kumla mnyama aliomuwinda kisha wakimbilie mzoga.
Mapema leo, Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma alifutilia mbali ziara yake ya kwenda Musumbiji baada ya kumtembelea hospitalini aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela. Rais Zuma amesema kuwa Bwana Mandela yuko katika hali mbali ya afya.
Msemaji wa Zuma Mac Maharaj alisema kuwa hali yake imedorora zaidi
Mandela ambaye, ni rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, amelazwa hospitalini tangu tarehe 8 mwezi Juni akiugua maradhi ya mapafu.
Madaktari wanasemekana kufanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa Mandela anapona.
Vikundi vya watu wenye huzuni mkubwa kuhusu hali ya afya ya Mandela, walikusanyika nje ya hospitali alikolazwa, wakiwa na ujumbe wa ugua pole kwa Mandela
Wadadisi wanasema kuwa wananchi wa Afrika Kusini wanaonekana kuwa tayari kwa habari zozote sasa kuhusu hali ya Mandela.
"tutasikitika sana ikiwa tutapata habari za kifo chake, lakini pia tutakuwa tunasherehekea maisha yake. Amefanya mambo mengi zaidi kwa nchi yetu,'' alisema kijana John Ndlovu, mwenye umri wa miaka 25.
Zuma alitarajiwa kuhudhuria mkutano wa marais nchini Msumbiji, hii leo lakini akaamua kuakhirisha safari yake.
Taarifa kutoka kwa ofisi yake ilisema kuwa anaendelea kuwapongeza wananchi wa Afrika Kusini wanaoendelea kuiombea familia ya Madiba.
Uamuzi wa Rais Zuma kufutilia mbali ziara yake ambako alitarajiwa kuhudhuria mkutano wa kikanda kuhusu uekezaji anaonyesha wazi kuwa hali ya Mandela inaendelea kuzorota zaidi 

Rais Morsi aonya dhidi ya maandamano

Rais wa Misri Mohammed Morsi ameonya kuwa vurugu za siasa zinaathiri demokrasia nchini humo.

Katika hotuba ya taifa kupitia televisheni kuadhimisha mwaka mmoja tangu achukue uongozi, Bw Morsi alikiri kuwa amefanya makosa kadhaa.

Hata hivyo uongozi wake umekumbwa na changamoto si haba ambapo Misri imeshuhudia maandamano ya kila mara kati ya wafuasi na wapinzani wa Morsi.Kadhalika aliutaka upinzani kuwasilisha matakwa yake kupitia kura.
Morsi pia amewonya wale wanaonekana kama wenye njama ya kutaabisha utawala wake na kujairbu kumwendea kichinichini pamoja na kusumbua demokrasia nchini humo.
Wanajeshi wamepelekwa katika miji mikubwa kote nchini kabla ya kufanyika kwa maandamano yanayopangwa dhidi ya utawala wake mwishoni mwa wiki hii.
Hotuba ya bwana Morsi imetolewa wakati makabiliano yakitokea Kaskazini mwa mji wa Mansoura.
Watu wawili waliuawa na wengine 170 kujeruhiwa kwenye mapigano kati ya wafuasi na wapinzani wa serikali, kwa mujibu wa afisaa wa afya.
Morsi anayeongoza chama tawala cha Muslim Brotherhood, alikuwa rais wa kwanza wa taifa hilo kwa chama cha kiisilamu babada ya kushinda uchaguzi mwezi Juni mwaka jana.
Uchaguzi huo ulisifiwa na wengi kuwa huru na wa haki. Mwaka wake wa kwanza mamlakani umekumbwa na maandamano ambayo hayaishi pamoja na uchumi unaodorora.

Chadema wamjibu Waziri Mkuu

Dodoma. Chama cha Maendeleo, Chadema kimeibuka jana bungeni na kusema Serikali inafahamu ukweli wa mlipuko wa bomu uliotokea katika mkutano wa chama hicho jijini Arusha.
Chama hicho kimesema Serikali ilitumia kutokuwepo kwao bungeni kupotosha wananchi kuhusu hali halisi juu ya mlipuko wa bomu hilo uliotokea wakati chama hicho kikihitimisha kampeni zake za uchaguzi mdogo wa udiwani katika Viwanja vya Soweto jijini Arusha, Juni 15, mwaka huu.
Akizungumza kabla ya kuanza kuchangia muswada wa sheria ya fedha ya mwaka 2013/2014, Waziri kivuli wa Nyumba, Ardhi na Maendeleo ya Makazi wa Chadema, Halima Mdee alisema, “Kabla sijaanza kuchangia Mheshimiwa Spika naomba nianze kwa kuwapa pole wakazi wote wa Arusha kutokana na mlipuko wa bomu uliosababisha watu kupoteza maisha, kwani tangu limetokea tukio hilo leo ndiyo nazungumza kwa mara ya kwanza,”
“Tunazilaani kauli potofu zilizotolewa na Serikali hapa bungeni, Serikali inajua nini kilichotokea Arusha na ilitumia kutokuwepo kwetu kupotosha,” alisema.
Source:Mwananchi

Tuesday, June 25, 2013

Hali ya wasiwasi kuhusu afya ya Mandela


Wananchi wa Afrika Kusini hii leo wamekuwa na wasiwasi baada ya rais wa nchi hiyo Jacob Zuma kutangaza kuwa hali ya afya ya rais mstaafu Nelson Mandela sio nzuri sana.
Asubuhi waliamkia kwenda kazini wasijue taarifa watakazopokea hii leo baada ya rais Zuma kutoa taarifa hiyo.
Afisaa mmoja mkuu alisema kuwa raia wa Afrika Kusini wasiwe na matumaini kupita kiasi.Taarifa kutoka ikulu ya rais zilisema Jumapili jioni kuwa Mandela alikuwa amezidiwa ingawa madaktari wanafanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa anapata afueni.
Mandela ambaye alikuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, akiwa na umri wa miaka 94,alipelekwa hospitalini mapema mwezi huu, ikiwa ni mara ya tatu kwake kulazwa hospitalini akiugua ugonjwa wa mapafu mwaka huu.
Rais Jacob Zuma alisema Jumapili kuwa alimzuru Mandela Hospitalini na kuzungumza na mkewe kuhusu hali ya rais mstaafu.
Madaktari wanaomtibu Mzee Nelson Mandela wamesema hali yake imekuwa sio nzuri kwa saa ishirini na nne zilizopita na sasa ni mahututi.
Habari hizo zimekuja kupitia taarifa iliyotolewa na ofisi ya rais ya Afrika Kusini.
Taarifa hiyo imesema bado Mzee Mandela ameendelea kusalia hospitalini mjini Pretoria kwa siku ya kumi na sita akitibiwa mapafu yaliyosababisha tatizo kwenye mfumo wake wa upumuaji.
Rais Jacob Zuma amemtembelea Mzee Mandela na pia kuzungumza na jopo la matabibu wanaomtibu.
Baadaye bwana Zuma alirejea kauli yake ya kulitaka taifa na dunia kumuombea Mzee Mandela apate nafuu.

