Wanamgambo
wa Al-Shabab nchini Somalia wanasema kuwa watamuua jasusi wa Ufaransa Denis
Allex, ambaye Ufaransa ilisema kuwa alikuwa tayari ameuawa wakati jaribio la
kumuokoa lilipotibuka.
Walisema
kuwa Ufaransa inapaswa kulaumiwa ikiwa atauawa. Na pia inapaswa kulaumiwa kwa
mauaji ya makomando wengine wawili waliouawa Ijumaa katika msako uliofanywa
mjini Bulo Marer.
Maafisa
nchini Ufaransa wanasema kuwa waliamini bwana Allex alikuwa ameuawa na mateka
wake wakati wa jaribio la kumuokoa ingawa al-Shabab wanasema hakuwepo hapo
wakati huo.
Hakuna
thibitisho lolote la kifo chake limetolewa hadharani.
Al-Shabab
imetuma picha ya mwili wa komando mmoja, aliyeuawa lakinin sio wa Allex, jina
la kikazi la jasusi huyo ambaye amekuwa akizuiliwa kwa zaidi ya miaka mitatu.
Katika
ujumbe wao kupitia Twitter, al-Shabab walisema ufaransa ndiyo imesababisha
kuuawa kwa Alex kwa sababu ya njama yao ya kutaka kumuokoa.
Waziri wa
ulinzi aliambia idhaa ya redio ya ufaransa, kuwa anaamiini Alex ameuawa tayari,
na kuituhumu Al Shabaab kwa kuchzea hisiasa za watu.
Ufaransa
inasema kwamba makombando wa Ufaransa waliwaua wanamgambo 17 Ijumaa.
Walioshuhudia makabiuliano hayo wanasema kuwa raia kadhaa pia walifariki kwenye
makabiliano hayo.
Waziri wa
ulinzi Jean-Yves Le Drian, alisema Ufaransa ilichukua hatua kwa sababu ya kile
ilichosema ni madai ya kupuuzi yaliyokuwa yanatolewa na Al-Shabab.
No comments:
Post a Comment