Thursday, January 31, 2013
Wednesday, January 30, 2013
Mwenyekiti mpya Chadema kupatikana Desemba 13
![]() |
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya chama hicho Dar es Salaam jana. Kulia ni Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene. |
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetangaza ratiba ya uchaguzi wake wa ndani, inayoonyesha kuwa kitapata mwenyekiti mpya ifikapo Desemba 13, mwaka huu.
Ratiba iliyotolewa na chama hicho Dar es Salaam
jana imeeleza kuwa uchaguzi huo wa mwenyekiti, utatanguliwa na chaguzi
nyingine za ngazi za majimbo, mkoa, wilaya, kata na tawi.
“Uchaguzi utaanza Aprili, mwaka huu na tunatarajia
umalizike Desemba mwaka huu kwa kumchagua mwenyekiti taifa,” alisema
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John Mnyika.
Alisema kuanzia Aprili hadi Septemba kutafanyika
chaguzi katika ngazi za msingi ambazo zinajumuisha matawi, majimbo na
wilaya kabla uchaguzi huo haujafanyika katika ngazi ya mkoa kuanzia
Novemba.
“Uchaguzi ngazi ya taifa utahusisha pia jumuiya za
chama ambazo ni Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Baraza la Vijana
(Bavicha), Wazee, Kamati Kuu na Baraza Kuu Taifa,” alisema.
Nafasi nyingine zitakazoshindaniwa ni za wajumbe wa mkutano mkuu wa taifa.
Source:Mwananchi
Source:Mwananchi
MGOGORO WA GESI MTWARA:Pinda azima uasi
![]() |
Waziri Mkuu Pinda |
Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Joseph Simbakalia
amewaomba radhi wananchi wa mkoa huo kutokana na kauli Desemba 21, mwaka
jana akiwakebehi baada ya kumwomba apokee maandamano yao ya kupinga
mpango wa kusafirisha gesi hiyo.
Akizungumza katika mkutano wa majumuisho
uliofanyika jana baada ya kusikiliza madai ya wananchi hao kwa siku
mbili mfululizo, Pinda alisema hakuna tone la gesi ghafi
itakayosafirisha kwa njia ya bomba na kusema kiwanda cha kusindika gesi
ghafi kitajengwa katika Kijiji cha Madimba, mkoani humo ili mabaki
yatokanayo na gesi hiyo yatumike kuvutia uwekezaji wa viwanda.
“Wataalamu wanasema gesi haiwezi kwa namna yoyote
ile kusafirishwa kama ilivyo, lazima ibadilishwe kuwa hewa au barafu…
kiwanda cha kusafisha gesi kitajengwa Madimba. Gesi yote itakayotoka
Mnazi Bay itasafishwa hapo na masalia yote yatabaki huku ili kuvutia
viwanda vya mbolea na vingine vinavyotumia malighafi hizo,” alisema
Pinda na kuongeza:
“Kama tungekuwa tunasafirisha gesi ghafi basi hata
kiwanda cha Dangote kisingejengwa hapa… gesi itakayopelekwa Dar es
Salaam ni ile iliyosafishwa kwa ajili ya matumizi ya kuzalisha umeme…
tusaidieni wenzetu kuliokoa Taifa na tatizo la umeme.”
“Gesi lazima isindikwe Mtwara, haitoki hadi
viwanda vije… nadhani hili ni jambo jema lazima tuliwekee utaratibu.
Nikawauliza wataalamu wangu kwani kiwanda cha kusafisha gesi kinajengwa
wapi, wakanijibu Madimba… nikasema kumbe tatizo kubwa ni kutowaeleza vya
kutosha wananchi suala la gesi.” alisema Waziri Mkuu huku akipigiwa
makofi... “Nafikiri tatizo ni sisi Serikali hatukuwa na mpango mzuri wa
kuwaelimisha wananchi.”
Awali, madai ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara yalikuwa
ku pinga usafirishaji wa gesi ghafi kwenda Dar es Salaam wakieleza kuwa
mpango huo utafukuza uwekezaji wa viwanda mkoani humo ambao ungechochewa
na upatikanaji wa malighafi baada ya kusafishwa kwa gesi.