Wamarekani wamwalika Kabwe Zitto


Dar es Salaam. Mbunge wa Kigoma Kaskazini(Chadema), Zitto Kabwe amealikwa kuhudhuria tamasha la tisa la Aspen mwaka huu, linaliofanyika Marekani.
Tamasha hilo linawajumuisha pamoja watu mashuhuri katika nyanja mbalimbali duniani lengo likiwa ni kuwawezesha kubadilishana mawazo na uzoefu.
Kwa mujibu wa taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Zitto amesema ushiriki wake katika tamasha hilo utamwezesha kukutana na kubadilishana mawazo na magwiji wa masuala mbalimbali duniani.
“Nimefurahi kupata mwaliko huu na nimekubali kushiriki kwa sababu kwangu mimi hii ni nafasi adhimu sana na kupanua uelewa wangu wa masuala mbalimbali, pia ni fursa kubwa ya kueleza maoni yangu kwa waalikwa wenzangu. Nina uhakika kuwa watu nitakaokutana na kubadilishana nao mawazo na uzoefu watasaidia kupanua uelewa wangu wa masuala kadhaa,” alisema Zitto.
Alisema tamasha hilo litaendeshwa litaanza Juni 26 mwaka huu, limegawanyika katika sehemu mbili.
Alisema ya kwanza itahusisha majadiliano ya pamoja, ya vikundi na ya mtu mmoja mmoja.
Source:Mwananchi

Monday, June 24, 2013

Mshtakiwa wa EPA asimulia jinsi wajanja walivyomzidi ‘kete’ kwenye akaunti yake

Mkurugenzi wa Kampuni ya Principal Ltd, Godfrey Mosha amesimulia jinsi Benki ya Akiba Commercial (DCB), tawi la Kariakoo, ilivyoidhinisha malipo ya fedha kwa mtu mwingine kutoka akaunti yake ndani bila yeye kujua.
Mosha ni mmoja wa washtakiwa katika kesi ya  wizi wa fedha kwenye  Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Pamoja na wenzake, Bahati  Mahenge, Manase Makale, Davis Kamungu na Eda Makale, wanakabiliwa na kesi ya wizi wa Sh1.86 bilioni za EPA, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuipitia Kampuni ya Changanyikeni Residential Complex.
Katika kesi hiyo dhidi ya DCB, inayosikilizwa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Warialwande Lema, Mosha anaidai benki hiyo Sh46.8 milioni, zilizolipwa kwa mtu asiyemfahamu kwa kutumia hundi nne tofauti na tarehe tofautitofauti.
Katika ushahidi wake Ijumaa  iliyopita, akiongozwa na Wakili wake, Michael Ngalo, Mosha alidai  alibaini uhamisho huo wa fedha  kutoka  akaunti yake namba 0400438671, Novemba 15, 2011 alipochukua taarifa ya benki.
Alidai kuwa baada ya kubaini uhamisho huo, alikwenda makao makuu ya benki hiyo ambako alimuona Meneja wa Fedha, Vicent Anthony na kumweleza kuhusu tukio hilo wakati yeye hajawahi kuidhinisha uhamisho huo.
“Vicent aliniambia kuwa siyo transfer (uhamisho), bali ni malipo yaliyofanyika kwa kutumia cheque (hundi). Aliniambia namba za hundi hizo na ikaonekana kuwa zililipwa kwa Rafael John Mkwabi, mwenye namba ya akaunti 11000787541,” alidai Mosha na kuongeza:
“Huyo John sijawahi kumwandikia hundi, wala sijawahi kufanya naye biashara, sijawahi kukutanana naye, wala simfahamu.”
Mosha alidai kuwa hundi hizo zilikuwa zimesainiwa na Vicent na Meneja Mkuu, Salehe Ramadhan, huku akidai kuwa saini inayoonekana katika hundi hizo siyo yake.
Alizitaja hundi hizo kuwa ni hundi namba 083722, ya Sh11.6 milioni iliyolipwa Novemba 11, 2011 na  hundi namba 083723 ya Sh9 milioni, iliyolipwa tarehe hiyo.
Nyingine ni  hundi namba 083724 ya Sh14.4 milioni iliyolipwa Desemba 2011, hundi namba 083725 ya Sh11.8 milioni iliyolipwa Desemba 3, 2011.
Aliziwasilisha mahakamani hundi hizo na nyaraka mbalimbali zinazoonyesha saini yake halisi, mahakama ilizipokea kama vielelezo vya ushahidi.
Baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake, Wakili Ngalo alifunga ushahidi na mahakama ilipanga kuendelea na usikilizaji kesi hiyo Julai 8, wadaiwa wataanza kujitetea.

Source:Mwananchi

Friday, June 21, 2013

Mabondia wa Tanzania wafungwa Mauritius

Mabondia waliohukumiwa


Mabondia wanne wa Tanzania wafungwa miaka 15 jela nchini Mauritius kwa makosa ya kuingiza dawa za kulevya aina ya heroin.

Mabondia hao ni Case Ramadhani Fills, Nathanael Elia Charles, Ally Rajabu Msengwa na Petro Charles Mtagwa.
Wakiwa mbele ya Jaji, waliiambia mahakama kuwa walilazimika kuingia katika biashara hiyo haramu kutokana na hali zao za maisha kuwa maskini.Wakati kesi hiyo ilipoanza kusikilizwa, wote walikiri makosa ya kuingiza mihadarati hiyo nchini Mauritius wakati walipokwenda kushiriki mashindano ya ndondi barani Afrika mwaka 2008.
"Tunaomba radhi kwa taifa la Mauritius", waliiambia mahakama.
"Tu watu maskini na tunategemewa na familia, watoto na wazee wetu wanatutegemea."
"Kwa dawa hizi tungepata kiasi cha Pauni £4,000". walisema
Jaji Benjamin Marie Joseph alisema katika kutoa adhabu hiyo yote hayo ameyafikiria, kwani walitoa ushirikiano mzuri wakati wote wa uchunguzi wa kesi hiyo, kulikowezesha hata wafanyabiashara hiyo, raia wa Mauritius kukamatwa.
Wamekuwa mahabusu kwa siku 1,722, sawa na miaka mitano, hivyo watatumikia miaka kumi iliyobakia jela. Pia watatakiwa kulipa faini ya pauni £1,600 na gharama nyingine za uendeshaji wa kesi hiyo.
Kwa mujibu chanzo cha habari nchini Mauritius, Jaji aliwashutumu kwa kuukosea umma wa Mauritius kwa kuingiza dawa hizo za kulevya aina ya heroin.
Mabondia hao waliwasili Mauritius tarehe 10 Juni 2008 na kuweza kupita uwanja wa ndege bila kunaswa hadi walipokamatwa katika hoteli waliyofikia ya Quatre Bornes.
Kwa pamoja walimeza gram 4639.04 za heroin zikiwa katika vifuko 358 vijulikavyo kama pipi.

