Monday, December 17, 2012

KATIBA MPYA MISRI YAUNGWA MKONO



Rais Mohamed Mursi aungwa mkono na Wamisri katika duru ya kwanza ya kura ya maoni juu ya katiba mpya ambayo anataraji itaitoa nchi hiyo kwenye mzozo wakati wapinzani wakiipinga kwa kukandamiza haki za jamii ya wachache.
 Katika siku ya kwanza ya kura ya maoni juu ya rasimu ya sheria za msingi za nchi hiyo asilimia 56.5 ya kura zimeikubali kwa kura ya ndio. Duru ya pili ya kura hiyo ya maoni hapo Jumamosi ijayo yumkini ikapiga kura nyingine ya ndio kutokana na maeneo mengi yanayotarajiwa kupiga kura hiyo yana wafuasi wa itikadi kali za Kiislamu na hiyo ina maana kwamba katiba hiyo itapita.Lakini wakati kura ya hapana ikiwa ni asilimia 43 jambo ambalo linaloonyesha kukaribiana kwa matokeo hayo hakumpi faraja kubwa Mursi kutokana na mgawanyiko mkubwa katika nchi ambapo anahitaji kuwa na muafaka kwa ajili ya kufanya mageuzi makubwa ya kiuchumi.

No comments:

Post a Comment