Pia wananchi walipinga uje nzi wa mitambo ya
kuzalisha umeme Kinyerezi, Dar es Salaam wakiitaka Serikali kujenga
mitambo hiyo mkoani Mtwara.
Alitoa wito kwa wabunge wa Mkoa wa Mtwara kufuta
tofauti zao za kisiasa ili waweze kuharakisha maendeleo ya mkoa huo...
“Purukushani hizi ndani ya chama hazina tija, tuseme basi… wabunge
hawaelewani, sasa bungeni wanakwendaje... kila mtu na lake … hebu tuseme
watu kwanza mimi badaaye,” alisema Pinda huku akishangiliwa.
Katika siku hizo mbili mkoani Mtwara, Waziri Mkuu
alikutana na viongozi wa vyama vya siasa, dini, wafanyabiashara,
madiwani na wenyeviti wa mitaa na wanaharakati mbalimbali.
RC aomba radhi
Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa, Simbakalia aliwaomba radhi wakazi wa Mkoa wa Mtwara akisema alipotoka kuwaita wananchi hao wapuuzi na baadaye wahaini kauli ambazo ziliwaudhi wengi
RC aomba radhi
Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa, Simbakalia aliwaomba radhi wakazi wa Mkoa wa Mtwara akisema alipotoka kuwaita wananchi hao wapuuzi na baadaye wahaini kauli ambazo ziliwaudhi wengi
“Kupitia hadhara hii nawaomba radhi kwa kuwakwaza,
nimesikitishwa kwa kauli yangu ambayo imepokewa kwa hisia kwamba
niliwadharau,” alisema Simbakalia.
Baadaye Waziri Mkuu aliwasihi wananchi wa Mtwara
kumsamehe Mkuu wao wa Mkoa wa Mtwara kwa kauli hiyo aliyoitoa 21
Desemba, mwaka jana katika kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa, (RCC), pale
alipoombwa kuyapokea maandamano ya wakazi wa mkoa huo Desemba, 27,
mwaka jana.
Source:Mwananchi
Source:Mwananchi
PICHA ZA LULU AKISHUGHULIKIA DHAMANA YAKE NA BAADAE KUWA HURU
Tuesday, January 29, 2013
Monday, January 28, 2013
Kutoka Baraza Kuu la CHADEMA - Diamond Jubilee Hall
Gesi isiondoke mpaka serikali iiweke wazi mikataba yote kwa wananchi!
- Serikali iende ikae na wananchi na kuwasikiliza ili waridhiane. Kila kitu kisitishwe kwa sasa hadi maridhiano yawepo
- Kinana ni mmojawapo wa Wakurugenzi wa ARTUMAS, imebainika Kinana na CCM wananufaika na mikataba hii
- Wawekezaji wanakaribishwa lakini wawe makini na mikataba ya kifisadi
- Serikali iende ikae na wananchi na kuwasikiliza ili waridhiane. Kila kitu kisitishwe kwa sasa hadi maridhiano yawepo
- Kinana ni mmojawapo wa Wakurugenzi wa ARTUMAS, imebainika Kinana na CCM wananufaika na mikataba hii
- Wawekezaji wanakaribishwa lakini wawe makini na mikataba ya kifisadi
PICHA 8 ZA LULU MAHAKAMANI LEO JAN 28
Mahakama kuu leo imetangaza
dhamana ya mwigizaji Lulu lakini iwapo atatimiza masharti aliyopangiwa
ambayo ni pamoja na kuwasilisha hati yake ya kusafiria, kutosafiri nje
ya Dar es salaam, kujiwakilisha au kuripoti mahakamani kila siku ya
kwanza ya kila mwezi pamoja na wadhamini wake wawili ambao kila mmoja
adhamini kwa shilingi milioni 20 za kitanzania.
Upande wa familia ya Lulu
umesema masharti yote yaliyotajwa wanaweza kuyatimiza leo leo hivyo
wanasubiri tu jibu la msajili ambae ndio anatakiwa kuhakikisha hayo
masharti yametimia kisha ruhusa ya kumkabidhi Lulu kwa familia yake
itolewe.
Taarifa za ndani ni kwamba
uwezekano wa Lulu kuachiwa upo kuanzia january 29 2013 ambayo ni kesho
kwa sababu kuna watumishi wawili wa serikali ambao wapo kikazi mkoani
Pwani na ndio walitakiwa kutia saini dhamana ya Lulu wakiwa ni sehemu ya
masharti.
kwa hisani ya millardayo.com
UNAWAFAHAMU MATAJIRI WATANO TANZANIA?
Anayeongoza katika orodha hiyo ni Bakhressa anayemiliki mali na fedha
zenye thamani ya Dola za Marekani 620 milioni sawa na Sh992 bilioni
(Dola moja Sh1,600) akifuatiwa na Dewji ambaye utajiri wake ni Dola 560
milioni (Sh896 bilioni). Wengine na kiasi cha mali na fedha wanazomiliki
kwenye mabano ni Rostam (Sh672 bilioni- Dola 420 milioni) Mengi
(Sh448bilioni- Dola 280 milioni) na Mufuruki (Sh176 bilioni - Dola 110
milioni).Chanzo cha utajiri wa Bakhressa ni mapato
yanayotokanana uzalishaji wa bidhaa mbalimbali kwenye viwanda vyake.
Gulam Dewji
Mfanyabiashara huyo ana utajiri unaokadiriwa kufikia Dola 560 milioni kutokana na kuzalisha bidhaa na kutoa huduma mbalimbali.
Ni mmoja wa mataikuni wa Tanzania tangu miaka ya 1970 na kazi yake kubwa ilikuwa kuingiza bidhaa mbalimbali kutoka nje.
Mfanyabiashara huyo ana utajiri unaokadiriwa kufikia Dola 560 milioni kutokana na kuzalisha bidhaa na kutoa huduma mbalimbali.
Ni mmoja wa mataikuni wa Tanzania tangu miaka ya 1970 na kazi yake kubwa ilikuwa kuingiza bidhaa mbalimbali kutoka nje.
Alianza na kampuni ndogo aliyoiita Mohammed
Enterprises Tanzania, ambayo kwa sasa ni kati ya kampuni kubwa Afrika
Mashariki na Kati.
Miongoni mwa mali zake ni Kiwanda cha 21st Century Textiles, moja ya viwanda vikubwa vya nguo Kusini mwa Jangwa la Sahara. Kampuni yake ina viwanda vinne, Tanzania na Msumbiji huku ikizalisha Dola 100 milioni kwa mwaka. Pia kampuni hiyo husindika juisi kwa matunda ya Tanzania, mafuta ya kula, sabuni na tishu.
Miongoni mwa mali zake ni Kiwanda cha 21st Century Textiles, moja ya viwanda vikubwa vya nguo Kusini mwa Jangwa la Sahara. Kampuni yake ina viwanda vinne, Tanzania na Msumbiji huku ikizalisha Dola 100 milioni kwa mwaka. Pia kampuni hiyo husindika juisi kwa matunda ya Tanzania, mafuta ya kula, sabuni na tishu.
Kampuni hiyo pia inamiliki kampuni ya bima, makontena, kampuni za kuuza mafuta ya petroli na maduka ya kuuza bidhaa mbalimbali zaidi ya 100 Tanzania nzima.
Hata hivyo, Gulam alisema jana kwamba takwimu zilizotolewa zimekosewa. Alisema kwa sasa yuko nje ya Dar es Salaam na atatoa taarifa sahihi atakaporejea.
“Kuna baadhi ya tarakimu zimekosewa niko Morogoro kuangalia biashara zangu nikirudi Dar es Salaam nitazungumza,” alisema Dewji.
Rostam Aziz
Ameelezwa kuwa utajiri wake umetokana na kuendesha shughuli zake mbalimbali ikiwamo kampuni za mawasiliano ya simu, madini na biashara za usafiri wa meli.
