Katika ujumbe aliomtumia mtangazaji wa Wapo Radio Fm 98.1, Silas Mbise, Lembo amesema kwa jinsi ajali hiyo ilivyotokea ilikuwa wote wafariki duniani lakini Jehovah amewatetea na kutoka salama ingawa mmoja kati ya watu 6 waliokuwemo katika gari hiyo Gastor Sapula damu zilikuwa zikimtoka mdomoni huku Lembo akisikia maumivu katika bega lake.
Ukiacha Lembo na Pascal watu wengine waliokuwemo kwenye gari hiyo ni pamoja na mwinjilisti Jailos Maloda, Gastor Sapula pamoja na vijana wengine wawili waliokuwa sambamba na Pascal kwa uimbaji katika huduma waliyoifanya jijini Mbeya.
Source:gospelkitaa.blogspot.com
No comments:
Post a Comment