Taasisi na mataifa mbalimbali duniani yamepinga hotuba ya Rais Bashar
al-Assad wa Syria aliyoitoa Jumapili (6.1.2013) na kusema ni lazima
angátuke ili kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini
mwake.
Katika hotuba hiyo Rais al-Assad amefuta uwezekano wa kuwa na mazungumzo
na makundi ya upinzani ambayo ameyaita kuwa ni "vibaraka" wa mataifa ya
magharibi na ameapa kuendelea kupambana na "magaidi" na "magenge ya
wahuni " wanaotaka kuangusha utawala wake.Akizungumza katika hotuba yake ya kwanza kwa umma baada ya kipindi cha zaidi ya miezi saba, Rais Assad amewaita wapinzani wake kuwa ni maadui wa wananchi na maadui wa Mungu ambao wameamua kufanya ugaidi.
No comments:
Post a Comment