Wabunge Chadema wasimulia mkong’oto

Mbunge wa Singida Mashariki,Tundu Lissu akiwaonyesha waandishi wa habari miwani yake aliyodai kuvunjiwa na polisi. Lissu alipata dhamana katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Kati, jijini Arusha jana baada ya kukamatwa juzi. Picha na Moses Mashalla 





Arusha/Dar es Salaam. Wabunge wanne wa Chadema, ambao waliachiwa na polisi kwa dhamana wamesimulia mateso waliyoyapata wakiwa rumande baada ya kukamatwa juzi.
Vigogo hao; Mbunge wa Mpanda Mjini Said Amour Arfi, Tundu Lissu (Singida Mashariki), Mustapha Akunaay (Mbulu) na Joyce Mukya (Viti maalumu), walikamatwa juzi baada ya wao na wafuasi wa chama hicho kutawanywa kwa mabomu ya machozi na polisi kwenye Viwanja vya Soweto, Arusha.
Wabunge hao waliachiwa baada ya kujidhamini wenyewe huku watu wengine 65 waliokamatwa pamoja nao wakiachiwa baada ya kudhaminiwa.
Wote wanatakiwa kuripoti kwenye kituo hicho Julai 22, mwaka huu na wataelezwa hatma ya suala hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja alisema jeshi lake linaendelea kuwasaka Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha, Godbless Lema na kuwaonya kuwa wanatakiwa kujisalimisha mara moja.
Chagonja alisema Mbowe na Lema wanatafutwa kwa kosa la kufanya kusanyiko lisilo halali katika viwanja hivyo vya Soweto walipokuwa wakitaka kuomboleza vifo vya watu watatu; Judith Moshi, Ramadhan Juma na Amir Ally waliofariki dunia baada ya kuumizwa kutokana na mlipuko wa bomu, Jumamosi iliyopita.
Pia aliwaamuru Mbowe na Lema kuwasilisha mara moja ushahidi wa kuwahusisha polisi na shambulio la bomu na kama hawana imani na Polisi, basi wawasilishe ushahidi wao kwa Rais Jakaya Kikwete.
Lissu
Lissu, ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alilalamikia kitendo cha polisi kumwagia maji ya kuwasha baada ya kumkamata.
“Walinimwagia maji ya kuwasha kwa mfululizo nikalazimika kulala chini kifudifudi huku nikiwa nimefunika macho kukwepa yasiingie maji. “Kuna askari walitaka kunipiga lakini niliokolewa na mwenzao mmoja aliyenikinga nisishambuliwe. Kwa kweli ilikuwa hali ya hatari,” alisema.
Alisema polisi hao waliomkamata walivunja miwani yake kwa makusudi akisema aliikabidhi kaunta ikiwa haijavunjika.
“Wakati naingia mahabusu nilikabidhi miwani yangu lakini ajabu wakati tukiachiwa ilikuwa imevunjika.” Alilalamikia hatua ya polisi kuwashambulia kwa mabomu, kuwamwagia maji ya kuwasha walipokuwa wakiwatawanya watu waliokusanyika Soweto akisema awali, waliwaruhusu.

Wednesday, June 19, 2013

Polisi yataka ushahidi wa Mbowe, Lema na Nape

Arusha/Dar es Salaam. Jeshi la Polisi limetishia kuwakamata Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na limesema litamhoji Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye baada ya wanasiasa hao kudai kufahamu watu waliohusika na tukio la kurushwa bomu mwishoni mwa wiki iliyopita.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja aliwataka wanasiasa hao kuwasilisha ushahidi wa kile wanachofahamu kuhusu kulipuliwa kwa bomu hilo.
Juzi, Mbowe akiwa na Lema, alisema wana ushahidi wa picha za video zikiwahusisha polisi na kulipuliwa kwa bomu hilo katika Uwanja wa Soweto wakati wa mkutano wa kuhitimisha kampeni za udiwani kwa Chadema, Jumamosi iliyopita.
Mkwara wa Chagonja
Kamishna Chagonja aliwataka Mbowe na Lema kupeleka ushahidi ili kusaidia uchunguzi wa tukio hilo.
“Tunamtaka Mbowe na Lema kutoa ushahidi wa askari wetu kuhusika na tukio la bomu pale Soweto. Wasipofanya hivyo tutatumia sheria kuwalazimisha kufanya hivyo kwani yeyote mwenye ushahidi unaoweza kusaidia upelelezi wa kosa la jinai akikataa kuuwasilisha kwa vyombo husika anaweza kuchukuliwa hatua,” alisema.
Nape naye kuhojiwa
Kwa upande wake, polisi limesema litamhoji Nape ambaye alikaririwa jana akidai kuwa Chadema ndiyo waliohusika na urushaji wa bomu kwenye mkutano wao baada ya kuhisi kushindwa kwenye uchaguzi wa kata nne za Jiji la Arusha.
Kamishna Chagonja alisema watamhoji ili kusaidia kazi yao ya upelelezi. Nape aliihusisha Chadema kwa kauli alizoita za kutishia amani zilizowahi kutolewa siku za nyuma kabla ya uchaguzi wa kata za Arusha.
Watatu wakamatwa
Kamishna Chagonja alisema watu watatu wamekamatwa wakihusishwa na tukio la kulipuliwa kwa bomu mkoani Arusha.
Alisema watuhumiwa hao wanahojiwa na polisi na watafikishwa mahakamani muda wowote ushahidi wa kutosha utakapopatikana au kuachiwa huru wakigundulika kutokuhusika.
Source:Mwananchi

Thursday, June 6, 2013

Uingereza kuwafidia Mau Mau Kenya

Serikali ya Uingereza inatarajiwa kuomba msamaha pamoja na kuwalipa fidia manusura wa harakati za ukombozi wa Uhuru wa Kenya Mau Mau.
Waliokuwa wanachama wa vuguvugu hilo waliwasilisha kesi mahakamani kwa mateso na dhuluma walizodai kutendewa na uliokuwa utawala wa ukoloni miaka ya 50.
Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague, anatarajiwa kutangaza kiwango cha pesa ambazo serikali ya Uingereza iko tayari kutoa kama fidia, duru zikisema kuwa huenda ikawa dola milioni 20
Zaidi ya wakenya 5,000, waliteswa baadhi wakinyanyaswa na waliokuwa wakoloni wa Uingereza.

Uingereza ilipigana vita vikali dhidi ya Mau Mau, waliokuwa wanadai ardhi na kuondoka kwa utawala wa kikoloni.
Manusura wa vita hivyo wamekuwa wakiidai Uingereza kuwalipa fidia kwa miaka mingi.
BBC ina habari kuwa bwana Hague atawaomba radhi waathiriwa wa vita vya Mau Mau, wakati akitangaza kiwango cha pesa watakazotoa kama fidia kwao.

Serikali ya Uingereza awali ilikuwa imesema kuwa madai yote ya vitedno walivyofanya wakoloni ni juu ya serikali ya Kenya tangu kuipa uhuru mwaka 1963 na kuwa kwa sasa haiwezi kutakiwa kulipa.
Lakini mwaka 2011, mahakama iliamuru kuwa, wanaodai fidia, Paulo Muoka Nzili, Wambuga Wa Nyingi na Jane Muthoni Mara, walikuwa na haki ya kudai fidia kutoka kwa Uingereza .

Mawakili wao wanasema kuwa Nzili alihasiwa , huku Bwana Nyingi akichapwa vibaya wakati Bi Mara akiteswa kimapenzi katika kambi za mateso ambako waliokuwa wanapinga ukoloni walikuwa wakifungwa.

Baada ya uamuzi wa kesi hiyo, ilirejeshwa katika mahakama kuu ili kuamua pesa watakazolipwa na ofisi ya jumuiya ya madola.
Habari zinasema kuwa serikali ilikumbwa na wakati mgumu kupata mashahidi na stakabadhi muhimu kuweza kuelezea ukweli katika kesi hiyo.
Lakini Oktoba mwaka jana, mahakama iliamua kuwa waathiriwa waliowasilisha kesi hiyo mahakamani walikuwa na haki ya kufidiwa kwani walikuwa na kesi nzito dhidi ya serikali ya Uingereza.

Watatu hao walikuwa wamesema kuwa wangekubali wahusika wa kesi kuafikiana nje ya mahakama lakini pia walikuwa wanataka kufuata sheria kwani waliona wangepata haki katika mahakama.

Vigogo wanne upinzani wafikishwa mahakamani vurugu za Mtwara

Viongozi wanne wa vyama vya upinzani mkoani Mtwara, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara, wakikabiliwa na mashtaka matatu ikiwamo kula njama, kufanya uchochezi na kuamsha hisia mbaya kwa wakazi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Washtakiwa hao ni Katani Ahmed Katani (33) na Saidi Kulaga (45) wa CUF, Hassan Uledi (35) wa NCCR Mageuzi, Hamza Licheta (51) wa TLP, wote wakazi wa Mtwara.
Awali Katani, Uledi na Licheta walifikishwa mahakamani Mei 31 mbele ya Hakimu Mfawidhi Mwandamizi, Dainess Lyimo, kabla ya kuunganishwa na Kulaga ambaye alikamatwa Juni 2 mwaka huu na kufikishwa mahakamani peke yake Juni 3.
Hata hivyo, juzi washtakiwa wote wanne waliunganishwa na kufikishwa kwa Hakimu Mkazi Mussa Esanju, kutokana na kile kilichoelezwa kuwa Hakimu Lyimo yupo safarini.
Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Justine Sanga, alidai washtakiwa hao kwa pamoja walikutana mahali na muda usiojulikana na kula njama hizo.
Sanga alidai shtaka la pili, Januari 16, mwaka huu eneo la Bima mjini Mtwara, washtakiwa kwa pamoja walidaiwa kufanya makosa ya uchochezi, kwa kutoa hotuba kwa wakazi hao, kwa lengo la kuleta chuki na kusababisha kuharibu mali za umma na binafsi.
Pia, alidai shtaka la tatu Januari 16, mwaka huu eneo la Bima washtakiwa kwa pamoja wanadaiwa kuamsha hisia mbaya, kufanya mikutano ya kisiasa, kutoa maneno makali na kusababisha kuamsha hisia mbaya za wananchi.
Wakili wa utetezi, Banana Biboze aliomba mahakama kumwachia mteja wake, Hassan Uledi, ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro (Mum) kwa ajili ya maandalizi ya mitihani yake Juni 16, mwaka huu.
Hata hivyo, mahakama haitoa dhamana kwa washtakiwa hao kwa kile kilichodaiwa ni kwa ajili ya usalama wa washtakiwa na jamii na kwamba, Hakimu Lyimo anayesikiliza kesi hiyo yupo safarini.
Washtakiwa kwa pamoja walikana mashtaka na kurudishwa rumande hadi Juni 13, mwaka huu.

Source:Mwananchi

Friday, May 24, 2013

Prof Jay: Sitaki hata udiwani!

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Joseph Haule (Profesa Jay) amesema amejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ili kukisaidia chama katika changamoto za kuikomboa nchi.
Akizungumza na Mwananchi jana Profesa J alisema hajajiunga na Chadema ili kugombea ubunge mwaka 2015, isipokuwa kwa dhumuni la kutaka kuongeza nguvu katika chama hicho akiwa kama kijana.
“Kujiunga na siasa si dhambi na haina maana kwamba nina mpango wa kugombea jimbo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Sihitaji kugombea hata udiwani ila ni kwa dhumuni la kutaka kuongeza nguvu katika chama ili kuyafikia malengo,” alisema.
Alisema yeye ni mfuasi wa Chadema tangu mwaka 2005 na amekuwa karibu na chama kwa nyakati nyingi lakini kwa sasa ameamua kuingia rasmi katika chama kama chachu katika kuongeza harakati kwa vijana.
“Nimeingia ili nisaidie hiki chama kuikomboa Tanzania kwani kwa muda mrefu niliokaa katika chama hiki nimegundua kuwa wamedhamiria kumkomboa msanii, kijana wa kawaida na wakubwa kwa wadogo hivyo nadhani nipo sahihi katika uamuzi wangu.”
“Natambua mimi ni mwanamuziki, sawa nina mashabiki wengi lakini haina maana kwamba sina haki ya kuchagua chama ninachoona mimi kinanifaa, lakini siwezi kusita kufanya kazi sehemu yoyote au wakati wowote chama kikinitaka nifanye kwa wakati husika,” alisema Profesa J.
Profesa J juzi alijiunga rasmi na chama hicho baada ya kukabidhiwa kadi ya Chadema mjini Dodoma na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi akiwa sambamba na msanii mwingine wa hiphop Kulwa Kinega maarufu kama K wa Mapacha ambaye alikabidhiwa kadi hiyo na Mbunge wa Ubungo John Mnyika.

 Source:Mwananchi

Thursday, May 23, 2013

Kikwete akemea vikali vurugu Mtwara

Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete amewaonya watu wanaosababisha uvunjifu wa amani nchini humo kuwa watakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Onyo hilo linafuatia ghasia ambapo ofisi kadha, maduka na nyumba zimechomwa katika mkoa wa Mtwara ulioko kusini mashariki mwa Tanzania leo.
Akihutubia kupitia televisheni ya taifa, TBC1, Rais Kikwete amesema wale waliokamatwa na polisi wakati wa ghasia hizo watashitakiwa.
Ghasia hizo zilianza muda mfupi baada ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kuwasilisha bajeti ya wizara yake bungeni. Akizungumzia madai ya waandamanaji hao, Rais Kikwete amesisitiza kuwa raslimali za nchi ni mali ya taifa zima.
Amesema mkoa wa Mtwara haujatelekezwa na kusema kwamba kuna mipango ya kutumia gesi hiyo kujenga viwanda vya mbolea na kutumia gesi hiyo asilia kuzalisha nishati ya umeme kwa mikoa ya Mtwara, Lindi, na Ruvuma ili kuunganishwa katika gridi ya taifa.

