Tuesday, December 18, 2012
MWENDESHA MASHTAKA MKUU AJIUZURU
Mwendesha mashtaka mkuu wa Misri, Talaat Ibrahim amejiuzulu wadhifa huo
baada ya kukabiliwa na shinikizo la kumtaka ajiuzulu kutoka kwa majaji na
waandamanaji. Wote walikarisirishwa na madai kwamba uteuzi wake mwezi
jana uliofanywa na Rais Momahed Mursi ulihujumu uhuru wa mfumo wa
mahakama nchini humo. Mursi awali alimfuta kazi mtangulizi wa mwendesha
huyo mkuu wa mashtaka, Abdel Maguid Mahmoud. Mahmoud alikuwa
amehudumu kwa miaka mingi katika wadhifa huo chini ya rais wa zamani
Hosni Mubarak ambaye aliondolewa madarakani kufuatia vuguvugu la umma
la kutaka mageuzi mnamo Februari mwaka wa 2011. Kujiuzulu kwa Ibrahim
kunatarajiwa kuwasilishwa mbele ya Baraza Kuu la Mahakama Jumapili ijayo.
Majaji wengi wamelalamika kuhusu amri aliyotangaza Mursi mnamo Novemba
22 iliyomlikimbikizia mamlaka mengi. Hali hiyo ilizusha maandamano ya kitaifa
na mapambano makali kati ya wafuasi wa Mursi na wapinzani wake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment