Tuesday, December 11, 2012

MAZUNGUMZO KATI YA DRC NA M23 YAANZA KAMPALA



Mazungumzo baina ya ujumbe wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo pamoja na waasi wa kundi la M23 yameanza rasmi mjini Kampala Uganda, chini ya usuluhishi wa mwenyekiti wa nchi za kanda ya maziwa makuu.
Mazungumzo hayo yataendelea, licha ya mkasa uliotokea jana, baada ya ujumbe wa waasi kuilaumu serikali ya Kongo kuwa inawafadhili waasi kutoka nchi jirani na walio tishio kwa usalama wa nchi hizo pamoja na raia wa mashariki mwa Kongo.

No comments:

Post a Comment