Ofisi zachomwa

Kwa mujibu wa mkuu wa polisi wa mkoa wa Mtwara kamanda Linus Sinzumwa, vurugu hizo zimetokea asubuhi ya leo mara baada ya Wizara ya Madini na Nishati kusoma bajeti yake ya makadirio ya mapato na matumizi huko Bungeni mjini Dodoma na kusababisha uharibifu wa mali.
Ametaja uharibifu huo kuwa ni pamoja na kuchomwa kwa majengo ya serikali kama mahakama, nyumba za watendaji wa serikali, baadhi ya majengo ya chama tawala na nyumba za watu binafsi.
Polisi wawasaka waandamanaji Mtwara
Hata hivyo, kamanda huyo, amekanusha taarifa za kuuawa kwa mtu mmoja katika eneo hilo na kubomolewa kwa daraja linalounganisha mji wa Mtwara na maeneo mengine.
Kamanda Sinzumwa amesema watu wapatao tisini na mmoja wanashikiliwa na jeshi na polisi kuhusiana na matukio mbalimbali ya ghasia hizo.
Ghasia hizo, zinahusishwa na madai ya muda mrefu sasa ya wananchi wa mkoa huo kupinga ujenzi wa bomba la gesi iliyogunduliwa mkoani humo kusafirishwa hadi Dar es Salaam, kaskazini mwa Mkoa wa Mtwara, kwa ajili ya kuzalisha nishati ya umeme.
Hii ni mara ya pili mkoani Mtwara kutokea kwa ghasia zinazohusisha maafa kwa binadamu na uharibifu wa mali kama ilivyotokea mapem

Wednesday, May 22, 2013

PROFESA JAY AJIUNGA NA CHADEMA TAYARI KWA KUENDELEZA MAPAMBANO YA KISIASA KAMA MKONGWE SUGU

Rapper mkongwe nchini, Joseph Haule aka Profesa Jay amejiunga rasmi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA.
Profesa amekabidhiwa kadi ya uanachama wa CHADEMA na mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu. 
Kujiunga rasmi kwa Profesa kwenye chama hicho kunaashiria kuwa huenda akawa na nia ya kugombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho mwaka 2015.
 

Tuesday, May 21, 2013

Dragon boy

John Kerry kuzuru mashariki ya kati na Afrika



Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry anatarajiwa kusafiri kwenda katika mataifa ya mashariki ya kati na Afrika kuanzia Jumanne ijayo kwa ziara itakayomchukua hadi Mei 27.
Kerry  anatarajiwa  kuanza ziara  yake  mjini  Muscat  siku ya  Jumanne (21.05.2013), ikifuatiwa  na  Jordan  siku  ya  Jumatano, ambako atakutana  na  kile  kinachoitwa  "washirika  muhimu  wa  kimataifa", kuangalia uwezekano  wa  kupatikana  kwa  suluhisho  la  kisiasa kupitia  majadiliano  nchini  Syria , wizara  ya  mambo  ya  kigeni nchini  Marekani  imesema  katika  taarifa.
Mkutano  huo  unakuja  kabla  ya  mkutano  mkubwa  wa  kimataifa kuhusu  Syria unaopangwa  na  Urusi  na  Marekani , na  ambao unatarajiwa  kufanyika  mwezi  ujao.
Kerry akiwa katika majadiliano na rais Putin wa Urusi
Siku  ya  Alhamis  na  Ijumaa , Kerry anatarajiwa  kuzuru  Jerusalem na  Ramallah  kufuatilia  mazungumzo  juu  ya  kuleta  pamoja  Israel na  Palestina  katika  meza  ya  majadiliano, kujadili amani, taarifa hiyo  imesema.


Pia  siku  ya  Ijumaa , Kerry  anatarajiwa  kusafiri  kwenda  mjini Addis Ababa kushiriki  katika  sherehe  za  siku  mbili  za kuadhimisha  miaka  50  tangu  kuundwa  kwa  Umoja  wa  nchi  za Afrika  OAU, ambao  hivi  sasa   unajulikana  kama  Umoja  wa Afrika, AU. viongozi  kutoka  sehemu  mbali  mbali  za  Afrika watahudhuria  sherehe  hizo.
Hapo  Mei 26 , waziri  Kerry  anapanga  kurejea  mjini  Amman Jordan  kushiriki  katika  jukwaa  la  kiuchumi  la    dunia.
Wakati  huo huo  baraza  la  usalama  la  umoja  wa  mataifa  linatafakari ombi kutoka  kwa  maafisa  wa  ngazi  ya  juu  wa  shirika  la  misaada  la umoja  huo  linalodai  kufikishwa  kwa  misaada  katika  nchi iliyoharibiwa  kwa  vita  ya  syria, hatua  ambayo  inaweza kusababisha  hali  ya  mivutano  baina  ya  Urusi  na  mataifa  ya magharibi  kuhusiana  na  upelekaji  wa  misaada  ya  kiutu  kupitia mipakani, wamesema  wanadiplomasia  wa  Umoja  wa  Mataifa.

Monday, May 20, 2013

NGASSA ASAINI MKATABA WA IAKA MIWILI YANGA KATIKA PICHA





Source:salehjembe.blogspot.com

Assad asisitiza hatajiuzulu

Rais wa Syria Bashir al Assad
 

Rais wa Syria Bashar al Assad amesisitiza kuwa hatajiuzulu kabla ya mwisho wa kipindi chake madaraka mwaka 2014, wakati bomu lililotegwa katika gari liua watu watatu katika mji mkuu Damascus.
"Kujiuzulu ni sawa na kukimbia", Assad amesema katika mahojiano na gazeti moja la Argentina la Clarin wakati alipoulizwa iwapo anaweza kufikiria kujiuzulu kama waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry anavyotaka.
"Sifahamu iwapo Kerry ama yeyote mwingine amepata madaraka ya watu wa Syria kuzungumzia kwa niaba yao juu ya nani anapaswa kuondoka madarakani na nani anapaswa kubaki. Suala hilo litaamuliwa na watu wa Syria katika uchaguzi wa rais mwaka 2014.