Mwanasiasa huyo mwenye asili ya Asia, alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuwa Mbunge wa Igunga mwaka 1993 na alishinda kwa vipindi viwili.
Aliachana na ulingo wa siasa mwaka 2011. Anamiliki asilimia 19 ya Hisa za Kampuni ya Vodacom ambayo ina wateja zaidi ya milioni nane.
Ameelezwa pia kuwa anamiliki Kampuni ya Ujenzi ya Caspian na sehemu ya Bandari ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Kampuni ya Hutchison Whampoa ya Hong Kong.
Akizungumzia utafiti huo, alisema: “Umefanyika kwa umakini isipokuwa tu kwa upande wangu wanasemas ninamiliki asilimia 19 ya Kampuni ya Vodacom kitu ambacho si sawa kwani ninamiliki asilimia 35.”
Reginald Mengi
Mengi anakimiliki kampuni mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari, viwanda vinavyozalisha vinywaji baridi vya Coca-Cola na ana mgodi wa dhahabu.
Mfanyabiashara huyo baada ya kufanya kazi ya uhasibu ambayo ndiyo taaluma yake, alifanya biashara ya kutengeneza kalamu za wino zilizopata soko kubwa Afrika Mashariki.
Leo hii, IPP Group ambayo Mengi ni mwenyekiti wake, inamiliki magazeti mbalimbali ikiwemo Financial Times, ThisDay na The Guardian, televisheni mbili kubwa Afrika Mashariki na Kati EATV na ITV na vituo vya redio. Anamiliki Kampuni za IPP Gold na Handeni Gold.
Ali Mufuruki
Utajiri wake unatokana na biashara mbalimbali za rejareja na za ushirika.
Ni mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa Tanzania Infotech Investment Group.
Kampuni hiyo inajumuisha Watanzania na Waganda kwa ajili ya kuuza bidhaa za Afrika Kusini za Woolworth.
Utajiri wake unatokana na biashara mbalimbali za rejareja na za ushirika.
Ni mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa Tanzania Infotech Investment Group.
Kampuni hiyo inajumuisha Watanzania na Waganda kwa ajili ya kuuza bidhaa za Afrika Kusini za Woolworth.
Infotech hufanya kazi ya uendelezaji makazi na ukodishaji, matangazo na shughuli za mawasiliano.
Maafa katika ukumbi wa Muziki Brazil
Raia wa
Brazili wanaomboleza vifo vya watu mia mbili thelathini na watatu waliofariki
dunia katika ajali ya moto iliyotokea kwenye ukumbi wa muziki katika mji wa
kusini wa Santa Maria.
Maafisa
wanasema kuwa wengi wa waathiriwa walikuwa ni wanafunzi waliokufa baada ya
kushindwa kupumua kutokana na moshi mkubwa .
Wengine
zaidi ya mia moja wanapata matibabu hospitalini . Serikali ya Brazil imetangaza
siku tatu za maombolezo . Taarifa zinasema kuwa moto huo ulianza wakati
waimbaji wa bendi moja walipowasha fataki.
Maswali
sasa yamekuwa yakiulizwa kuhusu usalama wa kumbui za starehe, huku kukiwa na
madai kuwa cheti cha huduma za zima moto kilikuwa kimepitwa na wakati. Hili ni
jana kubwa la moto kuwahi kuikumba Brazil kwa zaidi ya miongo mitano
Familia
za waathiriwa wamekuwa wakiomboleza juu ya majeneza za jamaa zao katika ukumbi
wa mamozezi ambao unatuimika kama jumba la kuhifadhia maiti.
Kwa
sababu ya heshima kwa waliofariki, serikali iliakhirisha sherehe iliyotarajiwa
kufanyika leo Jumatatu katika mji mkuu, Brasilia, kuadhimisha siku 500, kabla
ya kombe la dunia kungo'a nagna nchini humo mwaka ujao.
Mazishi
ya kwanza mjini Santa Maria yanatarajiwa kufanyika leo , kwa mujibu wa magazeti
ya nchi humo.
