Shahidi
wa kwanza katika kesi kuhusu wanaume watano waliombaka na kumuua msichana mmoja
nchini India ameanza kutoa ushahidi wake
Marehemu
aliyekuwa na umri wa miaka 23 na mwanafunzi wa chuo kikuu, alishambuliwa vibaya
akiwa ndani ya basi katia mji mkuu wa India lakini alifariki baadaye kutokana
na majeraha aliyoyapa.
Shambulizi
hilo liliwaghadhabisha watu wengi na kuzua mjadala kuhusu dhulma dhidi ya
wanawake.
Mmoja wa
mashahidi wa kwanza kuwasili katika mahakama maalum inayosikiliza kesi hii ya
ubakaji mjini Delhi, alikuwa rafiki ya marehemu aliyekuwa naye usiku wa shambulizi
hilo.
Aliletwa
mahakamani akiwa kwenye kiti cha magurudumu , kwani naye pia alichapwa vibaya
sana washukiwa watano waliokamatwa wote walikataa kosa la mauaji , ubakaji na
kuharibu ushahidi katika eneo la shambulizi.
Upande wa
mashtaka unatarajiwa kuwasilisha mashahidi takriban themanini kuweza wakiwemo
madaktari walimtibu marehemu nchini India na India na Singapore, ambako
alipelekwa kwa matibabu kujaribu kukoa maisha yake.
Kesi hii
inafuatiliwa kwa karibu nchini India ambako ilisababisha maandamano makubwa
kuhusu dhulma wanazotendewa wanawake na namna ambavyo polisi na taasisi za
kisheria hudhughulikia uhalifu wa kijinsia.
No comments:
Post a Comment