Juzi chama hicho kilizindua jimbo la Kanda ya Kaskazini inayojumuisha mikoa ya Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga.
Uzinduzi wa Kanda hiyo umefanyika Jijini Arusha
ambapo mbunge wa Karatu, Israel Natse ameteuliwa kuwa Mwenyekiti huku
Amani Golugwa akiwa Katibu wake.
Katika mahojiano na gazeti hili, Mwenyekiti wa
Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe amefafanua mikakati, malengo na sera
hiyo akisema hailengi kujitenga wala kugawa nchi kama inavyodaiwa
“waliofilisika kisera na kisiasa”.
“Kuwa na Kanda siyo kujitenga, bali ni kusogeza
mfumo na shughuli za chama kila sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania badala ya mtindo uliozoeleka wa kila kitu kuendeshwa kutokea
Dar es Salaam,” anafafanua Mbowe.
Mwenyekiti huyo ambaye ni kiongozi wa kambi rasmi
ya upinzani bungeni, anasema Sera ya Kanda siyo ukabila, akitolea mfano
Kanda ya Kaskazini inayoundwa na watu wa makabila zaidi 25 wenye imani
na dini tofauti.
Anasema sera hiyo itawezesha wanachama wa Chadema
waliotapakaa kila sehemu nchini kupata fursa ya kuonyesha na kutumia
vipaji na uwezo wao wa uongozi katika harakati za kukijenga chama hicho
kikuu cha upinzani.
Anasema mfumo huo utaondoa dhana kuwa Chadema ni
Mbowe, Dk Willibrod Slaa, Zitto Kabwe, Godbless Lema, John Mnyika na
wengine wachache wenye majina kitaifa, badala yake kila mwanachama
atatumia kipaji na uwezo wake pale alipo kukijenga na kukieneza Chadema.
“Kinachotuunganisha na ambacho tunakisimamia kama
chama cha siasa ni Utaifa wetu, umoja, mshikamano na heshima kwa kila
mtu bila kujali dini, imani wala kabila lake,” anasisitiza
Kanda zingine na mikoa inayoziunda kwenya mabano
ni Mashariki (Dar es Salaam na Pwani), Kusini (Lindi na Mtwara, Kati
(Morogoro, Dodoma na Singida), Nyanda za Juu Kusini (Njombe, Iringa,
Mbeya na Ruvuma) na Magharibi inayoundwa na mikoa ya Rukwa, Katavi,
Kigoma na Tabora.
Kanda zingine ni Ziwa Mashariki (Shinyanga, Simiyu
na Mara), Ziwa Magharibi (Mwanza, Geita na Kagera), Pemba (Kusini Pemba
na Kaskazini Pemba) na Unguja (Mjini Magharibi, Kusini Unguja na
Kaskazini Unguja).
Mbowe anasema utekelezaji wa sera na mfumo wa
Kanda kutaiwezesha Chadema kutumia mbinu anazoziita za medani kwa
kushambulia kwa kushtukiza kutoka kila kona bila ‘askari’ wake
kujulikana.
Source:Mwananchi
Source:Mwananchi
No comments:
Post a Comment