Wednesday, December 19, 2012

ICC YAMWACHA HURU KIONGOZI WA WAASI



Mahakama ya Kimataifa ya jinai ya ICC, iliyoko The Hague, imemuachilia huru aliyekuwa kiongozi wa waasi Congo, Mathieu Ngudjolo Chui.
Ngudjolo Chui alifikishwa mbele ya mahakama hiyo mwaka wa 2003, kwa tuhuma za uhalifu wa kivita ikiwa ni pamoja na mauaji ya watu 200 katika Kijiji cha Boogoro, iliyo na utajiri mkubwa wa madini, mkoani Ituri, nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Mahakama hiyo ilifahamishwa ripoti kuhusu watu waliouawa kwa kuchomwa, watoto wachanga kuuawa kwa kurusha ukutani na kubakwa na kina mama.
Bwana Ngudjolo, alikanusha madai kuwa aliidhinisha mashambulio hayo, akisema kuwa alifahamu kutokea kwa mauaji hayo siku kadhaa baada ya tukio hilo kutokea.

No comments:

Post a Comment