Wanne wafa kwenye msongamano kanisani


Waumini kanisani Afrika Magharibi
Watu wanne wamekufa na 13 kujeruhiwa katika mkanyagano ndani ya kanisa la kiavengalisti nchini Ghana.
Ajali hiyo ilitokea pale waumini walipoania kufikia maji matakatifu katika tawi la kanisa la Synagogue Church of All Nations (SCOAN) katika mji mkuu, Accra.
Ripoti zinasema maelfu ya watu walikuwa wamekwenda kanisani humo.
Kanisa hilo liloanzishwa na kasisi wa Nigeria, TB Joshua, ambaye anasema yeye ni mtume.
Pia amezusha utata kwa kudai kuwa anaweza kutibu magonjwa yasiyotibika kama HIV na UKIMWI.

Chuji atwaa tuzo ya SuperSport ya mchezaji bora wa mechi


Dar es Salaam. Kiungo wa Yanga, Athuman Idd ‘Chuji’ ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mechi ya kituo cha SuperSport katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya Simba iliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Chuji alionyesha kiwango cha juu katika mchezo huo ulioshuhudiwa na mashabiki 57,406 kwa kuiunganisha vyema safu ya kiungo ya Yanga.
Baada ya mechi hiyo kituo cha SuperSport kilichoonyesha mechi hiyo moja kwa moja kilimtangaza Chuji kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo na kuwafunika Didier Kavumbagu na Hamisi Kiiza wafungaji wa mabao ya Yanga.
Chuji alisema tuzo hiyo ameipokea kama changamoto kubwa kwake katika kuhakikisha anaendelea kucheza kwa kiwango cha juu siku zote.
“Nimefurahi kusikia hivyo sababu SuperSport ni watu wa mpira na watakuwa wameona uwezo wangu katika mechi hii, lakini hali hiyo naichukua kama moja ya changamoto kwangu,” alisema Chuji. Yaliyostaajabisha kipute cha watani wa jadi kama kawaida ya mtanange wa watani wa jadi yaani  Simba na Yanga huwa haukosi  matukio mageni ambayo huacha simulizi kwa mashabiki.
Haya ni baadhi tu matukio yaliyojiri kwenye mchezo huo uliopigwa mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mwamuzi aanguka, mpira wasimama
Mashabiki wa soka walipigwa na “bumbuwazi” baada ya mwamuzi Martin Saanya aliyekuwa anachezesha mpambano huu wa Simba na Yanga kulala chini ghafla.
Tukio hili ambalo ni nadra kutokea kwenye viwanja  vya soka lilisababisha mpira kusimama kwa muda mrefu, ingawa ilikuja kubainika kwamba alipigwa kiwiko wakati akisuluhisha ugomvi baina na beki Said Nasoro ‘Cholo’ wa Simba na mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu.

Gari la ofisa mwandamizi wa Polisi Arusha lakamatwa likiwa na magunia 18 ya bangi

Gari aina ya Toyota Landcruiser linalotumiwa na Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), Mkoa wa Arusha, lilikamatwa juzi mjini Moshi likiwa limesheheni magunia 18 ya bangi.
Habari za awali zilieleza kuwa gari hilo lilikamatwa juzi saa 4:00 usiku katika Mji mdogo wa Himo, Moshi Vijijini likisafirisha bangi hiyo kwenda Tarakea, Rombo.
Polisi wawili akiwamo dereva wa gari hilo wanashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Himo na gari lipo Makao Makuu ya FFU, Moshi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alithibitisha kukamatwa kwa askari hao: “Mchakato wa kuwafikisha mahakama ya kijeshi unaandaliwa. Bangi hiyo ilikuwa inapelekwa kwa mfanyabiashara mmoja huko Rombo na ndiye aliyewakodi.”
Hata hivyo, Kamanda Boaz alisema atatoa taarifa zaidi leo kwani uchunguzi bado unaendelea.
Bangi ilivyonaswa
Habari zimeeleza kuwa polisi waliokuwa doria waliliona gari hilo likitengenezwa na waliamua kuwauliza wenzao kulikoni? Wakajibiwa kuwa kuna kitu walikuwa wakirekebisha na lilikuwa ni tatizo dogo tu.
“Walipoulizwa kwani mnaelekea wapi wakasema wanapeleka mzigo wa bosi huko Tarakea mpakani na kwa taratibu zetu za kijeshi huwezi kuuliza ni bosi gani,” kilidokeza chanzo kimoja ndani ya polisi.
Hata hivyo, polisi hao wa doria walirudi katika gari yao ili waendelee na doria lakini baadhi ya polisi wakamweleza ofisa aliyekuwapo katika gari hilo kwamba wanashuku gari lile limebeba bangi.
“Lilikuwa na harufu kali ya bangi na hilo ndilo lililowafanya wale polisi kurudi tena kwa wenzao na kuwaambia wanataka waone wamebeba nini ndipo wakakutana na magunia 18 ya bangi,” 
Inadaiwa kuwa baada ya kukuta bangi hiyo, polisi hao waliwasiliana na Mkuu wa Upelelezi (RCO), Mkoa wa Kilimanjaro, Ramadhan Ng’anzi ambaye naye alimjulisha Kamanda Boaz.
Ilielezwa kuwa Kamanda Boaz aliagiza kuwekwa mahabusu kwa polisi hao katika Kituo cha Himo na gari hilo lipelekwe FFU, Moshi.


Source:Mwananchi

Mchungaji Peter Msigwa wa CHADEMA akamatwa na Jeshi la Polisi.

Taaarifa kutoka Iringa zinasema mbunge wa Jimbo la Iringa Peter Msigwa wa CHADEMA amekamatwa na jeshi la polisi muda huu na yuko chini ya Ulinzi wa jeshi hilo.
Mchungaji Msigwa amekamatwa kwa amri ya Kamanda wa Polisi wa mkoa huo Michael Kamuhanda kwa madai kwamba anawaunga mkono wafanyabiashara ndogondogo wa manispaa hiyo Machinga wanaopambana na polisi wanaowakataza kufanya biashara mjini.

Mchungaji Msigwa amekuwa mtetezi mkubwa wa wafanyabiashara ndogondogo kiasi kwamba kila anapoonekana maeneo ya manispaa hiyo hujikuta gari yake ikisukumwa na Machinga hao.

Itakumbukwa ni wiki iliyopita tu mbunge wa viti maalum Chadema Chiku Abwao alimshambulia vikali Waziri William Lukuvi kwamba analitumia jeshi la polisi Iringa kukandamiza Chadema na viongozi wake.

Mchungaji Msigwa ambaye pia ni mbunge machachari wiki iliyopita ametishiwa na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kufikishwa mahakamani kwamba amemtuhumu kufanya biashara haramu ya pembe za ndovu.