Maafisa
wa utawala wametoa majina ya waathiriwa hao,230 huku maiti watatu wakisalia
kutotambuliwa.
Kulingana
na taarifa za kituo cha televisheni cha Globo,wengi wa waathiriwa walikuwa kati
ya umri wa miaka16 na 20.
Zaidi ya
watu 100 wanapokea matibabu baada ya kushindwa kupumua kutokana na moshi
mkubwa.
Lowassa anusurika kifo ajali ya gari
WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amenusurika kifo baada ya gari
lake alilokuwa akisafiria kutoka jijini Dar es Salaam kwenda mkoani
Morogoro, kupata ajali.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana zilieleza kuwa Lowassa alipata ajali hiyo jana saa 2:00 asubuhi baada ya gari lake hilo kugongwa na basi la Moro Best eneo la Bwawani mkoani humo.
Kwa mujibu wa habari hizo ajali hiyo ilitokea baada ya basi la Moro Best lililokuwa likitokea Morogoro kuelekea Dar es Salaam, kujaribu kuyapita mabasi kadhaa na kukutana na gari la Lowassa kisha kuligonga ubavuni.
Hata hivyo, katika ajali hiyo hakuna aliyejeruhiwa na Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli, aliendelea na msafara yake.
Lowassa alikuwa anaelekea Morogoro ambako pamoja na mambo mengine, alishiriki harambee ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Kilakala.
Akizungumzia ajali hiyo kabla ya kufanyika harambee hiyo, Lowassa aliwaeleza waumini kuwa kunusurika kwake katika ajali hiyo ni kwa neema za Mungu tu.
“Mkono wa Mungu ni mkubwa, bila ya hivyo simulizi zingekuwa nyingine juu yangu. Wakati nilipoliona basi likiwa linakuja upande wetu kutugonga, ulinijia wimbo mmoja unaosema ‘’Hivi haya yote ya nini, ni huruma tu,’’ alisema Lowassa.
Akizungumzia tukio hilo Mkuu wa Usalama Barabarani (RTO), Mkoa wa Morogoro, Leonard Gindo alisema taarifa za tukio hilo walizisikia na kuamua kufika eneo la ajali na kukuta vioo vilivyopasuka bila magari kuwepo.
“Hakuna taarifa iliyoripotiwa, lakini tukio hilo lilitokea na kwamba tulifika eneo la tukio na kukuta vioo tu. Inaelezwa kilichotokea ni basi la Moro Best kujaribu kulipita basi lingine na ghafla gari la Lowassa nalo lilikuwa linakuja kwa mbele,” alisema Gindo.
Alisema kuwa taarifa walizozipata ni kuwa magari yote yaliendelea na safari zake baada ya tukio hilo.
“Inasemekana basi la Moro Best liliendelea na safari yake na Lowassa naye aliendelea na safari yake ila vioo tulivyovikuta hatujajua ni vya gari gani,” alisema Gindo.
Kuhusu harambee
Katika harambee hiyo, Lowassa alifanikiwa kuchangisha zaidi ya Sh48 milioni, fedha ambayo ndiyo waliyopanga kuikusanya.
Lowassa alisema yeye na marafiki zake, wanatoa kiasi cha Sh18 milioni ili kuweza kufanikisha shughuli za kanisa hilo.
Alisema anaona faraja kutumia kiasi kikubwa cha fedha zake makanisani na angependa wanaohoji mkakati wake huo kuelewa hivyo.
“Watu wanahoji kwa nini natumia fedha zangu kwenye makanisa, mimi nina Mungu na ninapata faraja kufanya hivi,” alisema Lowassa na kuongeza; Ninachofanya ni kazi ya Mungu.”
Lowassa amekuwa akishiriki katika harambee za ujenzi na shughuli mbalimbali za makanisa nchini tangu alipokuwa Waziri Mkuu.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana zilieleza kuwa Lowassa alipata ajali hiyo jana saa 2:00 asubuhi baada ya gari lake hilo kugongwa na basi la Moro Best eneo la Bwawani mkoani humo.
