Thursday, December 13, 2012

AFYA YA NELSON MANDELA YAENDELEA KUIMARIKA



Rais wa kwanza wa Afrika Kusini Nelson Mandela, anayetibiwa kwa ugonjwa wa mapafu, anaendelea vyema na matibabu yake na kwamba hali yake imeimarika.
Bwana Mandela,mwenye umri wa miaka 94, alikimbizwa katika hospitali ya kijeshi, mjini Pretoria, siku ya Jumamosi.
Madaktari wanaomtibu Mandela wameelezea kuridhika na anavyopata nafuu. Hii ni kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa ofisi ya rais Jacob Zuma.
Taarifa za bwana Mandela kuendelea kuwa hospitalini, zimezua wasiwasi nchini Afrika Kusini.
Magonjwa ya mapafu yanaweza kusababishwa na virusi au viini tete. Pia yanaweza kusambazwa kupitia kwa kikohozi au kupiga chafya na yanaweza kuambukizwa kwa kugusa sehemu ambazo mgonjwa amegusa.
Kuna majina tofauti ya magonjwa ikizingatiwa sababu na sehemu ya mwili ambapo ugonjwa ule umeambukizwa.

No comments:

Post a Comment