VIGOGO watano akiwamo Ofisa wa Usalama wa
Taifa wanashikiliwa polisi, kwa tuhuma za kutaka kusafirisha kontena la
madini aina ya Tantalite yenye thamani ya Dola 22,000 za Marekani
yaliyokuwa yakisafirishwa nje ya nchi.
Akizungumza na Dar es Salaam jana, Waziri wa
Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe aliapa kuilinda Mamlaka ya Bandari
Tanzania (TPA) kwa udi na uvumba.
Kiapo hicho alikitoa jana wakati akiwataja watu
wanaoshikiliwa na polisi kwa kuichafua TPA, wakati yeye akifanya
jitihada za kuisafisha.
Aliwataja watu hao kuwa ni Mfanyakazi wa Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA), Mmiliki wa Kampuni ya Uwakala wa Kusafirisha
Mizigo ya GFC na msaidizi wake.
Wengine ni Ofisa wa Mamlaka ya Ukaguzi Madini (TMAA), Mmiliki wa Bandari Kavu na Ofisa wa Usalama wa Taifa.
Wengine ni Ofisa wa Mamlaka ya Ukaguzi Madini (TMAA), Mmiliki wa Bandari Kavu na Ofisa wa Usalama wa Taifa.
Dk Mwakyembe alisema mzigo huo uliokamatwa ukitaka
kusafirishwa kwenda nje ya nchi, madini yake aina ya Tantalite
hayapatikani nchini, bali nchi za Burundi, Rwanda na Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo.
Alisema walibaini katika nyaraka zinazohusiana na
kusafirishwa kwa madini hayo kuwa, zinaonyesha madini hayo yanatoka
nchini wakati siyo kweli.
Kuhusu Ofisa wa Usalama wa Taifa, Mwakyembe alisema ni mtu muhimu ambaye taifa linamwamini kuficha siri za nchi, lakini akashangaa kuwamo kwenye mlolongo huo.
Kuhusu Ofisa wa Usalama wa Taifa, Mwakyembe alisema ni mtu muhimu ambaye taifa linamwamini kuficha siri za nchi, lakini akashangaa kuwamo kwenye mlolongo huo.
“Yaani sisi tunafanya kazi ya kuisafisha bandari,
watu hawa wanaichafua kuifanya kuonekana ni uchochoro wa kusafirisha
magendo,” alisema Dk Mwakyembe na kuongeza:
“Kutokana na hili, kampuni mbili za meli za
Safmaline na Maikesi zimesitisha kusafirisha mizigo yao, kutokana na
michezo michafu kama hii, watu siyo waaminifu wanabadilisha mizigo
halisi kama madini wao wanaweka simenti au magadi ambayo yana uzito
sawa na mzigo halisi.”
Aliongeza kuwa mmiliki wa Bandari Kavu ya PMM na mtendaji wake mkuu nao pia wanahojiwa polisi kutokana na tuhuma hizo.
Aliongeza kuwa mmiliki wa Bandari Kavu ya PMM na mtendaji wake mkuu nao pia wanahojiwa polisi kutokana na tuhuma hizo.
Kuhusu mfanyakazi wa TRA, Dk Mwakyembe alisema ndiye aliyetoa ridhaa ya mzigo huo kusafirishwa kwa magendo.
Pia, Dk Mwakyembe alisema amewaagiza maofisa wa
polisi kumtafuta raia wa Congo aliyepeleka mzigo huo bandarini, kwa
lengo la kuusafirisha kwenda nchini Romania.
No comments:
Post a Comment