Gari la Mbunge Mch.Msigwa kabla ya kukamatwa

Polisi wakitoka kumkamata Mch.Msigwa

Monday, May 6, 2013

Bomu Arusha:raia wa Saudia wanne wakatwa

Polisi nchini Tanzania inawashikilia watu wa nane kwa madai ya kuhusika na mlipuko wa siku ya jumapili katika kanisa Katoliki la Olasit viungani mwa mji wa Arusha.
Miongoni mwa washukiwa ambao wako mikononi mwa polisi ni raia wanne wa Saudi Arabia, na wengine wanne ni raia wa Tanzania.
Idadi ya watu waliofari dunia kufuatia mlipuko huo ni wawili na wala sio watatu kama ilivyoripotiwa hapo awali.
Polisi mjini Arusha vile vile wamethibitisha kuwa waliokufa wakati wa tukio hilo la kigaidi ni wawili.
Kwa wakati huu polisi wanachunguza ni kulipuzi aina gani kilitumika wakati wa shambulizi hilo.
Lakini Baruan Muhuza ambaye alitembelea eneo la tukio mbali na majeruhi hakuna hasara kubwa iliyotokea mahali hapo pia sakafi na kuta za kanisa hilo hazikuchimbika sana.
Watu wawili wamethibitishwa kufariki dunia katika mlipuko huo uliotokea majira ya saa tano asubuhi katika kanisa katoliki la Olasit nje kidogo ya mji wa Arusha nchini Tanzania na wengine kadhaa kujeruhiwa huku balozi wa papa na watawa waliokuwa katika shughuli hiyo maalumu ya uzinduzi wa parokia mpya ya mtakatifu Yosefu mfanyakazi wakinusurika pia .
Kwa mjibu wa Padri Festus Mangwangi ambaye ni paroko msaidizi wa kanisa katoliki jimbo la Arusha mlipuko huo unapotokea walikuwa tayari katika hatua ya kubariki maji kwaajili ya uzinduzi wa kanisa ulikuwa ukiongozwa na balozi wa Papa Fransis.
Hata hivyo Padre Mangwangi amesema kuwa taarifa walizonazo muda mfupi baada ya majeruhi kukimbizwa hospitali watu kati yao wamefariki huku wengine wakiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya Mount Meru mjini Arrusha.
Shughuli zote kuhusiana na ibada hiyo zimesitishwa huku watalaalamu wa milipuko na polisi wakiendelea na uchunguzi kuhusiana na mlipuko huo.
Bado hakuna taarifa zozote kuhusiana na chanzo halisi cha bomu hilo ama kundi lolote linalodaiwa kuhusika na utegaji wa bomu hilo.
Hili ni shambaulio la kwanza la bomu nchini Tanzania japo kuwa mwaka huu pia kulikuwa na mtukio ya mauaji ya Padre wa kanisa hilo visiwani Zanzibar ambaye alipigwa risasi wakati akiwa anajiandaa kuingia kanisani.

Friday, May 3, 2013

SERIKALI YAFUTA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012

Serikali imetangaza kuanzia leo kufuta rasmi matokeo yote ya kidato cha nne mwaka 2012 na mitihani yote itasahihishwa upya kwa kutumia utaratibu ule uliotumika katika matokeo ya mwaka 2011.
Akisoma  bungeni kwa niaba ya Waziri Mkuu ripoti ya awali ya Tume ya kuchunguza kushuka kwa matokeo  ,waziri wa Uratibu na Bunge Williamu Lukuvi amesema hatua hiyo inatokana na uamuzi wa Baraza la Mawaziri ambao waliopokea taarifa ya tume hiyo ambayo imependekeza hatua hiyo.


Kwa mujibu wa Tume hiyo, imependekeza mtihani wa kidato cha nne kusahihishwa upya huku ikiyafuta yale yaliyotangazwa kwa ajili ya kuweka usahihi na njia ya kuelekea kilele cha ubora wa elimu ya Watanzania wote.

Akizungumza Bungeni leo mjini Dodoma, Lukuvi alisema kuwa mitihani hiyo inapaswa kusahihishwa kwa kufuata kanuni ya mwaka 2011, hivyo uamuzi huo umetolewa na Tume ya Waziri Mkuu Pinda aliyounda baada ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kutangaza matokeo ya kidato cha nne huku asilimia 60 ya wanafunzi wote kufeli.

Suala hilo liliibua mtafaruku mkubwa kwa wadau na wanasiasa wa Tanzania, wakililia haki ya mtoto wa Tanzania kusoma, huku wakisema kufeli kwao kutaongeza joto la maisha magumu kwa watoto hao ambao wengi wanatoka kwenye familia masikini.

Taarifa zaidi ya Tume hiyo na uamuzi wako itaendelea kukujia katika blog yako hii, kwa ajili ya kukufikishia habari kamili na namna ya kuwapatia haki ya kupata elimu watoto wa Tanzania.

Kijiwe Ughaibuni-18

Kijiwe 18 from Luke Joe on Vimeo.

