Thursday, December 20, 2012

HATIMA YA LEMA KESHO



Hatima ya ubunge wa Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Bw.Godbless Lema itajulikana kesho ambapo majaji watatu  wa Mahakama ya Rufaa itapokaa na kutoa uamuzi juu ya rufaa hiyo,
Rufaa hiyo itasomwa kesho 21.12.12 saa tatu asubuhi katika mahama ya rufaa .
Bw.Lema alivuliwa ubunge mnamo April 5 mwaka 2012 katika hukumu iliyotolewa na Jaji Gabriel  Rwakibalia baada ya kesi iliyofunguliwa na makada 3 wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Bw.Musa Mkanga,Bi.Happy Kivuyo na Bi.Agness Mollel wakipinga ushindi alioupata Bw.Lema katika uchaguzi ulifanyika mwaka 2010

No comments:

Post a Comment