Kwa mujibu wa habari hizo ajali hiyo ilitokea baada ya basi la Moro Best lililokuwa likitokea Morogoro kuelekea Dar es Salaam, kujaribu kuyapita mabasi kadhaa na kukutana na gari la Lowassa kisha kuligonga ubavuni.
Hata hivyo, katika ajali hiyo hakuna aliyejeruhiwa na Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli, aliendelea na msafara yake.
Lowassa alikuwa anaelekea Morogoro ambako pamoja na mambo mengine, alishiriki harambee ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Kilakala.
Akizungumzia ajali hiyo kabla ya kufanyika harambee hiyo, Lowassa aliwaeleza waumini kuwa kunusurika kwake katika ajali hiyo ni kwa neema za Mungu tu.
“Mkono wa Mungu ni mkubwa, bila ya hivyo simulizi zingekuwa nyingine juu yangu. Wakati nilipoliona basi likiwa linakuja upande wetu kutugonga, ulinijia wimbo mmoja unaosema ‘’Hivi haya yote ya nini, ni huruma tu,’’ alisema Lowassa.
Akizungumzia tukio hilo Mkuu wa Usalama Barabarani (RTO), Mkoa wa Morogoro, Leonard Gindo alisema taarifa za tukio hilo walizisikia na kuamua kufika eneo la ajali na kukuta vioo vilivyopasuka bila magari kuwepo.
“Hakuna taarifa iliyoripotiwa, lakini tukio hilo lilitokea na kwamba tulifika eneo la tukio na kukuta vioo tu. Inaelezwa kilichotokea ni basi la Moro Best kujaribu kulipita basi lingine na ghafla gari la Lowassa nalo lilikuwa linakuja kwa mbele,” alisema Gindo.
Alisema kuwa taarifa walizozipata ni kuwa magari yote yaliendelea na safari zake baada ya tukio hilo.
“Inasemekana basi la Moro Best liliendelea na safari yake na Lowassa naye aliendelea na safari yake ila vioo tulivyovikuta hatujajua ni vya gari gani,” alisema Gindo.
Kuhusu harambee
Katika harambee hiyo, Lowassa alifanikiwa kuchangisha zaidi ya Sh48 milioni, fedha ambayo ndiyo waliyopanga kuikusanya.
Lowassa alisema yeye na marafiki zake, wanatoa kiasi cha Sh18 milioni ili kuweza kufanikisha shughuli za kanisa hilo.
Alisema anaona faraja kutumia kiasi kikubwa cha fedha zake makanisani na angependa wanaohoji mkakati wake huo kuelewa hivyo.
“Watu wanahoji kwa nini natumia fedha zangu kwenye makanisa, mimi nina Mungu na ninapata faraja kufanya hivi,” alisema Lowassa na kuongeza; Ninachofanya ni kazi ya Mungu.”
Lowassa amekuwa akishiriki katika harambee za ujenzi na shughuli mbalimbali za makanisa nchini tangu alipokuwa Waziri Mkuu.
source:Mwananchi
Mkuu wa kaya ilipo gesi anusurika kutekwa, wananchi wachoma moto gari
MKUU wa Kaya ya Msimbati ambako gesi asilia inachimbwa mkoani
Mtwara, Bibi Somoe Mtiti (106) amenusurika ‘kutekwa’ na mtu anayeaminika
na wakazi wa eneo hilo kuwa ni mfanyakazi wa Idara ya Usalama wa Taifa
baada ya wananchi kuvamia gari lake na kuliteketeza kwa moto jana usiku.
Hivi karibuni Bibi Mtiti aliionya Serikali
juu ya mpango wake wa kusafirisha gesi ghafi kwenda Dar es Salaam kwa
madai iwapo itapuuza onyo hilo bomba hilo litasafirisha maji badala ya
gesi iliyokusudiwa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Maria Nzuki alisema hana taarifa zozote kuhusiana na tukio hilo kwa kuwa mhusika hajakwenda polisi kulalamika.