KUFA AZIMIO LA ARUSHA:Nyerere alivyotofautiana na Mwinyi

Kumekuwa na mjadala kuhusu sababu za kufa kwa Azmio la Arusha. Azimio hilo lilianzishwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama cha Tanu kikiwa na lengo la kutilia mkazo imani na siasa yake ya Ujamaa na Kujitegemea.
Halmashauri hiyo iliyokutana mjini Arusha Januari 26 - 29, 1967, ilijadili maadili ya viongozi wa umma, Serikali na vyombo vingine, pamoja na wanachama wa Tanu.
Katika maadili ya viongozi wa umma, iliamuliwa kuwa kiongozi wa Tanu (baadaye CCM) au wa Serikali, sharti awe ama mkulima au mfanyakazi na asishiriki katika jambo lolote la kibepari au kikabaila.
Hata hivyo baada ya Mwalimu Julius Nyerere aliyekuwa anasimamia maadili hayo kung’atuka madarakani, misimamo hiyo ilianza kuyeyuka na kupigiliwa msumari wa mwisho huko Zanzibar.
Maamuzi ya Zanzibar
Mwaka 1991 Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi  (CCM) ilikutana mjini Zanzibar na kufanya mabadiliko ya azimio hilo.
Akizungumza na wazee wa chama, viongozi wa Taifa, mashirika ya umma na watu binafsi Februari 25, 1991 jijini Dar es Salaam, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM  hicho na Rais Ally Hassan Mwinyi aliwatoa hofu wale wanaodhani kuwa azio la Arusha linageuzwa.
“Inaelekea kuna hofu kwamba Azimio la Arusha linageuzwa. Kwa hiyo tangu mwanzo, kabla ya kusema lolote, nataka tuelewane kwamba siasa yetu bado ni ile ile ya Ujamaa na Kujitegemea,” anasema na kuongeza:
“Halikugeuka wala hatutazamamii kuligeuza. Kwa hali yoyote sisi wanachama wa Chama cha Mapinduzi hatutaweza kuigeuza siasa hii. Kule Zanzibar tulizungumza mengi, miongoni mwao ni kutoa tafsiri ya baadhi ya vipengele vya Azimio ili vifanane na wakati tulionao.”
Akifafanua zaidi, Mwinyi anasema tangu azimio hilo lilipoanzishwa mwaka 1967 hadi mwaka 1991 ilikuwa imepita zaidi ya miaka 20, hivyo kulikuwa na mabadiliko mengi duniani.
“Hali yetu ya sasa hasa ya kiuchumi, siyo ile ya mwaka 1967. Ndiyo maana mishahara ya wafanyakazi ingawa imeongezeka sana, lakini bado haikidhi mahitaji yao, haiwatoshi hata wale wanaopokea mishahara mikubwa miongoni mwetu,” anasema na kuongeza:
“Isitoshe, wakati wa Azimio idadi ya Watanzania ilikuwa ndogo, sasa hivi idadi yetu imeongezeka zaidi ya mara mbili . Kwa sababu ya wingi wetu, mahitaji yameongezeka sana, wakati mapato yetu yamekuwa yakipungua wakati wote.”
Mwinyi anaongeza kuwa kila zama na mwongozo wake:
“Msahafu wa Waislamu unasema “Likulli ajalin kitab’, yaani kila zama ina kitabu chake,” anasema na kuongeza:
“Sisi wana CCM tunakubali kuwa kila zama zinahitaji kuwa na mwongozo wake. Azimio la Arusha ni mwongozo wetu wa msingi. Ni dira inayoongoza mwelekeo wa jamii yetu. Lakini tafsiri zake inabidi zirekebishwe kila inapohitajika ili zisipitwe na wakati.”
Akisisitiza kuhusu ufafanuzi wa maamuzi ya Zanzibar anasema baada ya kutangazwa kwa azimio la Arusha mwaka 1967 lilifuatiwa na matamko kama vile Azimio la Iringa la mwaka 1971 la ‘Siasa ni Kilimo’ na mwongozo wa mwaka 1981 uliotolewa kwa lengo la kukuza tafsiri ya Azimio la Arusha.
Anaongeza kuwa hata mwaka 1974 kulikuwa na agizo la Musoma kuhusu Elimu ya Kujitegemea.
“Maandiko hayo yote hayakupingana na Azimio la Arusha, ila yaliongeza mambo ambayo yalihitajika yafanane na wakati wake,” anasema.
Akizungumzia sababu ya kuanzishwa kwa Azimio la Arusha mara baada ya nchi kupata uhuru, anasema baadhi ya viongozi walianza kutumia uongozi wao kama mradi wa kujineemesha.
Msimamo wa Nyerere
Licha ya Rais wa awamu ya pili kufafanua umuhimu wa uamuzi wa Zanzibar, bado Mwalimu Nyerere aliendelea kutoridhika kuhusu msimamo mpya wa CCM.
Akizungumza na waandishi wa habari mwaka 1999, Mwalimu Nyerere alisema bado alikuwa hajaona kasoro ya Azimio la Arusha. “Mimi bado natembea nalo (Azimio la Arusha). Nalisoma tena na tena kugundua kama kuna cha kubadili. Labda ningeboresha Kiswahili nilichokitumia, lakini Azimio lenyewe bado ni thabiti. Nisingebadili hata neno moja,” anasema Mwalimu Nyerere.

Source:Mwananchi

260,000 WALIKUFA KWA UKAME SOMALIA

Watoto wengi walikufa kwa Utapia mlo
Takriban watu 260,000 walifariki dunia wakati wa ukame ulioikumba Somalia kuanzia mwaka 2010 hadi 2012, utafiti umebaini.
Nusu ya waliofariki dunia walikuwa ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, inaeleza ripoti ya shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, pamoja Mtandao wa Kuonya Mapema Kuhusu Majanga ya Ukame unaofadhiliwa na Marekani.
Idadi ya vifo ilikuwa kubwa kuliko ile iliyokadiriwa ya watu 220,000 waliofariki wakati wa ukame wa mwaka 1992.
Janga hilo lilisababishwa na ukame mkali, uliochochewa na mapigano kati ya makundi hasimu yaliyokuwa yakigombea madaraka.
Umoja wa Mataifa kwa mara ya kwanza ulitangaza hali ya ukame Julai 2011 katika mikoa ya Somalia ya Bakool uliopo kusini na ule wa chini wa Shabelle, ambayo ilikuwa inadhibitiwa na kundi la wanamgambo wa Al – Shabab wenye mafungamano na Al – Qaeda.
Lakini kundi hilo lilikanusha kuwepo kwa hali hiyo na kuyapiga marufuku mashirika kadhaa ya misaada ya nchi za magharibi kufanya shughuli zake katika maeneo hayo.
Baadaye ukame ulisambaa katika maeneo mengine ukiwemo mkoa wa kati wa Shabelle na Afgoye na katika kambi za watu wasiokuwa na makaazi katika maeneo yaliyokuwa yakidibitiwa na serikali katika mji mkuu Mogadishu.
Mchumi Mwandamizi wa shirika la FAO, Mark Smulders amesema, ukweli kuhusu ukubwa wa janga hilo la kibinadamu umeibuka kwenye utafiti uliofanywa kwa kushirikiana na Mtandao wa Kuonya Mapema Majanga ya Ukame, Fews Net.
“Kwa kawaida, kukadiria vifo wakati wa dharura ni sayansi isiyo rasmi, lakini kutokana na ubora na kiwango cha takwimu zilizokuwepo, tuna uhakika na utafiti huo”, amesema ofisa wa Fews Net Chris Hillbruner.
“Utafiti huo unaeleza kuwa, kilichotokea Somalia ni moja ya majanga mabaya kabisa ya ukame kuwahi kushuhudiwa katika kipindi cha miaka 25 iliyopita, “ ameongeza.
Inakadiriwa kuwa 4.6% ya jumla ya idadi ya watu na 10% ya watoto chini ya umri wa miaka mitano walifariki dunia huko maeneo ya kusini na kati mwa Somalia, imeeleza ripoti hiyo.
“Ripoti hiyo imethibitisha kuwa hatua za ziada zingechukuliwa kabla ya ukame huo haujatangazwa, amesema Phillippe Lazzarini, Mratibu wa Shughuli za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia.
Somalia ilikumbwa na ukame mkali mwaka 2011, ulioathiri zaidi ya watu milioni 13 katika eneo lote la Pembe ya Afrika.
Maelfu ya watu walikimbia makaazi yao wakisaka chakula. Umoja wa mataifa ulitangaza ukame huo kumalizika Februari 2012.
Kwa zaidi ya miaka 20 ya vita vya weyewe kwa wenyewe, Somalia imeshuhudia wababe wa kivita wa koo, wanasiasa mahasimu na vikundi vya wanamgambo vikigombea madaraka, hali iliyoruhusu kushamiri kwa ukosefu wa utawala wa sheria.
Septemba mwaka jana, serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa iliingia madarakani baada ya miaka nane ya utawala wa mpito, hatua iliyoleta utengamano katika baadhi ya maeneo.