Huko
Ujerumani, msemaji wa serikali amesema kuwa anaheshimu kazi kubwa iliyofanywa
na Papa huyu aliyezaliwa katika Jimbo la Bavaria la nchini humo.
Waziri
Mkuu wa Uingereza David Cameron, amemsifu Papa kwa jitihada zake za kuimarisha
mahusiano baina ya Vatican na Uingereza.
Askofu
mkuu wa Canterbury amesema amazipokea taarifa za kujiuzulu kwa Papa kwa huzuni kubwa
ingawa anaelewa undani wa hatua yake.
Kiongozi
wa Ujeremani, Bi. Angela Merkel amesifu mchango wa Papa wa kupendekeza mjadala
baina ya makanisa, waislamu na wayahudi.
Alikumbusha
hotuba ya Papa alipozuru bunge la Ujerumani mnamo mwaka 2011.
Uwamuzi na
hatua ya Papa Benedict XVI wa kujiuzulu mwishoni mwa mwezi huu baada ya
takriban miaka minane akiongoza Kanisa Katoliki kwa hoja kuwa umri wake wa
miaka 85 ni mkubwa kiasi kwamba hawezi kuendelea kuhudumu zaidi ya umri huo.
Makao
makuu ya Kanisa Katoliki huko Vatican yanasema yanatarajia Papa mpya
atachaguliwa kabla ya mwisho wa mwezi wa tatu, na sherehe za Pasaka.
Tabia ya
kujiuzulu kwa Papa si ngeni, ingawa ni tukio jipya katika karne za hivi
karibuni.
Msemaji
wa Vatikani Father Federico Lombardi, amesema kuwa hata wasaidizi wa Papa wa
karibu mno hawakuwa na fununu juu ya tukio hili.
Kaka wa
Papa huyu mzaliwa wa Ujerumani alipewa ushauri na Daktari wake asifanye ziara
nyingine yoyote ya Marekani na kwamba kwa miezi kadhaa Mtakatifu Papa amekuwa
akitafakari kujiuzulu.
Akizungumza
kutoka nyumbani kwake huko Regensburg, Ujerumani, Georg Ratzinger amesema kuwa
Kaka yake alikuwa ameanza kupata shida ya kutembea na kwamba kujiuzulu kwake ni
hatua ya kimaumbile.
Wakati wa
kutawazwa kama Papa, Kadinali Joseph Ratzinger alikuwa mmojawapo wa mapapa
wapya kuchaguliwa akiwa mwenye umri mkubwa wa miaka 78.
Alitangazwa
Papa mnamo mwezi Aprili 2005 kufuatia kifo cha marehemu John Paul wa pili.
Uongozi
wake ulitokea wakati wa wimbi kali la ubakaji kulikumba kanisa katoliki katika
kipindi cha miongo mingi, ubakaji uliofanywa na watawa dhidi ya watoto
wavulana.
Katika
taarifa yake, Mtakatifu Papa amesema: "baada ya kujichunguza binafsi na
nafsi yangu mbele ya Mola wangu, nimefikia uwamuzi kuwa uwezo wangu na afya,
ukiambatana na umri mkubwa, ni mambo yatakayokwaza jitihada zangu za kuendelea
kuliongoza Kanisa Katoliki.
Kuna
kipengele katika sheria ya Kanisa kinachosema kuwa kujiuzulu kwa Papa
kunakubalika iwapo kitendo hicho kimefanywa kwa hiari na kwa utaratibu
unaostahiki.
No comments:
Post a Comment