Monday, December 3, 2012

PAPA KUANZA KUTUMIA MTANDAO WA TWITTER



Papa Benedict anafungua akaunti katika mtandao wa kijamii,Twitter, katika jitihada ya kusambaza ujumbe wa kanisa katoliki.
Taarifa kuhusu akaunti hiyo itatolewa baadaye hii leo katika mkutano na waandishi habari, lakini habari kutoka Vatican zinasema huenda asiandike mwenyewe ujumbe kwenye akaunti hiyo.
Wanasema Papa Benedict anapendelea kuandika kwa mkono kuliko kutumia tarakilishi.
Kanisa hilo la katoliki tayari linatumia mitandao kadhaa ya kijamii na hivi karibuni limezindua mtandao mkuu unaounganisha mitandao ya kanisa hilo kote ulimwenguni.
Wakatoliki kote duniani, wataweza kuwasilina na Papa kupitia Twitter wakati akaunti hiyo itakapozinduliwa rasmi.

No comments:

Post a Comment