Saturday, January 5, 2013

WAKAZI WA JANGWANI WASEMA KUHAMA KWAO SIO RAHISI


Mamlaka ya hali ya hewa ilitoa taarifa juu ya mvua zinazonyesha na kuwataadharisha wale wakaao mabondeni
wananchi waishio maeneo ya jangawani kata ya mchikichini wanaiomba Serikali iwatengenezewe miundombinu ya sehemu hiyo ili waendelee kuishi katika maeneo hayo.
"kama serikali inaweza kutengeneza barabara na sisi watuzibie huo mto lakini kuhama haitawezekana tutaenda wapi"mmoja wa wakazi hao wa jangwani alisema.
Mjumbewa eneo hilo Bw. Nurdin Omary aliomba serikali itengeneze mfereji kwa kujengea kuta kwenye kingo za mto unaopita eneo hilo .
Wakati huohuo kijiji cha Kunyansulumutu mkoani Mara, mto mara unaopita eneo la wilaya ya serengeti umefurika na watu wanokaa maeneo ya jirani wanaishi juu ya miti,makazi ya wanakijiji hicho wameathirika pamoja na mifungo na mazao yao.hali inaonekana kuwa mbaya sana eneo hilo.

No comments:

Post a Comment