Friday, February 8, 2013

MV VICTORIA YANUSURIKA KUUNGUA

Abiria wakiwa ndani ya meli hiyo tayari kwa kuanza safari

Meli ya MV Victoria muda wa saa 3.10 ikiwa inaanza safari kuelekea Bukoba
Meli ya Abiria na Mizigo inayofanya safari zake kati ya jiji la Mwanza na Bukoba imenusurika kuungua majira ya saa9:15 katika bandari ya Mwanza.Moto huo ulianza katika meli hiyo baada ya mafundi wa kucholea waliokuwa wakifanya ukarabati katika meli na cheche kurukia katika madodoro yaliyokuwa katika sehemu ya mizigo.kikosi cha zimamoto kilifika kayika tukio hilo muda mfupi baada ya moto kutokea na kufanikiwa kuuzima moto.meli hiyo ilikuwa ikmewasili kutoka bukoba muda wa asubuhi na ilikuwa inategemewa kufanya safari nyingine usiku wa leo.
Wafanyakazi wa meli hiyo wamelaani kitendo hivho cha meli kufanyiwa ukarabati katikatik ya wiki baada ya mwisho wa wiki.Chuma kilichokuwa kmehifadhi magodoro hayo pamoja na samaki kiliteketea na moto huoambapo mito ya viti yapatayo 400 yaliteketea kabisa.hasara kamili iliyosababishwa ba noto huo bado haijafahamika.Habari zinasema licha ya moto huo kutokea lakini meli hiyo ilifanya safari yake kama kawaida kuelekea Bukoba mnamo muda wa saa 3.10 usiku

No comments:

Post a Comment