Tuesday, January 8, 2013

ASSAD AKOSOLEWA NA MATAIFA KWA HOTUBA YAKE

Taasisi na mataifa mbalimbali duniani yamepinga hotuba ya Rais Bashar al-Assad wa Syria aliyoitoa Jumapili (6.1.2013) na kusema ni lazima angátuke ili kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini mwake.
Katika hotuba hiyo Rais al-Assad amefuta uwezekano wa kuwa na mazungumzo na makundi ya upinzani ambayo ameyaita kuwa ni "vibaraka" wa mataifa ya magharibi na ameapa kuendelea kupambana na "magaidi" na "magenge ya wahuni " wanaotaka kuangusha utawala wake.
Akizungumza katika hotuba yake ya kwanza kwa umma baada ya kipindi cha zaidi ya miezi saba, Rais Assad amewaita wapinzani wake kuwa ni maadui wa wananchi na maadui wa Mungu ambao wameamua kufanya ugaidi.

No comments:

Post a Comment