Tuesday, January 22, 2013

MH.J.MAKAMBA AZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI WA TTCL



Leo hii nilipozungumza na wafanyakazi wa TTCL. Shirika hili lina changamoto nyingi. Tumezizungumza zote. Tumedhamiria kuliinua Shirika hili. Wafanyakazi wamenikabidhi kabrasha lenye tuhuma dhidi ya uongozi. Nimewasiliana na TAKUKURU na kuliwasilisha kabrasha huko ili uchunguzi ufanyike, na itakapobainika kuna makosa, wahusika wakamatwe na kupelekwa mahakamani. Bodi pia ina nafasi yake katika kuamua kama utaitishwa ukaguzi maalum wa CAG. Katika wiki chache zijazo, tutapata uongozi mpya na pia tunatarijia kuanza mchakato wa kulimiliki Shirika kwa asilimia 100 (kwa sasa AirTel ina hisa asilimia 35 katika TTCL)

No comments:

Post a Comment