Kwa mujibu wa wanakijiji hao, mtu huyo ambaye ana asili ya kijiji hicho waliyemtambua (jina linahifadhiwa) aliwasili kijijini hapo jana saa 10 jioni akiwa na gari dogo aina ya Mark II na kwenda nyumbani kwa shangazi yake.
Habari zinadai kuwa saa 2 usiku mshukiwa huyo alidaiwa kwenda nyumbani kwa Bibi Mtiti akiwa na gari pamoja na shangazi yake.
“Unajua yule bibi tunamlinda, sasa ilipoonekana ile gari usiku pale, watu wakaanza kujiuliza linafanya nini…wakaanza kusogea, kadiri muda ulivyokuwa unakwenda ndivyo watu walivyozidi kuongezeka,”alisema Juma Ayoub mkazi wa kijiji hicho.
Asha Hamisi ni mtoto wa pili wa Bibi Mtiti, akihadithia juu ya tukio hilo, alisema yapata saa 2 usiku wakiwa wanakula chakula walipokea wageni wawili ambao baada ya kumaliza kula waliomba kuongea na mkuu huyo wa kaya.
“Alikuja kijana na mama wakaniomba kuongea na bibi…alimuuliza bibi kama ana uwezo wa kwenda Mtwara, bibi akajibu hawezi…wakaniuliza mimi kama naweza kwenda badala yake nikawaambia siwezi…akasema ametumwa na Rais Jakaya Kikwete na Hawa Ghasia...wamjie bibi wakazungumze naye mambo ya gesi,” alisema Hamis.
Aliongeza kuwa “Kama bibi yupo tayari Jumanne ijayo watamfuata kwa gari…mimi nikasema sitaki…nilipochungulia nje nikaona watu wengi wamezunguka.”
Kwa upande wa mtoto mwingine wa bibi huyo alisema,” Kwa kuwa tunamfahamu tulimwambia aondoke mpango aliojia haufai, akawa anabisha, tukaendelea kumsihi..wakati huo watu wanazidi kuongezeka…alipotoka akakosea njia, alipopita hakukuwa na njia…watu walimfuata wakaanza kumrushia mawe…aliacha gari akakimbia…ndipo wananchi walipoliteketeza gari kwa moto,” alisema Manzi Mohamedi Faki mtoto wa tano wa Bibi Mtiti.
Shangazi wa mtuhumiwa amethibitisha kumpokea mwanaye huyo na kumsindikiza kwa Bibi Mtiti na ambako alimwomba mkuu huyo wa kaya akubali kuondoka naye kwenda Dar es Salaam kwa maelezo kuwa ametumwa na viongozi wake wa juu.
“Ni mwanangu mtoto wa kaka yangu, alikuja akaniomba nimepeleke kwa bibi akamsalimie tuliondoka saa 2 usiku…watu walituzingira na hali ilipokuwa mbaya niliondoka na kumwacha mwanangu pale, naye alikimbia na ndipo walipochoma moto gari,” alisema shangazi huyo.
Alifafanua kuwa “Huyu mwanangu anaishi Dar es Salaam, anafanya kazi Usalama wa Taifa…nadhani alirudi jana hiyohiyo Mtwara.”
Mwenyekiti wa Kijiji cha Msimbati, Salum Tostao alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa ofisi yake haikupokea mgeni yeyote kutoka serikalini kwa siku hiyo.
“Ni kweli gari limechomwa lenye namba za usajili T 609 BXG mali ya Mussa Babu…taarifa hii ni kwa mujibu wa nyaraka tulizookota kutoka ndani ya gari hilo,” alisema Tostao.
Source:Mwananchi
VURUGU WILAYANI MASASI
![]() |
Haya ni magari yaliyochomwa moto katika vurugu hizo |
![]() |
Majengo pia yalichomwa moto |
Saturday, January 26, 2013
WANAFUNZI WA ST'JOHN WAANDAMANA KUPINGA UBAKAJI NA UZALILISHAJI WANAOFANYIWA
Subscribe to:
Posts (Atom)